Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,483
- 40,004
- Thread starter
-
- #61
muulize mwanakijiji ni nini kimo na hakimo kwenye muswada hatasema kwa undani lakini hotuba ya Rais ataichambua utadhani ndio katiba yenyewe.
Are you sure ? Yaonekana huijui Marekani.That can be done too.
Imagine Obama angekuwa na 83% ya congress...... angepitisha mswaada wowote anaoutaka,
Yeah, that's one and there's more.the only thing ambacho kingemzuia ni Supreme court based on constitutionality..... thats it.
Yeah, that's two and there's a lot more.Au labda na congressmen wake wamgeuke.....
Nay, it's not that easy......other than that, it's easy like.... (you know the rest).
muulize mwanakijiji ni nini kimo na hakimo kwenye muswada hatasema kwa undani lakini hotuba ya Rais ataichambua utadhani ndio katiba yenyewe.
sijui umeingiiaje lakini huo mswada nilishauchambua vipengele kwa vipengele kabla CCM jhawajacharuka. Ipo thread tafute tu hapa.
I do, more than what you think.Are you sure ? Yaonekana huijui Marekani.
SOBY, kuna mambo mengine yanawezekana tu hapa kwetu Bongo k.m. hotuba ya leo aliyotoa Kikwete, masikini Tanzania !
wengine mko nje ya nchi mnajifanya kuelewa sana kinachoendelea huku nyumbani hebu tuliizeni na sisi tulioko hapa ndio maana mnanukuu vitu ambavyo JK hakusema hata kama ni siasa sivyo hivyo
Kwa nini wameweka vitisho vya hukumu na vifungo mtu akihoji? kama huo si udikteta ni nini waache kabisa mchezo tutamalizana kwa ajili ya katiba, wachezee katiba ya CCM si hii.
nimemnukuu tu yeye kuwa anadai kuwa anayo mamlaka hayo na katiba na pia ametoa mfano wa tume mbalimbali huko nyuma za kushugulikia maswala ya katiba mwaka 1963 na mwaka 1983 ambazo ni Rais ndio aliziunda utaratibu ambao binafasi sikubaliani nao kwani kwa kuwa ulitumika mwaka 1983 na 1963 basi unafaa kwa watu wa 2011 that is wrong. kwahiyo kama hakuna kipengele chochote basi ndio itatupa hoja nzuri ya kuingia barabarani hiyo jumapili.
kwa kuanzia mwenye access na muswada uliopitishwa bungeni dodoma tuletee hapa tuone ni nini hakimo ambacho tulitaka kiwemo tutolee maoni kama JK alivyosema.
chadema ndio hawaelewi ni kwa nini huwezi kumwondoa kabisa Rais aliyopo madaraka kuwa sehemu ya mchakato lakini alisema hiyo haina maana yeye ndiye ataandika katiba bali ni maoni ya wananchi na kura itakayopigwa ama kukubali au kukataa katiba kabla haijawa rasmi
mwanakijiji, i am sorry to say you are wrong. kama umemsikiliza vizuri jk leo amekuwa akinukuu katiba hii iliyopo ambayo ina mpa mamlaka ya kuunda Tume ya katiba kwahiyo kama aliyowahi kusema mnyika huko nyuma kilichotakiwa kufanywa bungeni ni kufanya mabadiliko ya katiba iliyopo sasa na kuigiza kipengele kitachowapa rasmi mamlaka kamili wananchi ya kuunda katiba yao wenyewe bila kuingiliwa na mamlaka yeyote kwahiyo mabadiliko ya katiba nchi hii hayawezekani kwa utaratibu uliopo inatubidi tuingie mtaani kudai haki ya kuamua namna nchi yetu itakavyotawaliwa. we have to fight back otherwise forget about having the constitution with political and legal legitimacy.
By Mzee Mwanakijiji;
a. Kabla ya kuundwa kwa tume hiyo ya kukusanya maoni ilitakiwa kwanza yafanyike mabadiliko katika Katiba ya sasa ambayo yangeweza utaratibu wa kuandika Upya Katiba ya nchi. Katiba ya sasa inaruhusu kufanyiwa mabadiliko tu (ammendments) lakini hairuhusu kuwepo kwa mchakato wa kuandika Katiba Mpya.
b. Mabadiliko hayo ya Katiba ya kuweka mchakato ndio yangejadili nani na kwa vipi teuzi za tume ya kuandika Katiba unatakiwa kufanyika. Haiwezekani Rais aliyeko madarakani anajiamulia tu kuandika Katiba Upya yeye mwenyewe halafu wengine wafuate; Tukumbuke tamko la kuandika Katiba Mpya lilitolewa kwenye salamu za mwaka mpya! Halikutolewa Bungeni na wala hakukuwa na utaratibu wa kuonesha kuwa umejali wananchi. Ulikuwa ni uamuzi binafsi wa Kikwete. Tukumbuke kuwa kwenye hotuba ile hakusema "amedhamiria" la hasha alisema "ameamua".
c. Ni kutoka hapo sasa ndio sheria ya kusimamia mchakato wa kuelekea Katiba Mpya ungeweka. Ina maana ya kwamba suala la Kuandika Katiba Mpya lingewekwa ndani ya Katiba ya sasa na kuangaliwa kama tunavyoangalia yale mambo 8 ambayo yanahitaji ridhaa ya pande mbili za Muungano (theluthi mbili ya wajumbe). Lakini kwa hivi ilivyo Kikwete na Shein wataamua wao wenyewe. Sasa hiyo sheria ndio ingezingatia maoni ya watu wengine.
Utaona basi kuwa kosa la kwanza limefanyika kwa kutozingatia Katiba ya sasa kwanza - haina mchakato wa kuandika Katiba Mpya - na hivyo kufanya hoja ya Katiba Mpya haiwezi kutolewa na wale walioapa kuilinda ya sasa na kama inatolewa walitakiwa kwanza kufanyia mabadiliko hii Katiba ili wajipe uwezo wa kuzungumzia "katiba mpya".
Mimi ni mmoja wa wasiopenda kujadili watu na matukio bali napenda tujadili hoja za kuweka au kutokuweka katika katiba mpya na hii itasaidia wengi kupunguza ubishani hapa (small minds discuss people, average minds discuss events, great minds discuss ideas.)
mimi sijawahi kuona mwanasiasa anae zungumza na watu kwenye mkutano huku amekaa, nadhani huyu siyo raisi hata mtitiriko wa sauti yake haina hadhi ya uraisi