Kwa nini jaji haombi kujiuzulu kwa Jaji Mkuu?

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Kila siku tunaimbiwa kwa kuna Mihimili 3 inayojitegemea, sasa swali langu kwa nini Jaji akitaka kujiuzulu haombi kwa Jaji Mkuu badala yake anaomba kwa Raisi JMTZ?

Maoni yangu, bado hamjauelewa vizuri mfumo wa TZ, mnakwenda Shuleni kukaririshwa tu, halafu kuna watu wanajidanganya kwamba watamuondoa Raisi wa JMTZ kwa kutumia Mihimili mingine ,,inayojitegemea", ...
 
Kila siku tunaimbiwa kwa kuna Mihimili 3 inayojitegemea, sasa swali langu kwa nini Jaji akitaka kujiuzulu haombi kwa Jaji Mkuu badala yake anaomba kwa Raisi JMTZ?

Maoni yangu, bado hamjauelewa vizuri mfumo wa TZ, mnakwenda Shuleni kukaririshwa tu, ...
Sawa tumekaririshwa vizuri, ongeza lingine kabla sijaondoka
 
Kila siku tunaimbiwa kwa kuna Mihimili 3 inayojitegemea, sasa swali langu kwa nini Jaji akitaka kujiuzulu haombi kwa Jaji Mkuu badala yake anaomba kwa Raisi JMTZ?

Maoni yangu, bado hamjauelewa vizuri mfumo wa TZ, mnakwenda Shuleni kukaririshwa tu, halafu kuna watu wanajidanganya kwamba watamuondoa Raisi wa JMTZ kwa kutumia Mihimili mingine ,,inayojitegemea", ...
Awali ya yote, tukubali kuwa utaratibu wa uteuzi wa majaji hapa Tanzania hauendani kabisa na msingi ulioanza nao wa separation of powers, ( mihili mitatu). Ukitazama kiundani utaona kuwa jaji anateuliwa na Rais hivyo basi barua yake ya kujiuzulu lazima iende kwa aliyemteua.

Itafika siku dhana ya kukaririshwa itaisha, siku watu watakapojua kuwa executive na judiciary ni co-equal partners, na hivyo basi kwa dhana ya separation of powers jaji hatakiwi kuteuliwa na mkuu wa mhimili mwingine kati ya hiyo mitatu, kwa vile kwa kufanya hivyo ni kufifisha dhana ya separation of powers.
 
Hata ukifanikiwa kumuua Rais wa nchi bado utaenda mahakamani na wasipokuwa makini bado unaweza kushinda kesi.
 
Kila siku tunaimbiwa kwa kuna Mihimili 3 inayojitegemea, sasa swali langu kwa nini Jaji akitaka kujiuzulu haombi kwa Jaji Mkuu badala yake anaomba kwa Raisi JMTZ?

Maoni yangu, bado hamjauelewa vizuri mfumo wa TZ, mnakwenda Shuleni kukaririshwa tu, halafu kuna watu wanajidanganya kwamba watamuondoa Raisi wa JMTZ kwa kutumia Mihimili mingine ,,inayojitegemea", ...
Nafasi ya jaji ni ya uteuzi, kwanini ukitaka kujiuzulu usimuombe aliye kuteua? nafikiri hiyo hoja ikijibiwa itajibu swali hilo.
 
Hoja yako kwamba watu hawauelewi mfumo wetu na mihimili ya dola haina mashiko, watu wanafahamu vyema kuhusu madaraka makubwa ya Raisi na changamoto nyingi katika mifumo ya utawala. Hili limethibitishwa na maoni ya watu watu wengi yaliyopendekezwa katika mabaraza ya katiba kipindi mchakato upo hai, pitia maoni ya watu na mapendekezo ya tume pamoja na katiba utagundua si kwamba watu wamekariri bali wanafahamu vizuri mifumo ya mihimili inavyofanya kazi.
 
Back
Top Bottom