Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 9,324
- 15,005
Hivi ni kwa nini sisi Waafrika (wengi) hudhani kwamba mji wetu kuwa na Maghorofa mengi na Marefu ndio Maendeleo? Kwa mfano ni kawaida sana kukuta Mwafrika akifurahia kuona Jengo kubwa lenye Ghrorofa labda 50 likijengwa kwenye mji wake ingawaje hilo Jengo haliwezi kumsaidia yeye au ndugu yake yoyote kitu chochote, yaani kwanza kama likifunguliwa hata kuonekana karibu na hilo jengo Hatoruhusiwa atakamatwa na walinzi, sasa ni Kwa nini huwa tunaona Huo Ufahari kuwa na hilo Jengo?
Kuna watu hasa JF huwa wanapiga mapicha ya mavila yanayojengwa na Wahindi na Wazungu halafu kuja kusifia, ona Masaki mavilaa ya ukweli, lkn ukweli ni kwamba hayo mavila hayana faida yoyote kwake Si ajabu mwenyewe anaishi Sinza kijiweni!
Kuna siku wengine walikuwa wamesimama wanasifu msafara wa JK kwamba ni babu kubwa yaani ma BMW matupu, sasa BMW za JK zinakusaidia nini?
Sasa ni kwanini tuko hivi? Je, IQ ndogo ni ya kulaumu?
Kuna watu hasa JF huwa wanapiga mapicha ya mavila yanayojengwa na Wahindi na Wazungu halafu kuja kusifia, ona Masaki mavilaa ya ukweli, lkn ukweli ni kwamba hayo mavila hayana faida yoyote kwake Si ajabu mwenyewe anaishi Sinza kijiweni!
Kuna siku wengine walikuwa wamesimama wanasifu msafara wa JK kwamba ni babu kubwa yaani ma BMW matupu, sasa BMW za JK zinakusaidia nini?
Sasa ni kwanini tuko hivi? Je, IQ ndogo ni ya kulaumu?