Kwa nia njema tu: Rais asiwe Mwenyekiti wa Chama cha Siasa

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Wazo langu hili limezaliwa jana wakati wa mjadara wa Kigoda cha mwlimu Nyerere pale mlimani nilipomsikia katibu Mkuu wa CCM ndugu yetu A . Kinana, akiwaambia watawala wetu wawe tayari kukosolewa na kuomba radhi pale wanapotambua wamekosa!

Kwa wafuatiliaji wa mambo ya siasa za nchi yetu watakubaliana nami kuwa; hali kama ile agharabu haitokei pale ambapo mwenyekiti wa chama anapokuwa ndiye huyo-huyo rais wa nchi pia; hata kama kutakuwepo makosa kibao.

Ndipo nilipogundua kwamba kumbe nchi yetu kuendelea na mtindo wa kuwa na rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama kunasababisha tuwe na ombwe kuu la wakosoaji, watu wenye hurka ya Kinana , naam wale wenye nia njema ya kukosoa kwa kujenga.

Watu wanaochangia kuondoa magugu kwa upande mmoja na upande mwingine wakipalilia ngano ili izidi kustawi katika shamba Tanzania.
Hiki ndicho tulichokuwa tukikimiss kwa mda mrefu huko nyuma.
Mimi nimeipenda hali hii kwa kuwa itamsaidia rais yeyote atakayekuwa madarakani kutoka chama chochote cha siasa katika kuliongoza taifa hili.

Kama nawe wapenda karibu.
 
images-14.jpeg


ma ccm yatakuja kusutana.

swissme
 
Shida ni kila mtu atakapokuwa anatoa matamko yake, mwenyekiti yuko mahakamani na mgombe uraisi anamlima memo IGP. Dhana ni ukiwa presidaa kusiwe na mwengine juu yako, sasa mwenyekiti ukimzingua akianzisha zengwe la kukufuta uanachama, upresidaa si itakuwa bhaaaas.
 
Kuna kitu kinaendelea nyuma ya Pazia.

Kauli ya jana ya Kinana??

Kauli ya Gwajima??

Kusogezwa mbele kwa mkutano wa kumkabidhi Magufuli chama??
 
Kuna kitu kinaendelea nyuma ya Pazia.

Kauli ya jana ya Kinana??

Kauli ya Gwajima??

Kusogezwa mbele kwa mkutano wa kumkabidhi Magufuli chama??
Plus kauli ya Mkapa "Viongozi wa Afrika wanapata busara wakiwa wameacha uongozi" kuna kitu kinapikwa.
 
Tatizo mafisadi wanaotafuna nchi yetu wamejifisha ndani ya vyama, wanaogopa JMP akichukuwa chama watafukuzwa. MM naona kuanzia JK,Madabina na wengine wengi tu. Wafanyakazi wa umma wanaiba kidogo sana ukilinganisha na hawa viongozi wa vyama. Na tukitaka JMP afanikiwe kupambana na rushwa ni lazima hapewe chama.
 
Wazo langu hili limezaliwa jana wakati wa mjadara wa Kigoda cha mwlimu Nyerere pale mlimani nilipomsikia katibu Mkuu wa ccm ndugu yetu A . Kinana, akiwaambia watawala wetu wawe tayari kukosolewa na kuomba radhi pale wanapotambua wamekosa!
Kwa wafuatiliaji wa mambo ya siasa za nchi yetu watakubaliana nami kuwa; hali kama ile agharabu haitokei pale ambapo mwenyekiti wa chama anapokuwa ndiye huyo-huyo rais wa nchi pia; hata kama kutakuwepo makosa kibao.
Ndipo nilipogundua kwamba kumbe nchi yetu kuendelea na mtindo wa kuwa na rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama kunasababisha tuwe na ombwe kuu la wakosoaji, watu wenye hurka ya Kinana , naam wale wenye nia njema ya kukosoa kwa kujenga.
Watu wanaochangia kuondoa magugu kwa upande mmoja na upande mwingine wakipalilia ngano ili izidi kustawi katika shamba Tanzania.
Hiki ndicho tulichokuwa tukikimiss kwa mda mrefu huko nyuma.
Mimi nimeipenda hali hii kwa kuwa itamsaidia rais yeyote atakayekuwa madarakani kutoka chama chochote cha siasa katika kuliongoza taifa hili.

Kama nawe wapenda karibu.
Nakubaliana kabisa na maangalizo yako. Pia nakubaliana na wazo lako
 
Tayari wanataka kuanza kumwekea Magu figisu figisu, unajua wapigaji karibu wote nchi hii ni ccm, sasa wameona upepo huu sio, mahoteli makubwa karibu yote wana umiliki wa direct au indirect, makampuni makubwa mengi wana umiliki direct au indirect ndo maana mengi yako gizani. Sasa sera za jamaa zinaashiria anguko la kimaslahi, so watakuja na justifications nyiingi ili kumpunguza makali, ila wenye akili tunajua nia yao.
 
tayari CCM mmeanza kukanyagana.
Yeyote yule ambaye hataki Rais Magufuli awe mwenyekiti wa CCM, katumwa na viongozi ndani ya CCM ambao wanaogopa kutumbuliwa, wanahofia kukosa ulaji kwani kwenye chama kumekuwa ndo pahala pa mafisadi(a few -wachache), majangili, wafanya biashara kubwa kubwa na ndogo wanajificha(they get protection and immunity simply because they members of the ruling party),mfano kuna mbunge mmoja wakati wa misako ya sukari alidiriki kumkingia kifua ndugu yake kwa kusema 'sisi wabunge wa CCM tunataka ....wakati wa tv news ...sijui alikuwa ana undugu na zakaria.
 
Tayari wanataka kuanza kumwekea Magu figisu figisu, unajua wapigaji karibu wote nchi hii ni ccm, sasa wameona upepo huu sio, mahoteli makubwa karibu yote wana umiliki wa direct au indirect, makampuni makubwa mengi wana umiliki direct au indirect ndo maana mengi yako gizani. Sasa sera za jamaa zinaashiria anguko la kimaslahi, so watakuja na justifications nyiingi ili kumpunguza makali, ila wenye akili tunajua nia yao.
Historia ina tabia ya kujirudia rudia, kwani yeye si kaingia kwa figisu figisu?
 
Naona mtoa post katumwa na CCM asilia!! haha hah hah. Hii ndo raha ya kuwa ccm bana!! Huwezi ukawa na akili inayojitegemea.
 
Wazo langu hili limezaliwa jana wakati wa mjadara wa Kigoda cha mwlimu Nyerere pale mlimani nilipomsikia katibu Mkuu wa CCM ndugu yetu A . Kinana, akiwaambia watawala wetu wawe tayari kukosolewa na kuomba radhi pale wanapotambua wamekosa!

Kwa wafuatiliaji wa mambo ya siasa za nchi yetu watakubaliana nami kuwa; hali kama ile agharabu haitokei pale ambapo mwenyekiti wa chama anapokuwa ndiye huyo-huyo rais wa nchi pia; hata kama kutakuwepo makosa kibao.

Ndipo nilipogundua kwamba kumbe nchi yetu kuendelea na mtindo wa kuwa na rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama kunasababisha tuwe na ombwe kuu la wakosoaji, watu wenye hurka ya Kinana , naam wale wenye nia njema ya kukosoa kwa kujenga.

Watu wanaochangia kuondoa magugu kwa upande mmoja na upande mwingine wakipalilia ngano ili izidi kustawi katika shamba Tanzania.
Hiki ndicho tulichokuwa tukikimiss kwa mda mrefu huko nyuma.
Mimi nimeipenda hali hii kwa kuwa itamsaidia rais yeyote atakayekuwa madarakani kutoka chama chochote cha siasa katika kuliongoza taifa hili.

Kama nawe wapenda karibu.



Napinga hilo!
Kwa nchi iliyo nyuma kimaendeleo ktk kila eneo Dunia hii tunahitaji Kiongozi mwenye nguvu Serikalini na Chamani ili aweze kupambana na kuyatokomeza Mafisadi kote kote, msijaribu kuiga tu mambo bila ya kuyafikiria, hawo Wazungu ambao mnawaiga jaribuni kuwaelewa hata wao walikuja kubadilisha hii mifumo baada ya tayari kuwa wameshafikia hatua kubwa ya kimaendeleo, baada ya nchi kuwa ina uwezo wa kujiendesha yenyewe, ndiyo maana unaona Ulaya mpaka leo kuna nchi kama Ubelgiji au Uholanzi zinakaa mpaka miezi 6 bila ya Serikali yaani Kiongozi lkn hakuna anayelalamika kutolipwa mshara, huduma zote zipo Mwananchi wa kawaida wala hajui kama kuna Serikali ama la, hapa Tanzania tunaweza kuishi bila Raisi, Waziri Mkuu au kiongozi yoyote yule na nchi iende?

Hivyo hilo siyo jambo baya lkn kwa nchi iliyo bado nyuma siyo jambo jema kulifanya, kwani kitakachotokea ni mvurugano ambayo unaweza kuirudisha nchi nyuma sana na badala ya sasa kutumia muda mwingi kwenye mambo ya kimaendeleo tutakuwa tunatumia muda mwingi kwenye kushughulikia ugomvi wa kichama, HAPANA hatujafikia huwo uwezo wa kuweza kutenganisha kofia mbili, huwo muda utakuja lkn siyo leo!
 
Niwazo zuri, ukiangalia uongozi wa CCM ngazi za chini, mbuge au diwani hawana cheo katika chama, nahisi ni vizuri pia Rais hasiwe na cheo katika chama
 
Back
Top Bottom