Kwa usalama wako usinywe KITOKO

Kwa usalama wako usinywe KITOKO

Mangi flani hivi

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2016
Posts
2,026
Reaction score
3,111
Hii ni kwa wanywaji na wapenzi wa ulabu.

Kuna pombe mpya imeingia mjini inaitwa KITOKO. Hii sio pombe ya kawaida ni hatarious mno. Ipo kwenye vifungashio vya makopo ya plastic yaliyopendekezwa na serikali, Ina rangi nyekundu na imeandikwa kuwa Ina kilevi cha 40%..... Ambao sidhan Kama ni ukweli.

Kwa waliowahi kuionja watakuwa na Simulizi zake tofauti kabisa. Ni pombe ambayo naamini mtengenezaji wake ametengeneza kwa teknolojia ya kizamani kiasi kwamba zile sifa zote za pombe za zamani zipo kwenye hii KITOKO.

Kwanza ni pombe ambayo ukinywa kuna uwezekano mkubwa wa kupigana bar...
Pili unaweza ukajikuta umesahau kwako na kuanza kuzunguka mtaani Kama umelogwa...
Kulala mtaroni ni jambo la kawaida sanaaaaaa.....
Kuongea lugha za kigeni kwa ufasaha ni sifa nyingine ya hii KITOKO.

Nazungumza haya kwa sababu nimeyashuhudia huku nilipo.

Wito:
Naomba Wakati mamlaka husika ikiwamo TFDA wanachunguza viwango vya huu ulabu, wanywaji wenzangu Hebu tuususie kidogo...
Madhara ni Mengi mno.

Naomba kuwasilisha.
 
Hiyo kitoko cha mtoto kajaribu siku moja kuonja double punch au chamukwale ...Utakuja kuleta mrejesho hapa kama hawajaenda kukuokota ununio kawe ukiwa nyang'a nyang'a dadake.
 
Iyo kitoko ilikuwa nchi ya jirani Uganda Tangu miaka ya nyuma ni pombe kama pombe nyingine kali, ila alichokisema Mkuu hapo juu ni uongo maana nilishainywa sana Kampala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni kwa wanywaji na wapenzi wa ulabu.

Kuna pombe mpya imeingia mjini inaitwa KITOKO. Hii sio pombe ya kawaida ni hatarious mno. Ipo kwenye vifungashio vya makopo ya plastic yaliyopendekezwa na serikali, Ina rangi nyekundu na imeandikwa kuwa Ina kilevi cha 40%..... Ambao sidhan Kama ni ukweli.

Kwa waliowahi kuionja watakuwa na Simulizi zake tofauti kabisa. Ni pombe ambayo naamini mtengenezaji wake ametengeneza kwa teknolojia ya kizamani kiasi kwamba zile sifa zote za pombe za zamani zipo kwenye hii KITOKO.

Kwanza ni pombe ambayo ukinywa kuna uwezekano mkubwa wa kupigana bar...
Pili unaweza ukajikuta umesahau kwako na kuanza kuzunguka mtaani Kama umelogwa...
Kulala mtaroni ni jambo la kawaida sanaaaaaa.....
Kuongea lugha za kigeni kwa ufasaha ni sifa nyingine ya hii KITOKO.

Nazungumza haya kwa sababu nimeyashuhudia huku nilipo.

Wito:
Naomba Wakati mamlaka husika ikiwamo TFDA wanachunguza viwango vya huu ulabu, wanywaji wenzangu Hebu tuususie kidogo...
Madhara ni Mengi mno.

tanzania ndo nchi pekee mtu unamuambia mazara ya jambo furani ye anajibu haya cha mtoto mbona dable punch ni kali kuliko iyo utazani mashindano
Naomba kuwasilisha.
 
Yaani Uzi unachekesha aiseeeeh.

Any way, drink at your own risk and eventually die.
 
Back
Top Bottom