digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 7,896
- 14,358
Wakuu habari za Leo?, Nimatumaini yangu kuwa hamjambo.
Naomba kumzungumzia huyu Mgombea wa CHADEMA, mheshimiwa T.A.Lissu, nimejaribu kuhudhuria kampeni zake kama Mara nne hivi lakini hakuna nilichokiambulia tofauti na kusikia habari za risasi kumi na sita kiunoni na mbaya zaidi kampeni nzima unakuta imetawaliwa na neno CCM na Magufuli utadhani kuna vyama viwili tu vinavyoshindana kwenye uchaguzi huu.
Kinacho nifanya niamini kuwa Lissu anapoteza muda wake na itamuwia ngumu kwa chama chake kupata japo wabunge watano ni juu ya tabia yake ya kupinga na kudharau kila kitu kilichofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya tano na hivyo kupelekea kukosa muda wa kuinadi ilani ya CHADEMA.
Ikumbukwe kuwa kudharau juhudi kubwa zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano kumekuwa kukiwakera sana wapiga kura na wengi wamekuwa wakisisitiza kuwa huyu bwana (Lissu ) ajikite kwenye kumwaga sela na ilani ya chama chake.
Mwisho lissu atambue kuwa watanzania wengi wameshamshitukia kuwa kuna nguvu nyuma yake ambayo haina nia njema na taifa la Tanzania pamoja na raslimali zake hivyo kumpa kura Lissu ni kuikabidhi Tanzania na raslimali zake mikononi kwa Mabeberu na baadae kupelekea machafuko katika nchi yetu.
Naomba kumzungumzia huyu Mgombea wa CHADEMA, mheshimiwa T.A.Lissu, nimejaribu kuhudhuria kampeni zake kama Mara nne hivi lakini hakuna nilichokiambulia tofauti na kusikia habari za risasi kumi na sita kiunoni na mbaya zaidi kampeni nzima unakuta imetawaliwa na neno CCM na Magufuli utadhani kuna vyama viwili tu vinavyoshindana kwenye uchaguzi huu.
Kinacho nifanya niamini kuwa Lissu anapoteza muda wake na itamuwia ngumu kwa chama chake kupata japo wabunge watano ni juu ya tabia yake ya kupinga na kudharau kila kitu kilichofanywa na serikali ya CCM ya awamu ya tano na hivyo kupelekea kukosa muda wa kuinadi ilani ya CHADEMA.
Ikumbukwe kuwa kudharau juhudi kubwa zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano kumekuwa kukiwakera sana wapiga kura na wengi wamekuwa wakisisitiza kuwa huyu bwana (Lissu ) ajikite kwenye kumwaga sela na ilani ya chama chake.
Mwisho lissu atambue kuwa watanzania wengi wameshamshitukia kuwa kuna nguvu nyuma yake ambayo haina nia njema na taifa la Tanzania pamoja na raslimali zake hivyo kumpa kura Lissu ni kuikabidhi Tanzania na raslimali zake mikononi kwa Mabeberu na baadae kupelekea machafuko katika nchi yetu.