ADVOCATE NEWBOL
Member
- May 21, 2011
- 33
- 11
Kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Tanzania (ILIYOTUNGWA NA CCM) ya 1977 na sheria za uchaguzi mTanzania anaruhusiwa kugombea ama udiwani, au ubunge, au udiwani na ubunge kwa pamoja au urais. Mtanzania hawezi kugombea udiwani, ubunge na urais kwa wakati mmoja kama ilivyo kwa Kenya, Marekani na nchi nyingine nyingi zenye demokrasia ya kweli. Swali ni je, kwa nini tusigombee nafasi hizo kwa pamoja?
Suala hili ni muhimu sana hasa wakati huu wa mjadala wa Katiba mpya. Mawazo finyu ya CCM ni kuwa, kama ilivyo kwa mgombea binafsi ,hili litadhoofisha chama chetu kwani viongozi wa vyama pinzani kama Dr SLAA na LIPUMBA watapata mwanya wa kuingia bungeni, yaani CCM inawaadhibu wapinzani wanaothubutu kugombea urais na kuipinga CCM kwa kuwanyima nafasi ya kuingia bungeni. Jambo hili linaminya demokrasia nchini kwani kama Lipumba, SLAA, MTAMWEGA nk wangeruhusiwa kugombea urais na ubunge na udiwani kwa pamoja; sasa hivi tungekuwa nao bungeni wakichangia kwa nguvu zote kuijenga Tanzania yetu. Lakini wapi, hawako bungeni.
Swali jingine ni je, kutatokea nini iwapo mgombea atashinda udiwani, ubunge na urais? Jibu ni kuwa yeye mwenyewe atachagua kupitia TUME YA UCHAGUZI ni ktk nafasi gani, je ni ktk urais au udiwani au ubunge, angependa kuwatumikia waTanzania. Kama akichagua urais basi, ubunge na udiwani vitakuwa wazi na taratibu za kuziba nafasi hizo kwa mujibu wa SHERIA NA KATIBA zitafuata. WAMAREKANI wanafanya hivyo, kwa nini nasi tusifanye hivyo? Obama na Biden walishinda urais na umakamu wa rais, pia wote walishinda na useneta. Nafasi zao za useneta zilizibwa kwa mujibu wa sheria zao. Kwa nn nasi tusifanye kama wao, mbona kwenye umakamu wa rais tunafanya kama wao?
Suala hili ni muhimu sana hasa wakati huu wa mjadala wa Katiba mpya. Mawazo finyu ya CCM ni kuwa, kama ilivyo kwa mgombea binafsi ,hili litadhoofisha chama chetu kwani viongozi wa vyama pinzani kama Dr SLAA na LIPUMBA watapata mwanya wa kuingia bungeni, yaani CCM inawaadhibu wapinzani wanaothubutu kugombea urais na kuipinga CCM kwa kuwanyima nafasi ya kuingia bungeni. Jambo hili linaminya demokrasia nchini kwani kama Lipumba, SLAA, MTAMWEGA nk wangeruhusiwa kugombea urais na ubunge na udiwani kwa pamoja; sasa hivi tungekuwa nao bungeni wakichangia kwa nguvu zote kuijenga Tanzania yetu. Lakini wapi, hawako bungeni.
Swali jingine ni je, kutatokea nini iwapo mgombea atashinda udiwani, ubunge na urais? Jibu ni kuwa yeye mwenyewe atachagua kupitia TUME YA UCHAGUZI ni ktk nafasi gani, je ni ktk urais au udiwani au ubunge, angependa kuwatumikia waTanzania. Kama akichagua urais basi, ubunge na udiwani vitakuwa wazi na taratibu za kuziba nafasi hizo kwa mujibu wa SHERIA NA KATIBA zitafuata. WAMAREKANI wanafanya hivyo, kwa nini nasi tusifanye hivyo? Obama na Biden walishinda urais na umakamu wa rais, pia wote walishinda na useneta. Nafasi zao za useneta zilizibwa kwa mujibu wa sheria zao. Kwa nn nasi tusifanye kama wao, mbona kwenye umakamu wa rais tunafanya kama wao?