Kwa nini CHADEMA kila mahali?

Kwa nini CHADEMA kila mahali?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,197
Reaction score
7,533
Kila mahali chadema wanalaumiwa hivyo wanapaswa kuona wanapokosea na kujirwkwbisha
 
Wakuu nimefuatilia mahali mbali mbali na sasa nimethibitisha.Nimethibitisha kwamba sasa hivi kila mahali kwenye mjadala wa siasa, CHADEMA ni lazma itajwe sana, na kwa kadiri inavyotajwa ndivyo wachangiaji wanaongezeka.
Kwa mfano;

1. Ukija hapa JF; Kwa kila thread kumi zitakazo anzishwa kwenye jukwaa la siasa (iwe ni za kusifu au kuponda) utakuta nane (08) zinaihusu CHADEMA.

2. Hapa JF; Katika jukwaa la siasa, nyuzi zinazochangiwa na watu wengi ni zile zinazoitaja CHADEMA (Fuatilieni mtaniambia)


3. Bungeni karibu kila mzungumzaji akiongea bila kujali chama chake, atatafuta ka chance ahakikishe anaitaja CHADEMA, na akishafanya hivyo basi utakuta bunge zima linamtazama kwa makini kweli.


4.Mitaani ukipita ukikuta kuna kamjadala ka kisiasa wewe vizia tu usikilize, utasikia wahusika wakuu wanao jadiliwa ni chadema.

5.Ukienda vyuoni; kwenye mijadala ya vijana, kama ukiwakuta wanajadili siasa, lazma wahusika wakuu (wanaojadiliwa)utakuta ni CHADEMA

Na mifano mingine mingi.

Sasa mimi ninachojiuliza ni kama; hii inatokana na mapenzi ya watanzania kwa CHADEMA? AU ni kutokana na watu kuichukia CHADEMA? au ni watu kuiogopa CHADEMA? au CHADEMA Ina nini hata kila mtu akawa anaiwaza (iwe kwa wema au kwa ubaya)?
Nadhani hizi ndo sababu
1. Hakuna chama upinzani kilichowahi kuwa na wabunge wengi kama CDM
2. Uchache wao unawahangaisha wabunge zaidi ya 350 wa CCM
3. Wametaja madudu kadhaa ya serikali na inaoneka ni ya kweli eg Mafisadi, Meremeta, EPA etc
4. CCM wanaiogopa CDM utadhani ndo chama pekee cha upinzani
5. CDM imekuwa ikishinda karibu kila kesi iwahusuyo mahakamani


 
Kwa humu, ukitaka kufahamika, ipondee CDM au Dr Slaa.
 
Hii ni moja ya zile thread nyingi zinazoanzishwa zikiihusu CHADEMA, tarajia wachangiaji wengi!
 
:clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::majani7::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2:
 
Wabongo wamechoshwa na blablablabla kwa zaidi ya miongo mitano sasa tokea kupata uhuru - ufukara umekithiri kwa asilimia kubwa ya wabongo, mfano watoto wa shule wanakaa sakafuni katika vyumba vinavyoitwa madarasa, akina mama wajawazito wanajifungulia sakafuni katika vyumba vilivyobatizwa wodi za uzazi, watu wa vijijini wana-share maji ya vidimbwi na ng'ombe wao, nk. nk. Kila baada ya miaka mitano wanaona njemba zilizoshiba zinarejea majimboni kutoka Dar es Salaam kuja kuomba kura ili ziendelee kula na kuwaachia fulana na kanga ambazo hawawezi kupata sabuni za kuzifulia pamoja na ahadi hewa kibao. Wamekata tamaa. Wanatafuta kama inaweza kutokea njia mbadala ya kuwapa ahueni. CDM inaelekea kuwapa matumaini. Kinaweza kutokea chama kingine kujaza nafasi hiyo. Ila kwa sasa CDM ndio imeshika husukani. Kwa wanaonufaika na status quo wanailaani, na kwa walazwahoi wanaona ndio mkombozi.
 
Hii ni moja ya zile thread nyingi zinazoanzishwa zikiihusu CHADEMA, tarajia wachangiaji wengi!

Kitu unachokichukia huwezi kukitaja sana. Ukiona kitu au mtu anatajwa sana ni lazima ana umaarufu fulani na ambao ni mzuri. That is the only reason Chadema inatajwa. Na mara kitu hicho au mtu huyo anakuwa analinganishwa na kitu au mtu mwingine. Sasa jiulize. Chadema inalinganishwa na nini? :llama:
 
Peoplesssssssss! Chadema ndio chama bwana sio cuf,magamba nk.Najisikia kuwa chadema
 
CHADEMA ndio chama pekee kilichobeba matumaini ya watanzania wengi,chama chenye mtazamo chanya juu ya maendeleo ya hii nchi,chama kikichoamua kweli kupambana na CCM kuhakikisha kuwa demokrasia inakua nchini,chama ambacho viongozi wake wamejitolea kwa hali na mali kuhakikisha watanzania wanaondokana na kutawaliwa na wakoloni weusi.Kuna mambo mengi sana ambayo CHADEMA inayafanya na kuwafurahisha wananchi ndio maana wanakizungumzia sana.
 
mimi haipiti siku bila kupokea sms inayonisisitiza mabaya ya ccm na jinsi ya kuhakikisha tunaing'oa kwa mabaya yake..
Kijijini kwangu watu waliichukia ccm mpaka wameamua kwamba ukitaja ccm unatengwa..

Nilifurahi sana nilipoenda kijijini kwangu nikamkuta mzee wangu amaamua kurudisha mihuri na bendera za ccm!

Nilimuuliza mzee nini kimekukuta akaniambia ccm ni wabaya sana.. Matendo wanayofanya siku hizi siwezi tena kuipenda ccm...
Nilifurahi kwani Baba yangu alikuwa katibu wa kijiji cha Ruwa kwa chama cha mpinduzi....
Hakika nilifurahi.. Kwani sametime nilikuwa naenda nyumbani na kukuta mabendera yake ya ccm.
 
Nadhani hizi ndo sababu
1. Hakuna chama upinzani kilichowahi kuwa na wabunge wengi kama CDM
2. Uchache wao unawahangaisha wabunge zaidi ya 350 wa CCM
3. Wametaja madudu kadhaa ya serikali na inaoneka ni ya kweli eg Mafisadi, Meremeta, EPA etc
4. CCM wanaiogopa CDM utadhani ndo chama pekee cha upinzani
5. CDM imekuwa ikishinda karibu kila kesi iwahusuyo mahakamani


Mkuu hujakosea, hata wanachama wa magamba wamegeuka kuwa waenezi wa cdm, hata humu jf akina hammy-d na wenzie kila thread wanayoanzisha ni juu ya cdm raha kweli kweli.
 
Ni kama sisi mashabiki wa soka huwezi kuchambua mpira wa leo bila kumtaja Ronaldo au Messi Chadema wapo vizuri aise sheh!!
 
Back
Top Bottom