Kwa hili la Yanga sc, CHADEMA tumepuyanga

Kwa hili la Yanga sc, CHADEMA tumepuyanga

mwehu ndama

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2019
Posts
1,413
Reaction score
5,150
Licha ya kuwa Mimi ni mwanachama hai na kindakindaki wa CHADEMA, ila siungi mkono na nalaani vikali barua yetu yakuishitaki Yanga sc huko Fifa!

Nasema kwa hili la Yanga sc ,mmepuyanga , Yanga inaviongozi ,wanachama na mashabiki. Hayo yaliyofanywa yalifanywa na raisi wetu Eng.Hersi kwa utashi wake..Mngetafuta namna ya kumshitaki yeye na kamati yake na sio KUINGIZA timu nzima katika harakati za kisiasa ambazo Hadi sasa hazijawa na tija yoyote.

Kinachoonekana sasa ni kile kile cha miaka yote , kufanya siasa za matukio na mihemko..hivi hata kama Eng.Hersi angechangia yeye kama yeye au taasisi ya Yanga sc kuchangia kwa hao fisiemu sisi kama CHADEMA inatuuma nin?..

Je bila huo mchango LISSU angeachiwa huru.??bila huo mchango reform zingepatikana?..Hizi ni siasa za kipumbavu .Na kwa jinsi ninavyoipenda Yanga sc , Niko radhi kukishitaki chama changu cha CHADEMA na kuleta migogoro isiyokwisha hapo chamani.

Soma Pia: Barua ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwenda FIFA

Yanga inatupa tuliowengi furaha kuliko nyinyi mnaopigania matumbo ya familia zenu. Msijasahaulishe nakufikiri watu wanapenda siasa kuliko mpira , na haijawahi tokea , isipokuwa kama chama cha siasa ni lazima muwe na namna yakuyaendea mambo kwa weledi pasipo kuzua taharuki za kipumbavu. Infact sio lazima Kila shabiki wa Yanga sc au kiongozi wa Yanga sc aipende CHADEMA au CCM na hiyo ndio demokrasia tuyapigania, uhuru wa watu kufanya wayapendayo pasipo kuingilia uhuru wa wengine.
 
nimekuwa na mawazo kama yako mkuu.
1. CHADEMA walipaswa kufanya tafakuri ya kutosha kabla ya kuliendea suala hili.
2. Ni kweli Yanga wamekosea kwa walichokifanya, lakini CHADEMA wamekosea zaidi. CHADEMA wanapaswa kufahamu kuwa Yanga wana washabiki wengi kwenye nchi hii (pengine robo au nusu ya Watanzania wote).
3. Kama ikitokea Yanga wakafungiwa na FIFA kwa sababu ya mashtaka ya CHADEMA basi ni wazi kuwa mashabiki wa Yanga watakuwa na hasira na chuki dhidi ya CHADEMA.
4. CHADEMA wanapaswa kufahamu kuwa Watanzania wengi wanapenda hizi timu mbili (Simba na Yanga) zaidi ya wanavyopenda siasa.
5. kujiingiza kwenye mgogoro dhidi ya Yanga ni sawa na kujiharibia wenyewe.
Mimi ni mfuasi wa CHADEMA na shabiki wa Yanga pia
 
Kwa Utashi wake ?? Huku ametumia brand ya team !?

Wee Jamaa vipi Shule ulikwenda kusomea Ujinga !?
 
Kwa Utashi wake ?? Huku ametumia brand ya team !?

Wee Jamaa vipi Shule ulikwenda kusomea Ujinga !?
Wew nae kichwa unabeba kama helmet, Brand ya timu hata wew si unaweza itumia kwa utashi wako bila shinikizo la mtu..?Mfano Ile video yako iliyovuja ukiwa unapakuliwa nnya , c ulijitaja wewe ni Yanga damu?..sasa pale ulitumwa na wanayanga?
 
Back
Top Bottom