Uchaguzi 2020 Kwa mapokezi makubwa anayoyapata Lissu, chondechonde nawaomba NEC na Vyombo vyote vya Dola

Kuna tofauti kati ya mapokezi na wapiga kura. Usisahau hilo tafadhali.
Ingekua hakuna haja ya mapokezi CCM iliyofanya siasa peke yake kwa miaka mitano wasingepita hata kupiga kampeni kwa fedha nyingi na kuwanunua waandishi wa habari na vyombo vyote vya habari na kuwatisha wasanii wote nchini ili wazunguke nao kujaza watu kwenye mikutano.
Nguvu ya vijana kuunga mkono upinzani isipuuzwa ni taarifa mbaya sana kwa wapenda madaraka wanaotegemea wazee walioanzisha CCM ya madaraka.

Tatizo la wapinzani ni kukosa Timu nzuri ya kampeni na pia Wasimamizi wa uchaguzi kuvuruga uchaguzi mapema bila kuchukuliwa hatua yoyote inawakatisha tamaa wapiga kura . Hata kuchukuliwa sheria mkononi ingewatia moyo wapinga dhulma duniani na mbinguni pia. Kuacha dhulma ishamiri ni kuiunga mkono.
 
Nawaomba sana NEC na Vyombo vyote vya Dola, chondechonde kwa idadi ya Watanzania wanaojitokeza kumpokea na kumsikiliza Lissu kwa furaha na mapenzi yao ya dhati kwake na kwa chama chake nawaomba sana enyi watumishi wa NEC na Majeshi yetu, ruhusuni Haki ichukue mkondo wake, msiwanyime Watanzania haki yao ya kuongozwa na mtu wanaemtaka. Msiwanyime maelfu kwa mamilioni ya Watanzania furaha kwa kuwabadilishia mtu wanaemtaka na kumweka mtu wasiyemtaka.

Hata kikiingia chama kingine madarakani stahiki zenu mtapata tu, tena yaweza kuwa zaidi. Na mtu akishashindwa kihalali hawezi kuwafanya lolote,msiogope. Umati wote unaojitokeza kumlaki Lissu kuwakosesha Raha Mungu hata kaa kimya nasema.

Au maafa yakitokea kwa umati huo kuona umedhulumiwa, nyie mtapata faida gani kiuchumi na kiroho? Tazameni mapokezi ya Lissu tangu anarudi nchini na hata sasa wakati wa Kampeni,tazama Kawe,Arusha na leo Mwanza.

Kama atashindwa kihalali sawa, nyie simamieni Haki, lakini kama atashinda, mpeni Haki yake nanyi mtapata heshima ya milele na tuzo huko kwa Mungu.

Najua hata sasa hivi hatendewi Haki mtu huyu, kwa sababu hujuma juu yake Ni kubwa mno, kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea,ingawa bado watu wengi sana wanamuunga mkono.

Enyi NEC na Vyombo vya dola ruhusuni Haki itendeke.
Ni gharama nafuu mno kuruhusu Haki itendeke, lakini Ni gharama kubwa mno kuzuia Haki isitendeke.

Mkiruhusu Haki ikatendeka, mtakumbukwa Kama mashujaa wa Haki. Nayo majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu.

Vizazi vijavyo vitapenda kusoma habari zenu kwa furaha na majigambo,nayo mataifa yataja jifunza juu ya maamuzi yenu ya haki, nanyi mkiendelea kuheshimika.
Kamanda umenena hiyo haina ubishi,nchi hii imeenda kwa chadema wapende au wasipende
 
1599104215503.png
 
Mm nawashangaa sana CHADEMA, hivi kwa mawazo tu ya kawaida yaani hadi Salum Mwalimu form 4 failure awe mgombea mwenza, huwa mnajiaibisha sana.. Mmeshindwa kuchagua wagombea bora, mnatulea watu wasio na uwezo wowote hata nukta, Lissu atleast anaweza kuongea kama akitulia, ila jazba na kuumizwa kwake inamfanya asiwe settled mentally, anaongea kwa kuziacha hoja na kurukia personal attacks.. Chadema bado hamjaweza kuchagua wagombea, yaani nilichoka hadi Salum anagombea umakamu? Acheni utani nyie
 
Mapokezi 🍺🍺🍺🍺
Kujiandikisha 🥃🥃🥃🥃
Msiende kujiandikisha Hadi kuwe na tume huru ya uchaguzi mlevi mmoja alisikika anasema
 
Baada ya October 28 pengine ndio utaweza kunielewa.
Bila shaka tutaelewana tu. Kwa kuwa sababu za kuelewana zipo nyingi zaidi kuliko za kutoelewana. Ukosefu wa tume huru ya uchaguzi, matumizi ya vyombo vya dola nk. ni miongoni mwa sababu za kutufanya tuelewane baada ya October 28. Vinginevyo wewe ndiye usingenielewa baada ya hapo.
 
Nawaomba sana NEC na Vyombo vyote vya Dola, chondechonde kwa idadi ya Watanzania wanaojitokeza kumpokea na kumsikiliza Lissu kwa furaha na mapenzi yao ya dhati kwake na kwa chama chake nawaomba sana enyi watumishi wa NEC na Majeshi yetu, ruhusuni Haki ichukue mkondo wake, msiwanyime Watanzania haki yao ya kuongozwa na mtu wanaemtaka. Msiwanyime maelfu kwa mamilioni ya Watanzania furaha kwa kuwabadilishia mtu wanaemtaka na kumweka mtu wasiyemtaka.

Hata kikiingia chama kingine madarakani stahiki zenu mtapata tu, tena yaweza kuwa zaidi. Na mtu akishashindwa kihalali hawezi kuwafanya lolote,msiogope. Umati wote unaojitokeza kumlaki Lissu kuwakosesha Raha Mungu hata kaa kimya nasema.

Au maafa yakitokea kwa umati huo kuona umedhulumiwa, nyie mtapata faida gani kiuchumi na kiroho? Tazameni mapokezi ya Lissu tangu anarudi nchini na hata sasa wakati wa Kampeni,tazama Kawe,Arusha na leo Mwanza.

Kama atashindwa kihalali sawa, nyie simamieni Haki, lakini kama atashinda, mpeni Haki yake nanyi mtapata heshima ya milele na tuzo huko kwa Mungu.

Najua hata sasa hivi hatendewi Haki mtu huyu, kwa sababu hujuma juu yake Ni kubwa mno, kuliko Uchaguzi wowote uliowahi kutokea,ingawa bado watu wengi sana wanamuunga mkono.

Enyi NEC na Vyombo vya dola ruhusuni Haki itendeke.
Ni gharama nafuu mno kuruhusu Haki itendeke, lakini Ni gharama kubwa mno kuzuia Haki isitendeke.

Mkiruhusu Haki ikatendeka, mtakumbukwa Kama mashujaa wa Haki. Nayo majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu.

Vizazi vijavyo vitapenda kusoma habari zenu kwa furaha na majigambo,nayo mataifa yataja jifunza juu ya maamuzi yenu ya haki, nanyi mkiendelea kuheshimika.
Tukapige Kura ya ndio kwa wingi
 
Kina Halima Mdee, Msigwa, Bulaya na Mbowe wanaposhinda majimboni tume inakuwa na wajumbe kutoka sayari ya Jupiter?.

Acheni kudekadeka hovyo.
Mkuu! Inawezekana wewe haupo Tanzania. Hapa hoja yetu ipo kwenye uraisi, ni lini Mbowe au Mnyika alishinda uraisi halafu akatangazwa? Watumishi wote wa tume ni wateule wa Mwenyekiti wa CCM. Una la ziada hapo? Ni lazima wafanye kazi kadiri ya maelekezo ya bosi wao. Tume huru ambayo itatokana na watu wasioegemea upande mmoja, ndiyo ingekuwa dawa ya maigizo haya.
 
Bado sana Lissu,tena bado hata robo,mafuriko ya Lowasa hayajawai kufikiwa kwenye historia ya Tanzania.
 
Mbowe na Mnyika wanashindwa kuhakikisha CHADEMA inakuwa hai nchi nzima wanaweza kweli kuwa na hadhi ya urais?.

Tuache utani yanapokuja masuala makini na makubwa.
Mkuu,ndiyo maana nimekuambia inawezekana wewe haipo dunia hii tunayoishi sisi kwa kuwa dunia nzima inajua kuwa vyama vya upinzani vilikatazwa kufanya siasa kwa miaka mitano iliyopita,wangewezaje kuieneza CHADEMA nchi nzima? Ninyi mmefanya siasa wenyewe,lakini hofu tele zimewajaa,mnaogopa nini?
 
Back
Top Bottom