Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Wana JF,
Mimi nataka kufahamu ni kwa sababu gani Zito Kabwe haandamwi na matatizo ambayo wanapata Viongozi wengi wa CDM?
Mfano:
1. Kwenye tukio la January 5 2011, ilikuwaje hakuwepo kwenye yale maandamano na matatizo yote waliyopata viongozi wa CDM.....
2. Imekuwaje Ubunge wake haupingwi mahakamani kama wanavyosumbuliwa hawa wabunge engine?
3. Imekuwaje majuzi alikuwa mwanza kwenye ule msala wa Kina Kiwia na Machemuli yeye akakosekana?
4. Kama mnakumbuka imekuwaje ubunge wake kaupata kiulani, wakati wengine ni hadi nguvu ya umma kushinikiza?
5. Inakuwaje watetezi wengi wa Ufisadi na CCM wanamtetea kufa na kupona hata humu JF?
Nashindwa kuelewa kwa sababugani yeye amekuwa CDM lakini hajawahi kupata mskike mshike wowote tangu awe kwenye hizi siasa za upinzani wakati watu hadi mapanga wanapigwa... Selo wanawekwa...
Je ni kipi anachoweza kutuaminisha kuwa yeye ni mpiganaji na mtetezi wa wanyonge wakati kina Nelson mandela walikuwa wanakamatwa na kufungwa kwa ajili ya kutetea wananchi..
Tuache ushabiki wa ki CCM tujadili hili.....
Naumiza kichwa nimfahamu vizuri Zitto, nataka niende mbali zaidi ya kufahamu tu dini yake na uhusiano wake na Rostam