Pole sana kwa matatizo yanayokukuta kaika umri wako huu mdogo.
Naomba kwanza nikushauri kitu. Katika mmaisha yako yote, kwanza jifunze uvumilivu hasa wakati wa shida. Usipende kutafta suluhu za muda mfupi katika matatizo yako maana mwisho wake siku zote huwa mbaya.
Yes hauna baba lakini nina imani unao ndugu wa baba au mama au hata ndugu zako wa tumbo moja. Je, umeshaongea nao hao kwanza? Pili, kama webgine walivyokuuliza, unaishi wapi kwa sasa? Je umeshauona uongozi wa eneo unaloishi? Ni rahisi sana kupata msaada katika eneo unaloishi kuliko kuja kuomba msaada humu ambapo humfahamu mtu yeyote. Ninaelewa kuwa baadhi ya koo/familia/ndugu hawajaliani, ila kuna sehemu nyingi unaweza kupata msaada.
Kama wewe ni mkristo, natumaini unafahamu kuwa kuna jumuiya kila mtaa. Hebu uone uongozi wa jumuiya yako nina hakika WATAKUSAIDIA! Ninaongea hayo nikiwa na uhakika kwa sababu mimi ktk jumuiya yangu tunasomesha vijana 2 waliofiwa na wazazi wao, ambao walikuwa wanajumuiya wenzetu. Tulianza nao wakiwa kidato cha pili na mwaka huu wanamaliza kidato cha nne! Anza hapo nina hakika utapata msaada as msaada usiokuwa na masharti!!