Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,041
- 71,861
Tuliona ndani ya Bunge, wabunge watokanao na Chadema ndio wanaoonyesha uwezo wa kutoa hoja maridhawa na hata Makamu wa Rais alikiri hilo na kuwaambia wabunge ccm wajifunze nao kutoa hoja makini kama wapinzani.
Ukija kwenye mhimili wa uendeshaji serikali, wamepewa serikali za mitaa Dar tunaona mabadiliko na watu wanakubali. Ukienda Arusha watu wanasema wamechekewa sana kuwapa nafasi hiyo kwa jinsi walivyo makini.
Sasa na leo katika mhimili mwingine wa sheria tumeona mawakili wa serikali walivyokuwa kama wanafundishwa sheria na mawakili wa Chadema kuhusu dhamana ya Lissu.
Ndio maana tunajiuliza huko Chadema inakuwaje kuna watu mahiri ambao wana fit katika mihimili yote? Jee sio wakati muafaka kwa ccm badala ya kuendekeza ugomvi na wivu wakajifunza toka huko ili tujenge nchi?
Ukija kwenye mhimili wa uendeshaji serikali, wamepewa serikali za mitaa Dar tunaona mabadiliko na watu wanakubali. Ukienda Arusha watu wanasema wamechekewa sana kuwapa nafasi hiyo kwa jinsi walivyo makini.
Sasa na leo katika mhimili mwingine wa sheria tumeona mawakili wa serikali walivyokuwa kama wanafundishwa sheria na mawakili wa Chadema kuhusu dhamana ya Lissu.
Ndio maana tunajiuliza huko Chadema inakuwaje kuna watu mahiri ambao wana fit katika mihimili yote? Jee sio wakati muafaka kwa ccm badala ya kuendekeza ugomvi na wivu wakajifunza toka huko ili tujenge nchi?