Kwa hiyo Jangwani kunajengwa Soko la Machinga au Uwanja wa Mpira?

Kwa hiyo Jangwani kunajengwa Soko la Machinga au Uwanja wa Mpira?

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,621
Reaction score
6,510
Ukiacha maswali juu ya usalama na ufanisi wa kuweka mradi wowote wa kijamii maeneo ya Jangwani, kumekuwa na mkanganyiko juu ya ni mradi gani hasa unajengwa maeneo hayo.

Juzi nimemsikia Samia anawahakikishia machinga kuwa mradi wa kuwajengea soko kubwa pale Jangwani uko pale pale.

Pia soma Rais Samia: Serikali kujenga Soko kubwa kama la Kariakoo eneo la Jangwani

Wakati huo huo, Yanga imeendelea na mauzauza yake ya kusema wanaenda kujenga uwanja mkubwa maeneo yale. Tena wamefikia hatua ya kutuambia wanaenda kujenga uwanja wenye hadhi ya kuchezewa hadi AFCON na fainali zingine za CAF!

Ni mimi pekee ninayeona tunadanganywa?
 
Jangwani Kuna eneo kubwa sana mjomba

Wanaweza ongeza hata chuo na hospital na bado pakatosha

Huenda hupajui wewe jangwani huwa unapaona ukiwa unapita tu kwenye gar
 
Jangwani Kuna eneo kubwa sana mjomba

Wanaweza ongeza hata chuo na hospital na bado pakatosha

Huenda hupajui wewe jangwani huwa unapaona ukiwa unapita tu kwenye gar
Na hapo hapo kuwe na mradi wa bonde la msimbazi? Jangwani kuna nyayo zangu pale wakati wewe ulikuwa bado upo kwenye mfumo wa maji maji ya uteee.
 
Ukiacha maswali juu ya usalama na ufanisi wa kuweka mradi wowote wa kijamii maeneo ya Jangwani, kumekuwa na mkanganyiko juu ya ni mradi gani hasa unajengwa maeneo hayo.

Juzi nimemsikia Samia anawahakikishia machinga kuwa mradi wa kuwajengea soko kubwa pale Jangwani uko pale pale.

Wakati huo huo, Yanga imeendelea na mauzauza yake ya kusema wanaenda kujenga uwanja mkubwa maeneo yale. Tena wamefikia hatua ya kutuambia wanaenda kujenga uwanja wenye hadhi ya kuchezewa hadi AFCON na fainali zingine za CAF!

Ni mimi pekee ninayeona tunadanganywa?
Hivi kwa nini kila mahali tunataka tujenge? Jangwani ingeachwa kama bustani. Mto ungesafishwa, pange pandwa miti ya asili na kuwekwa sehemu za watu kutembea. Ingegeuzwa kuwa Central Park au Uhuru Park yetu. Mji ungepumua, na mafuriko yangepungua. Miji yote ya maana yana sehemu ya kupumulia. Sisi hata eneo la ufukweni kama Coco tunalijenga na kulibinafsisha tukiamini kuwa hayo ndio maendeleo. Kwa kweli tunasikitisha.

Amandla...
 
Hivi kwa nini kila mahali tunataka tujenge? Jangwani ingeachwa kama bustani. Mto ungesafishwa, pange pandwa miti ya asili na kuwekwa sehemu za watu kutembea. Ingegeuzwa kuwa Central Park au Uhuru Park yetu. Mji ungepumua, na mafuriko yangepungua. Mimi yote ya maana yana sehemu ya kupumulia. Sisi hata eneo la ufukweni kama Coco tunalijenga na kulibinafsisha tukiamini kuwa hayo ndio maendeleo. Kwa kweli tunasikitisha.

Amandla...
Matajiri na wanasiasa wa kiswahili walivyo na uchu wa ardhi. Wakiona kipande cha ardhi mate yanawadondoka.
 
Hivi kwa nini kila mahali tunataka tujenge? Jangwani ingeachwa kama bustani. Mto ungesafishwa, pange pandwa miti ya asili na kuwekwa sehemu za watu kutembea. Ingegeuzwa kuwa Central Park au Uhuru Park yetu. Mji ungepumua, na mafuriko yangepungua. Mimi yote ya maana yana sehemu ya kupumulia. Sisi hata eneo la ufukweni kama Coco tunalijenga na kulibinafsisha tukiamini kuwa hayo ndio maendeleo. Kwa kweli tunasikitisha.

Amandla...
Kigali kuna park wamejenga kwenye eneo kama hilo la Jangwani. Hawa viongozi wanavyozunguka huko nchi za watu sijui kwa nini hawajifunzi na kuona umuhimu wa kuwa na vitu kama hivi.
WA_1771229738842.jpeg
 
Jangwani Kuna eneo kubwa sana mjomba

Wanaweza ongeza hata chuo na hospital na bado pakatosha

Huenda hupajui wewe jangwani huwa unapaona ukiwa unapita tu kwenye gar

Tena wanaweza jenga viwanja hata vitano vya mpira standard ya Fifa, wakajenga na masoko makubwa hata matatu na wakaacha maeneo ya kufanyia mikutano ya wazi. Huwa panatanuka pale. Napajua.
 
Hivi kwa nini kila mahali tunataka tujenge? Jangwani ingeachwa kama bustani. Mto ungesafishwa, pange pandwa miti ya asili na kuwekwa sehemu za watu kutembea. Ingegeuzwa kuwa Central Park au Uhuru Park yetu. Mji ungepumua, na mafuriko yangepungua. Mimi yote ya maana yana sehemu ya kupumulia. Sisi hata eneo la ufukweni kama Coco tunalijenga na kulibinafsisha tukiamini kuwa hayo ndio maendeleo. Kwa kweli tunasikitisha.

Amandla...

Awethu !✊
 
Ukiacha maswali juu ya usalama na ufanisi wa kuweka mradi wowote wa kijamii maeneo ya Jangwani, kumekuwa na mkanganyiko juu ya ni mradi gani hasa unajengwa maeneo hayo.

Juzi nimemsikia Samia anawahakikishia machinga kuwa mradi wa kuwajengea soko kubwa pale Jangwani uko pale pale.

Pia soma Rais Samia: Serikali kujenga Soko kubwa kama la Kariakoo eneo la Jangwani

Wakati huo huo, Yanga imeendelea na mauzauza yake ya kusema wanaenda kujenga uwanja mkubwa maeneo yale. Tena wamefikia hatua ya kutuambia wanaenda kujenga uwanja wenye hadhi ya kuchezewa hadi AFCON na fainali zingine za CAF!

Ni mimi pekee ninayeona tunadanganywa?
Mpira hapana ...jangwani ni karibu na cbd
 
Eneo la jangwani linatakiwa kufukiwa na kuwekwa level na kujengwa gadeni, chini mto ...ni swala la kiinjinia tu
Sina utaalamu wa kiinjinia ila sidhani kama watafukia na kuweka level. Nadhani wazo watakalolifanyia kazi ni kutengeneza mkondo wa maji katikati halafu pembeni kujenga miti na bustani.
 
Hivi kwa nini kila mahali tunataka tujenge? Jangwani ingeachwa kama bustani. Mto ungesafishwa, pange pandwa miti ya asili na kuwekwa sehemu za watu kutembea. Ingegeuzwa kuwa Central Park au Uhuru Park yetu. Mji ungepumua, na mafuriko yangepungua. Miji yote ya maana yana sehemu ya kupumulia. Sisi hata eneo la ufukweni kama Coco tunalijenga na kulibinafsisha tukiamini kuwa hayo ndio maendeleo. Kwa kweli tunasikitisha.

Amandla...
Naunga mkono hoja

Ova
 
Back
Top Bottom