Elections 2010 Kwa nini elimu bure inawezekana

Nimepata uhakika elimu bure inawezekana baada ya kumsikiliza Dr. Slaa. Kama JK anaweza kusambaza picha zake nchi nzima kwenye nyumba za maskini zilizoezekwa kwa nyasi, kwa nini Dr. Slaa asiweze kusambaza elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha sita nchi nzima?

Kwanza pesa kusambaza za kusambaza sura yake kwenye mabango nchi nzima zimepatikania wapi?

Hiyo hela ya mabango ya JK ni hela ya KILIMO KWANZA, wewe subiri uchaguzi uishe, na mabomu yaanze kulipuka. Noni wa TIB kajitayarisha kukimbia nchi tayari, tutarudi kama mambo ya Balali sasa.
 
Mkuu vitaje vyanzo vyz elimu bure ili watu waelewe kuwa siyo pesa iliyotumika kusambaza mabango ya JK kwenye nyumba za nyasi ingeweza kusambaza elimu bure nchi nzima bali Dr Slaa atatumia vyanzo vingine pia. Mkuu vitaje, tunafanya windo shopingi. Eleza wazi, watu wajue hili linawezekana kuanzia tarehe Dr. Slaa anayoapishwa kuwa rais na kuwekwa sawasawa katika muhula mpya wa masomo wa kuanzia tarehe 1.1.2011.

Mkuu, according to Dr. Kitila Mkumbo (Phd) katika kipindi cha tuongee asubuhi cha startv jana asubuhi ni kwamba;
Gharama za uendeshaji wa shule za msingi na sekondari including na tuition fees kwa mwaka ni shilingi takribani shilingi bilioni 100.
Akaeleza kuwa, kwa mujibu wa ripoti ya CAG, mwaka jana serikali ilitoa misamaha ya kodi inayofikia kiasi cha shilingi bilioni 700 ambayo ni kutokana na serikali kutoa msamaha wa kodi wa 2.7% kiwango ambacho ni kikubwa sana tofauti na nchi nyengine na kinyume na ushauri wa TRA kwamba serikali ipunguze misamaha hadi 1% ambacho ndio kiwango wanachosamehe wengine huko duniani.
Kama serikali ingefuata ushauri wa TRA, basi kiasi cha shilingi bilioni 500 kingeweza kuokolewa na hivyo tukapata bilioni 100 kugharimia elimu ya lazima ya kidato cha sita kwa kila mtanzania na tukabakiwa na chenchi ya bilioni 400 zikaelekezwa kwenye huduma nyengine.
Kwahiyo elimu ya lazima ya kidato cha sita inawezekana, afya bure inawezekana na makazi bora kwa kila mtanzania yanawezekana chini ya Chadema na Dr.Slaa(Phd).
 
Mkuu, according to Dr. Kitila Mkumbo (Phd) katika kipindi cha tuongee asubuhi cha startv jana asubuhi ni kwamba;
Gharama za uendeshaji wa shule za msingi na sekondari including na tuition fees kwa mwaka ni shilingi takribani shilingi bilioni 100.
Akaeleza kuwa, kwa mujibu wa ripoti ya CAG, mwaka jana serikali ilitoa misamaha ya kodi inayofikia kiasi cha shilingi bilioni 700 ambayo ni kutokana na serikali kutoa msamaha wa kodi wa 2.7% kiwango ambacho ni kikubwa sana tofauti na nchi nyengine na kinyume na ushauri wa TRA kwamba serikali ipunguze misamaha hadi 1% ambacho ndio kiwango wanachosamehe wengine huko duniani.
Kama serikali ingefuata ushauri wa TRA, basi kiasi cha shilingi bilioni 500 kingeweza kuokolewa na hivyo tukapata bilioni 100 kugharimia elimu ya lazima ya kidato cha sita kwa kila mtanzania na tukabakiwa na chenchi ya bilioni 400 zikaelekezwa kwenye huduma nyengine.
Kwahiyo elimu ya lazima ya kidato cha sita inawezekana, afya bure inawezekana na makazi bora kwa kila mtanzania yanawezekana chini ya Chadema na Dr.Slaa(Phd).

Mkuu nimeipenda sana hii, tuendele kuwaambia ndugu zetu elimu bure kwa Dr Slaa inawezekana. Kumbe Tanzania siyo masikini, ni nchi Tajiri sana. CCM ndio wanaifanya nchi yetu kuwa maskini, tuwamwage, hakuna cha kujiuliza tena ni kuachana na CCM na mambo yao yote, na JK wao na wabunge wao wote, tuwaingize Chadema tupate elimu bure na yenye ubora siyo ya voda fasta.
 
tatizo elimu inaonekana kuwa ghali; ndio maana sasa tunajaribu ujinga.
 
Halafu mbona anasa zote za CCM hazijawahi kukosekana, ila pesa ya elimu na afya tu ndo iwe haitekelezeki!

basi tu kwa vile ni sisi Tanznia. lakini ingekuwa wenzetu CCM ishakuwa chali longiiiiiii!
wewe mpaka waongeze ukubwa wa serikali (yaani wakuu wa mikoa, wilaya) hatuna hela kweli, ufisadi wote wanaofanya!

Elimu bure inawezekana sana tu, na ndo maana wanmwogopa sana Dr. Slaa maana anasema ukweli

Wananchi wanaficha watoto kwa sababu hawana uwezo wa kuwapeleka shule. Elimu bure inaanza tarehe ngapi rasmi?, tunahitaji elimu bora ya Dr Slaa.
 
Hii ni moja ya sababu ya Dr. Slaa HAFAI KUWA RAIS. Hivi hakumbuki kwamba Nyerere alishindwa kuwapa Watanzania elimu bure kwa muda wa miaka 25? Slaa kasahau kwamba Tanzania ipo nyuma kielimu kwa sababu Nyerere aliamini serikali itawapatia elimu bure Watanzania wote?
Hivi anataka apewe nchi halafu arudie makosa yale yale ya Nyerere ya UJAMAA.
 
IMETULIA SANA.

Hebu basi tuchambulie kiduchu kuhusu fedha itakayopatikana iwapo viwango vyetu vya kodi ya uchimbaji madini vikiwa sawa na vile vya Botswana, tutakula ngapi kila mwaka.
 
..Tatizo si lake na huko alipopewa hizo taarifa kuwa ELibu ya bure haiwezekani kwani hakugundua pia waliompatia hizo taarifa hawana uelewa wowote kama yeye..Kazi ipo kwa kweli
 
Back
Top Bottom