kumbe kweli........mtanzania hapendi kuambiwa ukweli
hivi yale ma BMW anayotumia katika msafara wake ni ya bei rahisi au?sijamuelewa anamaanisha mtanzania/watanzania wepi wanaopenda anasa
Huo ukweli angeanza kuutekeleza yeye. Angepunguza safari zisizo na tija na hizo pesa zinunue matreka yawekwe Mwanza, Moshi, Arusha, Moro, Mbeya, Iringa, Rukwa na Ruvuma uone kama hajakaa wiki moja na kununuliwa yote.
Hiyo ni demagogue politics ambayo ni trick ya zamani sana, unawaambia watu wasifanye ambacho wewe unafanya sijui maana yake nini. Yeye mwenye anauwezi mkubwa wa kununua hayo matrekta sijui amenunua mangapi. Na sijui kama kuna hata moja huko Chalinze au bagamayo. Mkuu anatakiwa aoneshe mfano yeye.
hivi yale ma BMW anayotumia katika msafara wake ni ya bei rahisi au?sijamuelewa anamaanisha mtanzania/watanzania wepi wanaopenda anasa
labda na yeye ni miongoni mwa wapenda anasa kwa sababu hakueleza bayana.
lakini ukweli uko pale pale kuwa hivi ni asilimia ngapi ya watz tunaheshimu kilimo? wengi tunafikiria kufanya biashara ndogondogo ambazo ni rahisi za kuuza vitu ready made kutoka china.
tuna manpower kubwa lakini ipo under utilized. kuna vijana huko barabarani ana kifuko kimoja cha apples, mwingine ana sabuni 2 za kuogea na wengi wapo tu wanazunguka zunguka kuibia watu. hivi kweli tunatarajia miujiza kwamba kuna Rais atatokea abadilishe haya mazingira kirahisi?
LETS THINK TWICE
nafikiri changes/atitude zibadilike kwa pande zote watu &serikali