Kwa mujibu wa Sheria mpya za madini, CAG hana mamlaka ya kukagua migodi

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,992
17,892
Kwa mujibu wa hizi Sheria mpya za zilizotungwa baada ya ripoti za mchanga wa madini ni kuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kwa sasa hana mamlaka ya kukagua migodi tena.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), Prof. Mussa Assad amesema Sheria mpya ya Madini haimpi ruhusa ya kufanya ukaguzi katika migodi na ameisihi Serikali iifanyie marekebisho.

Aidha, amesema mpaka sasa kuna vyama vya siasa 7 havikuwasilisha taarifa za mahesabu yao.

Pia, CAG amesema madeni ya matibabu nje ya nchi yamekuwa makubwa na yanatishia kusitishwa kwa huduma hiyo, hivyo ameishauri Serikali kulipa haraka madeni hayo ili kuepuka matatizo ikitokea dharura.

My take:
Nashauri hii sheria ifanyiwe marekebisho ili CAG awe na uwezo wa kukagua migodi yote nchini. Mfano ni juzi tu Rais katoka kuzindua ukuta wa Mirerani ambao utalinda madini yasitoroshwe kwenda nje kinyemela.

Hili eneo la ukuta wa Mirerani ni mfano wa maeneo ambayo yalipaswa kukaguliwa na CAG ili kujua tathmini kama wizi wa madini umefanikiwa kudhibitiwa na huo ukuta ama lah.
 
Kama hili ni kweli, basi inathibitisha kwamba huu utawala ni very corrupt na ili kuficha uovu wake; ikaanza kwanza kung'oa mizizi inayoweza kukemea uovu!

Hebu tutafakari haya...

-Uhuru wa maoni upo ICU
-Bunge halina nguvu tena
-Vyama vya upinzani vimepigwa nyundo visiwafikie wananchi
-Wakosoaji wa serikali; wengine wameponea chupuchupu kuuawa na wengine hawajulikani walipo and presumably dead.

Wakati hayo yakifanyika; tukaona efforts binafsi za Mkuu zikifanyika kwenye sekta ya madini with reference to makinikia

Wenye akili timamu wakaona hitilafu zilizomo kwenye efforts zile!

Tunaotumia namba kufanya analysis, tukaona ghiliba zilizojaa kwenye zoezi husika from day one!

Huku na kule, ikatungwa sheria mpya ya madini... wenzangu mimi wakapiga makofi kudhani ni jambo jipya kumbe lipo kwenye sheria ya madini ya 2010 kwamba iwe inafanyika revision after every 5 years!

Leo tunaambiwa eti sheria mpya inamkataza CAG kutia pua yake kwenye sekta ya madini!

BINAFSI, SIAMINI HADI NIIONE SHERIA YENYEWE.

Na kama ni kweli, basi yooooote yale ya kujionesha ana uchungu na sekta ya madini ilikuwa na lengo moja tu: KUPUMBAZA WATU!

HAPANA!

Hapo juu nimeandika kinafiki... nilichokusudia kusema ni: Kuwafanya Werevu kuwa Wajinga na Wajinga kuwa Wapumbavu!

Ni nani anaweza kukihujumu alichokitolea jasho?

Tumejazwa kwamba yupo concerned na sekta ya madini (ref: kutolea jasho) kumbe ni maandalizi ya kuifanyia ufisadi sekta husika!

Unless kama hizi habari za CAG na madini sio sahihi vinginevyo sioni tafsiri yoyote ya hatua hiyo kama sio UFISADI!

Na kv no freedom of speech; watu watashindwa kuongea openly!

Na kv Bunge halina nguvu; hao nao watashindwa kuhoji!

Na kwavile shughuli za siasa zimepigwa nyundo; vyama vyama upinzani vitakosa uwanda mkubwa wa kuelezea uhalifu huu kwa wananchi.

Na kwavile kuna Wakosoaji wameponea chupuchupu kufa; itakuwa ngumu kutokea majasiri wengine kuupinga uharamia huu!

Na kwavile tuna Mwandishi ambae hafahamiki alipo and presumably dead simply because alijitoa mhanga kutaka kufuatilia uovu; ni Mwandishi gani mwingine ata-risk maisha yake kufuatilia uovu huu?!
 
Kwa mujibu wa hizi sheria mpya za mheshimiwa raid zilizotungwa baada ya ripoti ya mchango ni kuwa Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa sasa hana mamlaka ya kukagua migodi tens
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), Prof. Mussa Assad amesema sheria mpya ya Madini haimpi ruhusa ya kufanya ukaguzi katika migodi. Aisihi Serikali ifanyie marekebisho.
-
Aidha, amesema mpaka sasa kuna vyama vya siasa 7 havikuwasilisha taarifa za mahesabu yao.
-
Pia, CAG amesema madeni ya matibabu nje ya nchi yamekuwa kubwa na yanatishia kusitishwa kwa huduma hiyo, hivyo ameishauri serikali kulipa haraka madeni hayo ili kuepuka matatizo ikitokea dharura..

my take: Nashauri hii sheria ifanyiwe marekebisho ili CAG awe na uwezo wa kukagua migodi yote nchini mfano ni juzi tu mheshimiwa raisi katoka kuzindua ukuta wa MERERANI ambao utalinda madini yasitoroshwe kwenda nje kinyemela,
Hili eneo la ukuta wa MERERANi ni mfano wa maeneo ambayo yalipaswa kukaguliwa na CAG ili kujua tathmini kama madini tumefanikiwa kudhibitiwa na huo ukuta kutoroshwa ama lah
Kwanza gharama halisi za kujenga huo ukuta. Pili uhalali wa hizi 'dharura'.
 
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo
 
Mkuu jina lenyewe linajionyesha wapi mipaka ya cag ipo.Yeye ni mkuguzi mkuu wa hesabu za SERIKALI NA TAASIS ZAKE na sio KKAMPUNI BINAFSI.
Taasis pekee ambayo inaweza kufanya ukaguzi kwa mujibu wa sheria ni TRA.
Hivyo sio kweli hata kidogo kwamba sheria mpya ya madini imemzuia cag kufanya ukaguzi kwenye makampuni binafsi.
 
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo
Heee!!miaka yote hiyo alipokuwa ana kagua alikuwa na hao mainjinia?huko kwenye ujenzi wa barabara anakokagua hadi leo ana mainjinia?inaonekana hata hujui nini kazi ya CAG!!wakati mwingine ukimya una ficha mengi!!!daaa kweli elimu elimu,kwani kazi ya CAG ni kujenga mgodi?
 
Hili eneo la ukuta wa MERERANi ni mfano wa maeneo ambayo yalipaswa kukaguliwa na CAG ili kujua tathmini kama madini tumefanikiwa kudhibitiwa na huo ukuta kutoroshwa ama lah
CAG aweza kagua thamani ya jengo? hata ukuta? Ana Quantity Surveryors au watathmini majengo kwenye office yake? Hao wataalamu hana
 
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo
Hujielewi nenda shule Kwanza then utaelewa Wat is the definition of auditing kwani for your fake and minor capacity do you know wat their going to audit? Kwani zamani before sheria kufanyiwa amendments walikuwa wanakagua nini? Have a big mind of thinking sometimes if u have nothing to contribute it's better to be quite rather than thinking to answer and respond on every point be wise man and that's my advice as ur fellow citizen thanks.
 
Heee!!miaka yote hiyo alipokuwa ana kagua alikuwa na hao mainjinia?huko kwenye ujenzi wa barabara anakokagua hadi leo ana mainjinia?inaonekana hata hujui nini kazi ya CAG!!wakati mwingine ukimya una ficha mengi!!!daaa kweli elimu elimu,kwani kazi ya CAG ni kujenga mgodi?
CAG anakagua zaidi matumizi ya pesa hizo barabara kama zilipangiwa milioni kumi kama zilitumika au hazikutumika ,tenda zake ziko sawa nk lakini mambo ya imejengwa kwa viwango au la kiwango cha mchanganyo wa mfano kokoto na lami kiko sahihi huko hayuko atatoroka mbio hana hao wataalamu.Hakagui barabara anakagua matumizi ya hela za barabara
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo

Mkaguzi wa hesabu...

Naomba tu kama ikikupendeza upitie link yao (National Audit Office of Tanzania » About) usome japo in summary mamlaka na upana wa kazi zake.


Mkuu jina lenyewe linajionyesha wapi mipaka ya cag ipo.Yeye ni mkuguzi mkuu wa hesabu za SERIKALI NA TAASIS ZAKE na sio KKAMPUNI BINAFSI.
Taasis pekee ambayo inaweza kufanya ukaguzi kwa mujibu wa sheria ni TRA.
Hivyo sio kweli hata kidogo kwamba sheria mpya ya madini imemzuia cag kufanya ukaguzi kwenye makampuni binafsi.

Ofisi ya CAG naamini ina wataalamu wa PUblic Contract management. Hapo ndipo mkono wake unapoingia kwenye migodi maana kampuni zote zimeingia mkataba na serikali. Kwa kusema hivyo, kama una kampuni binafsi lakini imeingia mkataba na serikali wa kutoa huduma (service or product) kama serikali ilikuwa makini kwenye kuandika mkataba huo ni lazima muweke kipengele cha kukubali kuaguliwa na CAG.

TRA wao wanaangalia very narrowly..kodi imelipwa ama la.

CAG anachambua mahesabu yote na huko ndipo madudu mengi yanapofichwa, si kwenye kodi.

Umenikumbusha kuna wakati nilitamani sana kwenda kusoma hii kozi (Public Contract Management)...nadhani ni wakati muafaka kuirudia ndoto hii.
 
v
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo
itabu vya risiti vitakua vinakaa katikati ya combustion chamber za cylinder head ya grinder machine so kwa hapo CAG anatakiwa awe na ma engineer wa kutosha hasa wa mitambo inayozalisha fikra kama zako!
 
Heee!!miaka yote hiyo alipokuwa ana kagua alikuwa na hao mainjinia?huko kwenye ujenzi wa barabara anakokagua hadi leo ana mainjinia?inaonekana hata hujui nini kazi ya CAG!!wakati mwingine ukimya una ficha mengi!!!daaa kweli elimu elimu,kwani kazi ya CAG ni kujenga mgodi?
Kwa jinsi ulivyoandika nadhani unadhani kulikuwa na sheria ya CAG inayompa mamlaka ya kukagua makampuni binafsi ya madini.

Kwa kukusaidia haijawahi kuwepo sheria ya CAG kukagua kwenye migodi ya makampuni binafsi hapa nchini tokea kuanzishwa kwa CAG.

Kumbuka pia haya makampuni yana mkataba ambao yaliingia kabla hata ya sheria nyingine za madini zilizoletwa na Rais Magufuli.

Sio kwamba serikali haikufahamu umuhimu wa kutunga sheria inayompa mamlaka CAG kuingia kwenye migodi na kufanya ukaguzi bali haikufanya hivyo kutokana na msingi wa faida kwa wote.

Kutunga sheria hiyo kungepelekea makampuni ya madini kufungua kesi katika mahakama za kimataifa kwa sababu hiyo ingekuwa ni kuvuka red line. Hii ingepelekea kushindwa kesi na kujikuta tukidaiwa mabilioni ya pesa kama madai.

Sheria anayosema CAG ingewezekana kama tungekuwa tunaanzisha migodi kwa mara ya kwanza.
 
Kwa jinsi ulivyoandika nadhani unadhani kulikuwa na sheria ya CAG inayompa mamlaka ya kukagua makampuni binafsi ya madini.

Kwa kukusaidia haijawahi kuwepo sheria ya CAG kukagua kwenye migodi ya makampuni binafsi hapa nchini tokea kuanzishwa kwa CAG.
Si migodi binafsi tu bali hata makampuni binafsi hana huo uwezo.
 
We ni universal kichwa maji umeambiwa anaenda kuchimba madini au kukagua hesabu za migodi?
kazi zake ni hizi "the responsibilities of the CAG, is the controllership of funds from the Consolidated Fund and auditing of the use of such funds"

Hiyo migodi ni ya pesa za watu binafsi hakuna hela ya serikali au ya shirika la umma akakague nini? Hakumuhusu
 
Twende turudi CAG ana Mining engineers na mainjinia wengine kwenye office yake wenye utaalamu wa kukagua migodi? Kule Kwa CAG naona kama kumejaa wahasibu tu wakienda mgodini wataishia kukodoa macho tu.Vyombo vingine vifanye kazi hiyo
Wanavyokagua miradi ya maji kwani CAG wana Mafundi Bomba?

Wanapokagua miradi ya kilimo na wizara ya kilimo ina maana wana Mabwana Shamba na Mabwana Mifugo?

Wanapokagua hesabu za sekta ya afya ina ofisi ya CAG ina manesi na madaktari?

Wanapokagua miradi ya ujenzi kwani wana Mafundi Ujenzi kule?

All in all; kama issue ni ofisi ya CAG kutokuwa na hao ma-Engineers; solution ni CAG kumpiga stop asifanye ukaguzi au kumpa manpower itakayomwezesha kufanya ukaguzi?!
 
Back
Top Bottom