Lugha itakayotumika ni ile lugha ya kwanza aliyoitumia MUNGU baada ya kumuumba Adamu na Hawa pale Bustanini. Mimi nikiwa kama Mkristo nimesoma kwenye Biblia kuwa BWANA MUNGU alikuwa akiongea na Adamu, sasa lugha hiyo ndiyo iliendelea kutumika duniani mpaka ile siku lugha ilipochafuliwa wakati ule wakiujenga mnara wa Babeli na zikawa lugha nyingi.Ni maswali ninayojiuliza pasipo kupata jibu. Kwa kuwa hili ni jukwaa la wajuzi wa mambo mengi naomba kupata majibu ya maswali yangu kwa anaefahamu.
Mkuu Son of Gamba ahsante kwa majibu yako kwa kuzingatia imani yakoLugha itakayotumika ni ile lugha ya kwanza aliyoitumia MUNGU baada ya kumuumba Adamu na Hawa pale Bustanini. Mimi nikiwa kama Mkristo nimesoma kwenye Biblia kuwa BWANA MUNGU alikuwa akiongea na Adamu, sasa lugha hiyo ndiyo iliendelea kutumika duniani mpaka ile siku lugha ilipochafuliwa wakati ule wakiujenga mnara wa Babeli na zikawa lugha nyingi.
Hivyo basi kama kulikuwa na lugha ya kwanza ambayo aliitumia mtu wa kwanza ambaye ni Adamu, basi ipo siku wanadamu wote wataitumia hii lugha na siku hii ni ile siku ya mwisho ambapo Ufalme wa MUNGU utakuja duniani.
Kuhusu lugha hiyo ni ipi? mimi sijui ilikuwa ni lugha gani, na kuhusu watu watajifunzaje lugha hii, jibu ni kwamba uwezo wa MUNGU ni mkubwa sana, hakuna analoshindwa kufanya.
Habari wana jamvi? Poleni na mihangaiko ya kimaisha.
Kwanza kabisa nianze kwa kusema nimekuwa na hili swali fikirishi sana kuhusu dini hizi mbili Uislam na Ukristo na mpaka sasa sijapata majibu yenye kujitosheleza kabisa.
1. Kwa nini hizi dini mbili zimekuja kutoka nje ya bara la Afrika?
2. Kwa nini hakuna mtume mweusi? Mitume yote utasikia na kusoma kwenye vitabu hivyo yaani Quran na Biblia kuwa walikuwa waarabu au wayahudi nk lakini hakuwa mtu mweusi
3. Kwa nini maandiko ya dini hizi yanataka waumini wake waamini kuwa race hizo zilizopokea dini hizo ni bora kuliko race zingine? ?
4. Kwa sisi tunaoamini katika dini hizi mbili, tunaamini tukifa tunaenda kukutana na mungu alietuumba nk kila dini ina mafundisho yake kuhusu maisha baada ya kufa. Swali langu liko hapa Je ni lugha ipi itakayotumika huko mbinguni??? Mfano waislam tunaamini kuna maisha ya kaburini na kuna maisha ya kisimamo cha hukumu yaani kiyama ( mtanisahibisha kama nimekosea) na pia kuna maisha imma ya motoni au peponi je ni lugha gani itakayotumika katika maisha hayo baada ya kufa.??
Ni maswali ninayojiuliza pasipo kupata jibu. Kwa kuwa hili ni jukwaa la wajuzi wa mambo mengi naomba kupata majibu ya maswali yangu kwa anaefahamu.
Ahsanteni.
Ile ambayo Mungu anaskia lugha yoyoteIpi hiyo mkuu?
KABISA.Dini ni way of life
Utasikia jibu lake DINI YA HAKI ndo hiyo mamtu yanachinjia binadamu wenzie na kutaja jina la Mungu waoIpi hiyo mkuu?