Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk. Idrisa Rashidi ni miongoni mwa watu kumi mashuhuri walioshiriki na kujipatia mabilioni katika kashfa ya radar. Wahusika wengine wakuu ni pamoja na Andrew Chenge, Sailesh Pragji Vithlani na Tanil Kumar Chandulal Somaiya.
Iliwahi kutajwa kuwa mnamo May 1998, Chenge alimgawia nusu ya pesa za rushwa alizopata (kiasi cha Tsh. 750,000,000.00) Dr. Idris kupitia kampuni yake ya Langley Investments Ltd.
Chenge akiwa Mwanasheria Mkuu wa serikali na Dr. Idris akiwa Gavana wa Benki Kuu walilipwa fedha hizo kwa ushiriki wao katika kufikiwa kwa mkataba wa ununuzi wa rada hiyo iliyouzwa kwa serikali na shirika la kuuza vifaa vya kijeshi la Uingereza, BAE System.
Kufuatia kashfa hii, Chenge alilazimika kujiuzulu lakini Dr. Idris bado kajaa tele pale Tanesco akiwa Mtendaji Mkuu na hivi sasa anapendekeza serikali inunue mitambo ya Dowans.
Kwa nini Dr. Idris Rashidi bado yuko pale hadi leo hii !! Ni siri gani anayo huyu fisadi ?
Iliwahi kutajwa kuwa mnamo May 1998, Chenge alimgawia nusu ya pesa za rushwa alizopata (kiasi cha Tsh. 750,000,000.00) Dr. Idris kupitia kampuni yake ya Langley Investments Ltd.
Chenge akiwa Mwanasheria Mkuu wa serikali na Dr. Idris akiwa Gavana wa Benki Kuu walilipwa fedha hizo kwa ushiriki wao katika kufikiwa kwa mkataba wa ununuzi wa rada hiyo iliyouzwa kwa serikali na shirika la kuuza vifaa vya kijeshi la Uingereza, BAE System.
Kufuatia kashfa hii, Chenge alilazimika kujiuzulu lakini Dr. Idris bado kajaa tele pale Tanesco akiwa Mtendaji Mkuu na hivi sasa anapendekeza serikali inunue mitambo ya Dowans.
Kwa nini Dr. Idris Rashidi bado yuko pale hadi leo hii !! Ni siri gani anayo huyu fisadi ?