MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 20,897
- 63,796
Raisi Obama ni kiongozi wa taifa kubwa na lenye nguvu sana hapa duniani.
Kwenye masuala ya Ulinzi ndiyo usiseme kabisa. Wako mbele zaidi ya nchi nyingi hapa duniani kwenye masuala ya TEHAMA, miaka kama mitatu iliyopita tulisikia shutuma mbali mbali dhidi ya shirika la kijasusi la Marekani (N.S.A) kwamba lilikuwa linadukua mawasiliano ya viongozi wakubwa wa nchi tofauti hapa duniani.
Hata kwa kiburi zaidi satelaiti ya shirika hilo iliyorushwa mwaka juzi ilichorwa mnyama aina ya Pweza akiizunguka dunia na wakaandika maneno "NOTHING IS BEYOND OUR REACH" . Wamarekani walimdukua Waziri mkuu wa Ujerumani hata kabla hajawa waziri mkuu. Kiukweli kuyafanya haya inahitaji taifa liwe na uwezo wa kipekee sana katika teknolojia.
Lakini kuna msemo husema "MUOSHA HUOSHWA"
Marekani na yeye kadukuliwa tena kibaya zaidi siyo na taifa bali na genge la watu.
Kama taarifa za muhimu za Waziri wa mambo ya nje zinavuja vile Je nchi ya Marekani ipo salama kweli? Sasa kinacholeta maswali mengi ni kwamba wanaofanya hivyo ni akina nani?
Je, ni kweli Warusi? Wachina? Wikileaks? Wamarekani? au ni Edward Snowden?
Kudukuliwa kwa mtu kama Hillary Clinton kunaweza kusamehewa kwasababu yule mama alitumia barua pepe binafsi: Lakini hili la leo la mawasiliano ya barua pepe za raisi Obama kuvujishwa na WIKILEAKS limekuwa ni gumu kumeza. Kwa kifupi raisi wa Marekani anatumia anuani ya peke yake ya barua pepe ambayo mtu wa kawaida huwezi kujua. Lakini cha kushangaza mawasiliano ya Obama kabla na baada ya kuwa raisi yamevujishwa nje leo.
Kama hili lingetokea wakati wa vita wangepona kweli?
Na kuvuja kwa taarifa hizi siyo mkono wa mtu wa nje peke yake lazima Wamarekani wenyewe wanahusika moja kwa moja. Sasa wataalamu mtuambie kama Raisi Obama anadukuliwa kama mimi MALCOM LUMUMBA, bado tutaendelea kujiaminisha kwamba Marekani haigusiki na bado ipo salama?
Link:WikiLeaks - The Podesta Emails
CC: Bukyanagandi , Bowie , maalimu shewedy , Barbarosa
Kwenye masuala ya Ulinzi ndiyo usiseme kabisa. Wako mbele zaidi ya nchi nyingi hapa duniani kwenye masuala ya TEHAMA, miaka kama mitatu iliyopita tulisikia shutuma mbali mbali dhidi ya shirika la kijasusi la Marekani (N.S.A) kwamba lilikuwa linadukua mawasiliano ya viongozi wakubwa wa nchi tofauti hapa duniani.
Hata kwa kiburi zaidi satelaiti ya shirika hilo iliyorushwa mwaka juzi ilichorwa mnyama aina ya Pweza akiizunguka dunia na wakaandika maneno "NOTHING IS BEYOND OUR REACH" . Wamarekani walimdukua Waziri mkuu wa Ujerumani hata kabla hajawa waziri mkuu. Kiukweli kuyafanya haya inahitaji taifa liwe na uwezo wa kipekee sana katika teknolojia.
Lakini kuna msemo husema "MUOSHA HUOSHWA"
Marekani na yeye kadukuliwa tena kibaya zaidi siyo na taifa bali na genge la watu.
Kama taarifa za muhimu za Waziri wa mambo ya nje zinavuja vile Je nchi ya Marekani ipo salama kweli? Sasa kinacholeta maswali mengi ni kwamba wanaofanya hivyo ni akina nani?
Je, ni kweli Warusi? Wachina? Wikileaks? Wamarekani? au ni Edward Snowden?
Kudukuliwa kwa mtu kama Hillary Clinton kunaweza kusamehewa kwasababu yule mama alitumia barua pepe binafsi: Lakini hili la leo la mawasiliano ya barua pepe za raisi Obama kuvujishwa na WIKILEAKS limekuwa ni gumu kumeza. Kwa kifupi raisi wa Marekani anatumia anuani ya peke yake ya barua pepe ambayo mtu wa kawaida huwezi kujua. Lakini cha kushangaza mawasiliano ya Obama kabla na baada ya kuwa raisi yamevujishwa nje leo.
Kama hili lingetokea wakati wa vita wangepona kweli?
Na kuvuja kwa taarifa hizi siyo mkono wa mtu wa nje peke yake lazima Wamarekani wenyewe wanahusika moja kwa moja. Sasa wataalamu mtuambie kama Raisi Obama anadukuliwa kama mimi MALCOM LUMUMBA, bado tutaendelea kujiaminisha kwamba Marekani haigusiki na bado ipo salama?
Link:WikiLeaks - The Podesta Emails
CC: Bukyanagandi , Bowie , maalimu shewedy , Barbarosa