Swagger is alive
JF-Expert Member
- Jul 8, 2016
- 559
- 467
Hakika CHADEMA wamethubutu, wamefanya na wamefanikiwa kuonyesha njia.
Kazi yeyote ukiifanya kwa dhamira ya moyo na kutumia akili halisi sio ya kuongozwa na unafiki lazima iwe nzuri.Jana nimeamini kuwa Lisu na Kibatala ni watu hatari sana kwenye fani hii ya uwakili. Ilikuwa kama sinema isiyochosha kuitazama.
[emoji106]Wanapaswa wajitizame sasa
Mungu ibariki chadema .Tuliona ndani ya Bunge, wabunge watokanao na Chadema ndio wanaoonyesha uwezo wa kutoa hoja maridhawa na hata Makamu wa Rais alikiri hilo na kuwaambia wabunge ccm wajifunze nao kutoa hoja makini kama wapinzani.
Ukija kwenye mhimili wa uendeshaji serikali, wamepewa serikali za mitaa Dar tunaona mabadiliko na watu wanakubali. Ukienda Arusha watu wanasema wamechekewa sana kuwapa nafasi hiyo kwa jinsi walivyo makini.
Sasa na leo katika mhimili mwingine wa sheria tumeona mawakili wa serikali walivyokuwa kama wanafundishwa sheria na mawakili wa Chadema kuhusu dhamana ya Lissu.
Ndio maana tunajiuliza huko Chadema inakuwaje kuna watu mahiri ambao wana fit katika mihimili yote? Jee sio wakati muafaka kwa ccm badala ya kuendekeza ugomvi na wivu wakajifunza toka huko ili tujenge nchi?