Kwa hili hapana!

Kwa hili hapana!

Bornvilla

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2011
Posts
924
Reaction score
272
Watu wanamiminika Loliondo,tamko kwa waislam msiende huko,kakobe hiyo ni deci,askofu mpemba loliondo ni uchawi,wengine mbona shekhe yahaya? Nianze na waislam.Waislam mtume na nabii wa mwisho ni Muhammad(s.a.w) hivyo hakuna ndoto wala ujumbe zaidi ya maandiko matakatifu yaliyoachwa. Ili kuwa mtume na nabii utapata ndoto za kweli na pia kutokewa na kuletewa ujumbe na malaika Gabriel(Jibrili). Kwakuwa utume na unabii ulishafungwa wote wanaokuja kwa staili hiyo hao ni wafuasi wa shetani,na mashetani ndio wanaowaletea ndoto hizo. Wengi tu wameoteshwa ndoto na mashetani na waliyoota yakatokea.Kuhusu Shekhe Yahaya anayofanya kwa mujibu wa uislam anayofanya ni kazi ya shetani na ni ushirikina ambao umepigwa vita na uislam.Anatumia elimu yake kupotosha uislam na kufundisha uchawi,ambapo Qur'an inasema wazi kuwa watu wanamna hiyo watatumikia motoni milele. Kwa upande wa loliondo kwa waislam hiyo ni haramu.Kwa wakristo hivi sasa kumezuka wimbi kubwa sana la manabii wa uongo na wachawi wakubwa.Madhehebu safi sasa za kikristo zinahesabika.Mfano ni hapa jijini Mwanza ambapo manabii wauongo wametia nanga sasa wanahaha baada ya kufichuliwa kwa shuhuda nyingi zinazotolewa kwaneema fm.Mengi niwaachie wachangiaji kwani ndio wanaojua mengi zaidi,na itatusaidia sisi wote kujifunza,kwani lengo kuu ni kuupata ule ufalme wa mbinguni.Haya na tuongozane.
 
Hata yesu alisema nitarudi kupitia wanangu nitakaowateua mimi mkiwaamin wao mtaniamin mimi pia. hao wanaodai mch wa loliondo ni muongo watakuwa wana matatizo mch hakuweka bango lolote wala hakujitangaza
 
Hata yesu alisema nitarudi kupitia wanangu nitakaowateua mimi mkiwaamin wao mtaniamin mimi pia. hao wanaodai mch wa loliondo ni muongo watakuwa wana matatizo mch hakuweka bango lolote wala hakujitangaza

nilivyomfahamu mtoa mada, babu wa loliondo anafanyiakazi ndoto za shetani.
 
Dhibitisha kwamba ni uchawi. Je kama afanyayo ni kwa neema ya mungu,wewe uliyemtukana na kumdhihak utajfcha wap?
 
Hili la loliondo lisituchanganye vichwa. Babu aendelee na kazi yake, wanaoamini watapona. Kama huamini acha wanaoamini tu/wapate huduma. Wengine wanaamini maneno ya yesu wengine ya mtume mohamed, mbona siku zote tu wapole hatuhoji juu ya tofauti za kiimani katka hilo la mtume mohamed na Jesus? Sasa la babu linatugusa kiasi gani mpaka kumpinga? Babu endelea kufanya kama ulivyooteshwa.
 
Kwani tatizo liko wapi? Mwache Babu atoe huduma zake. Hawajatangaza redioni wala magazetini kuhusu huduma yake. Watu wachache walienda kwake wakapata dawa wakapona na kuwaanmbia wengine. Mimi sioni tatizo kama kweli watu wanapona, I dont care amepata wapi ndoto hiyo. Ukimuona ndugu yako ana cancer au Ukimwi ukaambiwa kuna mtu anaweza kumsaidia, kama kweli una uchungu na ndugu yako hautauliza mtoa dawa kapata wapi uwezo, utafanya liwezekanalo kumsaidia.
 
Bornvilla hebu weka mambo hadharani nasikia huko mwanza kuna makanisa ambayo ibada zao zinaendeshwa na mtumishi ambaye baadaye anageuka kuwa joka kubwa watu wanapofumba macho kuomba. Kuna ukweli juu ya hilo?
 
huyo aliyeleta mada ni mpumbavu anaingiza imani za kidini kwa kuwa dini zao zinaamin mashetan(majin) Babu siyo sheikh yahya wala sheik sharif ambaye amekuwa brazamen wa ukonga.
 
Bornvilla hebu weka mambo hadharani nasikia huko mwanza kuna makanisa ambayo ibada zao zinaendeshwa na mtumishi ambaye baadaye anageuka kuwa joka kubwa watu wanapofumba macho kuomba. Kuna ukweli juu ya hilo?
Tupeni habari zaidi!!
 
Kwa hili la makanisa ya kishetani Mwanza, hii ni habari nzito sana tena sana.Naona kuna mtu hapo juu kanitukana ila abarikiwe sana.Najua nikiweka siri hizo za makanisa haya hapa Mwanza,nitatukanwa kupita kiasi kwani kuna baadhi hapa hawataki ukweli hata maramoja,na hasa ukweli unaogusa hisia zao.
 
Back
Top Bottom