kwa nini simu inahitaji minara mingi?

JAYJAY

JF-Expert Member
Oct 31, 2008
7,492
7,515
nimekuwa nikijiuliza kwa nini simu za mkononi zinahitaji minara mingi tofauti na ile ya redio.karibu maeneo mengi yana minara ya simu lakini minara ya redio sijawahi kuiona huku mitaani lakini bado redio hizo zinasikika karibu maeneo yote. pia nafahamu kuwa redio na simu zote zinatumia electromagnetic waves sasa nini kinasababisha tofauti hii?
 
Lakwanza ni kuwa simu inasend na kureceive, radio inareceive tu.
Transmission capacity ya simu obviously ni ndogo sana ukifananinisha na mnara, so haiwezi kusend mbali.
Pia kila tower ina limited capacity ya kusupport calls kwa wakati mmoja, so kwenye watu wengi inabidi kuwe na towers nyingi ili wote waweze kuongea. Mwisho waves tofauti zina characteristics tofauti pamoja kwamba zote ni electromagnetic waves.
 
nimekuelewa mkuu, maelezo yako yanajitosheleza kabisa!
Lakwanza ni kuwa simu inasend na kureceive, radio inareceive tu.
Transmission capacity ya simu obviously ni ndogo sana ukifananinisha na mnara, so haiwezi kusend mbali.
Pia kila tower ina limited capacity ya kusupport calls kwa wakati mmoja, so kwenye watu wengi inabidi kuwe na towers nyingi ili wote waweze kuongea. Mwisho waves tofauti zina characteristics tofauti pamoja kwamba zote ni electromagnetic waves.
 
nimekuwa nikijiuliza kwa nini simu za mkononi zinahitaji minara mingi tofauti na ile ya redio.karibu maeneo mengi yana minara ya simu lakini minara ya redio sijawahi kuiona huku mitaani lakini bado redio hizo zinasikika karibu maeneo yote. pia nafahamu kuwa redio na simu zote zinatumia electromagnetic waves sasa nini kinasababisha tofauti hii?

Niliwai kujiuliza maswali kama haya na kusoma article na kitabu vilinifafanulia vizuri sana

Ila ngoja nijaribu kueleza kuona kama nilikariri au kuelewa yale niliyoyasoma . teh teh teh teh. Watalama watanikosoa.

Ni hivi
Kimsingi simu ni kama radio kama ulivyosema lakini tofauti yake na radio ni kuwa Radio zimetengenezwa kupokea tu matangazo.(google maneno kama broadcast, Muliticast,unicast uelewe zaidi ) Wakati simu za mkononi zinapokea na zinatakiwa kuwa kuwa uwezo wa kurusha matangazo. Kwa hiyo simu zina transmiiter japo transmiister za kwenye simu uwezo wake ni mdogo sana hivyo kuhitaji retramsiiter ambayo ndio hiyo minara



Kwa lugha nyepesi unaweza kusema kila simu ni kama kituo cha radio lakini transimmiter za kwenye simu za mkononi hazina uwezo( power) kurusha matangazo na hivyo kuhitaji uwepo wa mnara maeneo ya karibu. Ndiyo maana simu zinahitaji kuwa na minara karibu tofauti na radio sabbau radio kazi yake ni kupokea tu wakati simu ili iwe na maana inatakiwa kuwa na uwezo kupokea na kupiga ( transmit).

Sasa power ya simu binasfi haitoshi kurusha mawimbi kutoka kwa mpigaji mpaka kwa mpokeaji bila kupitia kituo fulani( Mnara) na hivyo hivyo power ya reciver kwa mpokeaji haina nguvu ya kumfanya mtu apokee pokea mawasilino bila kupitia kwenye re transmiiter ya karibu(Mnara)

Vile vile kuna uhaba wa frequency.au Masafa.
Mahitaji ya masafa ni makubwa sana kuliko uwezo uliopo. Imebidi zitumiwe mbinu za kuwezesha kitu kinaitwa frequency re use. Kwa hiyo kampuni za simu zinatenga mji katika Cell mbali mbali . kila cell inaweza kutumia frequency fulani. Frequncy iliyotumika inaweza kutumika tena na kituo cha mbali kidogo.

Mfano Cell au mnara wa tigo kijitonyama unaweza kutumia frequency/ masafa ya “x” then mnara wao Posta ukatumia frequency “Y” na mnra wa Uwanja wa ndege ukatumia tena frequency “X” na mnara wa mbagala ukatumia tena frequency Y. Hii inawawezesha kutumia frequency ndogo waliyopewa kuwahudumia wateja wengi.


Hope nimejaribu nikipata ile link ya kitabu na article nilizosma nita kudondoshea hapa.
 
@ kang, asante kwa maelezo mazuri sana.
Pia kwa kuongezea, ni kuwamba katika maeneo yenye watu wengi, minara inawekwa katika mpangilio wa seli (cellular system) kiasi cha minara hiyo kupokezana mara mtu anapokuwa anaongea na simu. Kadri unavyotembea na simu yako kutoka sehemu moja hadi nyingine, ukubwa wa mawimbi unapungua kuzingatia sheria ya kinyume cha kipeo cha pili cha umbali ( inverse square law). Hii inamaanisha kuwa ukienda mbali zaidi, wingi au nguvu za mawimbi zinapungua.
Hivyo ukienda mbali na mnara mmoja, unakaribia karibu zaidi ya mnara unaofuatia, kwa hivyo vipimo vinavyofanyika kati ya simu yako na mtambo kwa kudhibiti minara ( base station controller) vinawezesha mtambo huo kufanya maamuzi ya kukuhamishia kwenye mnara mwingine ulio karibu nawe ili uendelee kutandaa kwa ubora ule ule wa sauti au data.
Kwa maeneo yaliyo mbali lakini yakipokea weak signals kutoka kwenye minara mingi kwa wakati mmoja huku zikiwa mbovu, huwa kunatokea kuruka ruka kwa simu kati ya minara hiyo, hii huitwa ping pong handover. Husababisha mawasiliano kuwa mabovu sana.
Maeneo kama haya endapo yana watu ila si wengi kuwezesha mwekezaji kuweka mnara mwingine kwa hofu ya kuoata kipato (maana mnara mmoja unagharimu si chini ya m300), sehemu hizo hufungwa kikuza mawimbi (repeater).
Kama kuna mtu ataoenda kujua zaidi namna kikuza mawimbi kinavyofanya kazi na aina zake, naweza kutoa somo fupi. Naachia hapo kwa sasa nisiwachoshe maana najua si watanzania wengi wenye kupenda kujua kwa kina sana, ila kama itaonekana kuna wanaopendelea, tunaweza kuendelea tuuuuuu. Pia kama kuna mwenye kuoenda kuvhallenge nilichoandika, namkaribisha sana maana tuko humu kufundisha na kujifunza.
 
lakini mbona minara ni mingi kwenye bara la africa na hasa Tanzania wakati Ulaya au marekani huoni utitiri wa minara? au ndo tunatumia outdated technologies?
 
lakini mbona minara ni mingi kwenye bara la africa na hasa Tanzania wakati Ulaya au marekani huoni utitiri wa minara? au ndo tunatumia outdated technologies?

Technolojia more or less ni ile ile sema wenzetu wako clever kidogo.

4b94b59f-ed07-4d7d-9ee1-64ea81ca15d1.jpg

Disguised Cell Towers - A Waymarking.com Category
 
@ kang, asante kwa maelezo mazuri sana.
Pia kwa kuongezea, ni kuwamba katika maeneo yenye watu wengi, minara inawekwa katika mpangilio wa seli (cellular system) kiasi cha minara hiyo kupokezana mara mtu anapokuwa anaongea na simu. Kadri unavyotembea na simu yako kutoka sehemu moja hadi nyingine, ukubwa wa mawimbi unapungua kuzingatia sheria ya kinyume cha kipeo cha pili cha umbali ( inverse square law). Hii inamaanisha kuwa ukienda mbali zaidi, wingi au nguvu za mawimbi zinapungua.
Hivyo ukienda mbali na mnara mmoja, unakaribia karibu zaidi ya mnara unaofuatia, kwa hivyo vipimo vinavyofanyika kati ya simu yako na mtambo kwa kudhibiti minara ( base station controller) vinawezesha mtambo huo kufanya maamuzi ya kukuhamishia kwenye mnara mwingine ulio karibu nawe ili uendelee kutandaa kwa ubora ule ule wa sauti au data.
Kwa maeneo yaliyo mbali lakini yakipokea weak signals kutoka kwenye minara mingi kwa wakati mmoja huku zikiwa mbovu, huwa kunatokea kuruka ruka kwa simu kati ya minara hiyo, hii huitwa ping pong handover. Husababisha mawasiliano kuwa mabovu sana.
Maeneo kama haya endapo yana watu ila si wengi kuwezesha mwekezaji kuweka mnara mwingine kwa hofu ya kuoata kipato (maana mnara mmoja unagharimu si chini ya m300), sehemu hizo hufungwa kikuza mawimbi (repeater).
Kama kuna mtu ataoenda kujua zaidi namna kikuza mawimbi kinavyofanya kazi na aina zake, naweza kutoa somo fupi. Naachia hapo kwa sasa nisiwachoshe maana najua si watanzania wengi wenye kupenda kujua kwa kina sana, ila kama itaonekana kuna wanaopendelea, tunaweza kuendelea tuuuuuu. Pia kama kuna mwenye kuoenda kuvhallenge nilichoandika, namkaribisha sana maana tuko humu kufundisha na kujifunza.

Aah Mkuu mimi ningependa kujua zaidi kuhusu hizi repeater....na especially gharama zake...Natoka kijiji kimoja huko songea ambapo mawasiliano ya simu hayafiki...(signal inapatikana kama 40-50Km away from the village); mnara tumeomba lakini wahusika wanaona hailipi!!
Je tunaweza kutumia hizi repeaters??
 
Na mimi nachangia kama ifuatavyo,
mawimbi ya simu na ya radio ni tofauti.
Simu inatumia mawimbi aina ya microwave ambayo yana madhara katika protin aka mtu
hivyo kulingana na athari wame yadogosha mawimbi ya simu ili madhara yawe madogo.
Baada ya kudogeshwa hayo mawimbi yakapelekea mawasiliano yawe hafifu maana wave za kwenye simu ni low range hazifiki mbali sana.
Kuboresha mawasiliano wakaweka minara mingi kwa ku target user.
Kingine minara hiyo ni switch yaani mnara mmoja unapokea mawasiliano kutoka mnara mwengine na kupasiana mnara hadi mnara.
Kama ukiwa mbali na mnara ukatumia simu inakuwa inafanya kazi kubwa na kutumia nguvu nyingi.
 
Mbona nchi za wenzetu minara ya simu haizagai ovyo kama bongo??

Minara ipo sema wanaiweka katika design amabyo ni kama si ya kuvutia basi ni ya kificho. kama jamaa lvyoweka hapo juu hiyo picha ni mnazi artificial lakini una vifaa vya vya simu
dzn_sq2_FutureFlower03HcAnnaLiu01.jpg



mesa-del-sol.jpg


pine-tree.jpg



Kwa hiyo hata wakiweka vifaa vyao kwenye majengo mrefu wanavifweka kwa njia amabayo mtu unaweza usijue kama ni tower ya simu. Unaweza kuona kitu kwenye jengo kama tanki la maji kumbe ndo wamemaliza.

Art+ Design+ engineering= ????
 

Attachments

  • dzn_sq2_FutureFlower03HcAnnaLiu01.jpg
    dzn_sq2_FutureFlower03HcAnnaLiu01.jpg
    23.3 KB · Views: 51
Jibu langu ningesema ni tatizo la kiteknologia ndo linasababisha minara ya simu iwe mingi kuliko ya radio... Ingawa sina utaalam wa aina yoyote. Jibu langu nalilinda na sababu moja kuwa ukienda Marekani au Uingereza na nchi zilizoendelea minara ya simu ipo michache au hakuna kabisa ukilinganisha na Tanzania ambapo kila mtaa unakuta minara si chini ya minne....
 
Jibu langu ningesema ni tatizo la kiteknologia ndo linasababisha minara ya simu iwe mingi kuliko ya radio... Ingawa sina utaalam wa aina yoyote. Jibu langu nalilinda na sababu moja kuwa ukienda Marekani au Uingereza na nchi zilizoendelea minara ya simu ipo michache au hakuna kabisa ukilinganisha na Tanzania ambapo kila mtaa unakuta minara si chini ya minne....
Ipo mingi zaidi! ila inafichwa.
wao wanatumia simu kama zetu, watakosaje minara!
Ukiona Bundi ujue Panya wapo!
 
Back
Top Bottom