Kwa hili simuungi mkono Lema!

Kwa hili simuungi mkono Lema!

manuu

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2009
Posts
4,064
Reaction score
10,745
Katika mkutano uliyofanyika Arusha maeneo ya kilombero,
Nilimsikia Mh:Lema akihutubia aliongea mambo mengi sana yenye tija kwa maslahi ya wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama,Wakati akiendelea kuhutubia alisema,"Ndugu zangu wamachinga pamoja na kupelekwa katika viwanja vya NMC mi sijaridhika na mkae karibu na Redio zenu mkisikia nimerudishiwa kiti changu cha ubenge wote mrudi mlipokuwa mkifanya biashara zenu na migambo wakiwasumbua andamaneni mje ofisini kwangu"
Mwisho wa kunukuu.
Na kweli baada ya Lema kurudishiwa kiti chake wamachinga wametoka kule NMC na kurudi katikati ya mji kitu ambacho kinaleta usumbufu na kero kubwa kwa watumiaji barabara wengine.
Mfano kwenye ile barabara ya Shekh Amr Abeid kama unashuka stnd kubwa, Wamachinga wanafanya biashara mpaka njia ya wapita kwa miguu inakosekana inabidi wapita kwa miguu wapite katikati ya Barabara kitu kinachohatarisha maisha ya watembea kwa miguu.
WITO WANGU:
Wakati umefika sasa wa kuacha siasa za vyama,Jambo hata kama limefanywa na CCM na lina tija kwa wananchi wote lisipingwe ili tu kuonyesha kubishana,kwani wamachinga walivyopelekwa kule NMC mji ulikuwa safi sana na hata mzunguko wa hewa ulikuwa mzuri.
Sasa hivi baada ya kurudi katikati ya mji imekuwa kero kero kero.

 
Katika mkutano uliyofanyika Arusha maeneo ya kilombero,
Nilimsikia Mh:Lema akihutubia aliongea mambo mengi sana yenye tija kwa maslahi ya wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama,Wakati akiendelea kuhutubia alisema,"Ndugu zangu wamachinga pamoja na kupelekwa katika viwanja vya NMC mi sijaridhika na mkae karibu na Redio zenu mkisikia nimerudishiwa kiti changu cha ubenge wote mrudi mlipokuwa mkifanya biashara zenu na migambo wakiwasumbua andamaneni mje ofisini kwangu"
Mwisho wa kunukuu.
Na kweli baada ya Lema kurudishiwa kiti chake wamachinga wametoka kule NMC na kurudi katikati ya mji kitu ambacho kinaleta usumbufu na kero kubwa kwa watumiaji barabara wengine.
Mfano kwenye ile barabara ya Shekh Amr Abeid kama unashuka stnd kubwa, Wamachinga wanafanya biashara mpaka njia ya wapita kwa miguu inakosekana inabidi wapita kwa miguu wapite katikati ya Barabara kitu kinachohatarisha maisha ya watembea kwa miguu.
WITO WANGU:
Wakati umefika sasa wa kuacha siasa za vyama,Jambo hata kama limefanywa na CCM na lina tija kwa wananchi wote lisipingwe ili tu kuonyesha kubishana,kwani wamachinga walivyopelekwa kule NMC mji ulikuwa safi sana na hata mzunguko wa hewa ulikuwa mzuri.
Sasa hivi baada ya kurudi katikati ya mji imekuwa kero kero kero.



Mkuu simtetei lema, lengo langu kudadisi ukweli basi.

Kila kauli huwa na sababu, je umedadisi ni sababu zipi unadhani zilipelekea Lema kutoa kauli hiyo?
 
Nakubaliana na wewe kuhusu kero za wafanyabiashara barabarani, lakini hata huko walikopelekwa uwanja wa NMC hakufai pia. Umepita hapo hivi karibuni? Wamachinga walipelekwa huko kwa lengo moja tu: Kuwanyima CHADEMA sehemu ya kufanyia mikutano yao, PERIOD. Pakiachwa hivyo palipo patakuwa ni mazalia ya kipindupindu na madhara yake yatakuwa ni kwa Arusha nzima.
 
Kwa hoja ni mji uwe safi hata kama wamachinga wanateseka? Kweli akili ni nyweli,kila mtu ana zake!
 
Mkuu simtetei lema, lengo langu kudadisi ukweli basi.

Kila kauli huwa na sababu, je umedadisi ni sababu zipi unadhani zilipelekea Lema kutoa kauli hiyo?
sababu kubwa ni kwamba NMC hapafai mf. mvua ikinyesha hapakaliki
 
Watu wengi huwa wanapotosha dhana nzima ya umachinga. Hizi ni biashara za kutembeza na siyo za kufungua duka barabarani. Tuwe wastaarabu.
Kuhusu Lema, yeye hana uwezo wa kuruhusu watu kufanya biashara barabarani, kwa hiyo siwezi kumlaumu.
Nailaumu halmashauri ya jiji la Arusha kwa either kushindwa kutunga sheria au kushindwa kuenforce sheria.
 
Katika mkutano uliyofanyika Arusha maeneo ya kilombero,
Nilimsikia Mh:Lema akihutubia aliongea mambo mengi sana yenye tija kwa maslahi ya wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama,Wakati akiendelea kuhutubia alisema,"Ndugu zangu wamachinga pamoja na kupelekwa katika viwanja vya NMC mi sijaridhika na mkae karibu na Redio zenu mkisikia nimerudishiwa kiti changu cha ubenge wote mrudi mlipokuwa mkifanya biashara zenu na migambo wakiwasumbua andamaneni mje ofisini kwangu"
Mwisho wa kunukuu.
Na kweli baada ya Lema kurudishiwa kiti chake wamachinga wametoka kule NMC na kurudi katikati ya mji kitu ambacho kinaleta usumbufu na kero kubwa kwa watumiaji barabara wengine.
Mfano kwenye ile barabara ya Shekh Amr Abeid kama unashuka stnd kubwa, Wamachinga wanafanya biashara mpaka njia ya wapita kwa miguu inakosekana inabidi wapita kwa miguu wapite katikati ya Barabara kitu kinachohatarisha maisha ya watembea kwa miguu.
WITO WANGU:
Wakati umefika sasa wa kuacha siasa za vyama,Jambo hata kama limefanywa na CCM na lina tija kwa wananchi wote lisipingwe ili tu kuonyesha kubishana,kwani wamachinga walivyopelekwa kule NMC mji ulikuwa safi sana na hata mzunguko wa hewa ulikuwa mzuri.
Sasa hivi baada ya kurudi katikati ya mji imekuwa kero kero kero.

Tatizo si Lema, bali ni sera mbaya za serikali iliyoko madarakani. Kwanini hao wamachinga wanakimbilia mjini?
 
Mgambo wako wapi jamani, si watembeze viboko mpaka ofisini kwa Lema. Naona huyu amerudia siasa za fujo,safari hii serikali itamshughulikia kiume, ni kupiga mpaka anasahau nyumbani.
 
kidukumu umekosa la kuandika humu?leta mada zenye mawazo mapya,achana na mawazo mtumba
 
Lema hakuwahi kutegemea bunge kwenye swala hilo kwani alicho kuwa akikifanya ni kuwaunganisha wawe kitu kimoja ndiyo maana baada ya ule mkutano walienda kupabomoa pale kwenye eneo alilo nunua Mramba wakati ndiyo sehemu inayopaswa kuwa soko..juu ya mama zetu kucharazwa viboko na mgambo ni kitu ambacho hakivumiliki na siku ya mkutano Lema aliwalaumu sana kwa kutegemea mbunge kuwatete ikumbukwe walishaandamana zaidi ya mara 3, Lema akiwa amesimamishwa
 
kero kwako wewe tu!wale wamachinga wanawauzia nani bidhaa zao?
 
Mgambo wako wapi jamani, si watembeze viboko mpaka ofisini kwa Lema. Naona huyu amerudia siasa za fujo,safari hii serikali itamshughulikia kiume, ni kupiga mpaka anasahau nyumbani.
Yaani wewe inaonekana huna management and leadership skills hata kidogo,inaonekana unaamini kutumia nguvu zaidi ya kutumia akili.Pole sana kwa hili mkuu!
 
Kobello na manuu sakata la machinga manispaa ililifanya la kisiasa ikumbukwe mgombea wa ccm aliwahi kupigwa matango na mama hao sasa baada ya leo kusimamishwa wakawa wanawaambia mlikuwa mnajivunia lema sasa hayupo sasa katika hali hiyo unategemea nini? lema anachotaka kwanza waonyeshwe eneo husika la kufanyia biashara zao lakini siyo kihuni huni tu unawapeleka kwenye dimbwi eti ndiyo weke biashara zao hao..hakuna vyoo,maji,hapatoshi,vua ikinyesha hapafai
 
Last edited by a moderator:
pia Lema alisema kama wamachinga wakikamatwa sheria zifutwe siyo mtu unamnyanganya bidhaa zake saa tatu ya usiku then kesho akizifatilia manispaa hazikuti sasa hapo hao mgambo si ni uizi tu na nani aliwapa haki yakuwapiga viboko.

Najua iko siku hapa Arusha patatifuka ni siku mgambo watakapo tumia nguvu..
 
Hakuna tatizo wapange mitaa yote mpaka mbele ya maduka Lema yupo hakuna tatizo.
 
Machinga hata beijin na chenzen wapo kibao mjini

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom