Kwa hili, Dr. Slaa wewe ni 'Mdini' pia!

Kwa hili, Dr. Slaa wewe ni 'Mdini' pia!

Status
Not open for further replies.
Eti kwa macho na masikio yako ulishuhudia slaa akiomba kura kupitia maaskofu!?!

Tumwogope Mungu jaman!!
Hivi ule waraka uliotolewa na maaskofu uliwahi kuusoma?!

Nakumbuka mwanahalisi wali'compare na ku'contrast nyaraka hizi zilizotolewa na viongozi wa dini! Sidhani kama ulipata nafasi ya kupitia hilo gazeti.

Tusiandike vitu kwa sababu tu tunaingiza elfu saba!!


Mimi nadhani kuna baadhi yetu(Jamii forum) tunania ya uchochezi na uwongo! Hivi kweli kusema Dr. Slaa alipita kuomba kura makanisani na maaskofu kumpigia kampeni ni UKWELI? Kama ni kweli wanajamii tungependa ushahidi wa kina ili tuamini hayo madai. Nyaraka zina kurasa. Ni kuras gani na waraka upi unaosema Dr. Slaa apigiwe kura za urais?
 
Nakumbuka wiki miezi miwili kuelekea uchaguzi 2010,ilikuwa ni mwanzoni mwa mwezi september jk alialikwa baraza la idd.ni wazi kuwa hotuba yake haikuwafurahisha waislamu hasa akijibu swala la MOU,alisema kwani waislamu wamekatazwa nao kuomba,kama wanaproject zinakidhi waombe watapewa.
Akijibu swala la mahakama ya kadhi alisema serikali haijawazuia kuanzisha mahakama hizo wao wenyewe.
Pia alitumia mda huo kukemea suala la wanasiasa kuingiza siasa kwenye dini etc .
Waislamu wengi tu hawakupenda,kwa ujumla licha ya uchaguzi kuwa wiki chache mbele lakini jk hakutaka kuegemea kwa muslim ili wampe kura.sasa huyu silaa atwambie ni lini jk ghafla alianza kupita misikitini akiomba kura?.
Wiki chache kuelekea uchaguzi rais alikua kila anapoenda akiwaasa watu wasikubali kuingiza udini katika campagn kwani suala hilo linaweza hatarisha amani.kina slaa na media zao walikua busy kukanusha kwamba hakuna udini.
Leo bila aibu wanageuka na kusema eti jk alitumia udini.
Kwanini hakuyasema kipindi kile?
 
Nimeisoma thread yako mleta hoja vizuri. Baada ya hapo nimeisoma habari yenyewe katika gazeti la TANZANIA DAIMA. Mwisho imebidi niagize gazeti lenyewe halisi na kisha kuisoma tena habari hiyo

Mimi nimegundua kitu kimoja kwamba sehemu kubwa ya watu kwa sasa hasa wale ambao wana forum ya kusemea hisia zao iwe ni mbunge Bungeni, sisi katika mitandao ya kijamii,wana media zote iwe ni radio,gazeti nk...iwe kwa kuandika au kusema wana tatizo moja kubwa.

Nalo ni kuwa kila mtu ameamua kuchukua mtu au upande wa kuutetea kwa gharama yeyote bila kujali anachokitetea au kukisemea, muhimu kwake yeye ni kuwa anamtetea mtu wake,wa upande wake,wa maslahi yake!!....Na kwa style hii ya uchambuzi wa mambo kamwe hatutaweza kupata mwafaka na suluhu ya matatizo yanayoikabili jamii yetu!!.

Lililo baya zaidi ni kuwa, haitawasaidia wale wenye mamlaka katika taifa letu katika kuamua hatua njema za kuchukua ili kurekebisha kasoro za kuinusuru jamii na matatizo kama haya ya udini, umaskini,rushwa na ufisadi,kuporomoka kwa elimu na maadili yetu kama taifa nk,nk.

Nikirudi kwenye mada na kwa maoni yangu ni kuwa Dr SLAA na KIKWETE ni watu wawili tofauti kwa nafasi zao katika jamii.Dr SLAA ni raia tu na ni kiongozi wa taasisi(chama cha kisiasa kinachoitwa CHADEMA) ambacho kwa namna yoyote hakina maamuzi juu ni nini kifanyike katika nchi.Huyu kwa nafasi yake kama ilivyo kwa mimi na wewe ni mtu wa kutoa maoni,ushauri na pia kukemea na kuwakosoa wale wenye mamlaka na uongozi wa nchi hii ili mradi hatuvunji sheria na taratibu za nchi yetu.

Kwa upande mwingine Kikwete si tu kwamba naye ni raia wa kawaida wa nchi hii lakini pia huyu ni mtu mwenye mamlaka ya juu kabisa ya katika nchi yetu....RAIS WA JMT. Anabeba tumaini na hofu ya kila mmoja wetu!!..Huyu ni mtu ambaye chochote kikitokea katika nchi anayepaswa kuwajibika ni yeye. Ndiye mtu ambaye ana kauli au uamuzi wa mwisho juu ya jambo lolote linalotokea au litakalotokea katika nchi yetu.Huyu ndiye kichwa na taswira ya Tz. Haya yote haondoi ukweli mmoja kuwa huyu ni binadamu ana STRENGTH na WEAKNESS....,so ni lazima akosolewe na anapofanya vyema ni hima apongezwe

Tatizo hapa ni kuwa Katajwa KIKWETE baaaasi!!. Kwa kuwa yeye ni mfalme kanuni ni ileile kuwa kamwe ukimwona mfalme yu uchi hakuna anayepaswa kusema Ee mfalme angalia u uchi!.....So, maneno yote haya ni kujaribu kuficha uchi wa mfalme.......BUT THE TRUTH IS THERE TO REMAIN kwamba mfalme yu uchi

Kwa maelezo haya naweza sasa kusema kwa ujasiri kabisa kuwa sioni kosa la Dr Wilbroad P. Slaa kwa kile alishokisema na kunukuliwa na gazeti la Tanzania Daima. Hayo ni maoni yake na ndicho anachokiona na ni jukumu la anayekosolewa kujitazama na kuona alipokosea. Pia sioni tatizo kwa wale wanaoweza kusema kuwa Dr Slaa naye ni mdini so long as wanaweza kuthibitisha tuhuma zao. Tatizo ninaloliona mimi ni sisi tunaowatazama watu hawa.Tunawatazama na kuwasema kwa mtazamo wa dini zao.Hatuwatazami na kuwasema kwa kuangalia makosa yao wao kama wao.Kwa hiyo tatizo la UDINI tunalikuza sisi wenyewe tukidhani tunatetea maslahi yetu na ya wale tunaowatetea!!.

Mwisho waasisi wa mitafaruku ya kidini na udini inasemwa ni KIKWETE na CCM kwa ujumla. Ukimwondoa Dr W. P. Slaa, pia yalisemwa kwa uwazi bila chenga ndani ya Bunge na Ndugu Godbless Lema(MB) na kwa sababu humo ni lazima uongee jambo ambalo ni kweli...GODBLESS LEMA aliombwa kuthibitisha ni kwa vipi CCM na KIKWETE ni waasisi wa mitafaruku ya KIDINI na UDINI kwa kupeleka ushahidi thabiti Bungeni......akapewa siku saba. Ni bora CCM na sisi sote tukamwomba spika wa Bunge letu amalize jambo hili mara moja na wote tukubali kuupokea ukweli.....na kama hawa Lema aliyetoa hoja hii hataweza kuthibitisha hili na sisi sote wote tukaridhika kabisa kuwa hana ushahidi,basi huo ndo wakati mwafaka wa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya LEMA ambaye kwa namna yeyoye ndiyo hoja Dr Slaa na ndiyo hoja ya CHADEMA.....Na Spika akinyamazia hili akaliacha likapita basi huo ndio ukweli na Kikwete na CCM yake tutawalazimisha wawajibike maana hawa ndo watakuwa chanzo cha vurugu!!...
 
Ukisoma na Ukataka Kumuelewa Dr slaa juu ya Swala la Udini, Utamuelewa kwa mapana sana Kwani Kaeleza Ukweli Mtu juu ya JK na Washiriki wake.
Leo Nimesikia Majibu ya Ikulu juu ya Kauli ya Rais wa Mioyo ya Watanzania.Katika majibu hayo Sikutegemea Ikulu kugeuka kuwa Makapeni meneja Wa jk 2010 Wakati walikuwa hawapo kipindi hicho ni ukweli upya wanaujua kuhusu jambo hili?Ukitafakari majibu yao Utagundua Udhaifu wao.

Kiukweli Msumari aliyopigilia Dr Slaa ni Msumari wa Moto kwa JK na Washiriki wake. Hakuna atakayeweza Kuuchomoa Msumari huwo japokuwa unauma ila Hawanabudi kuuvumilia na kutafuta majibu badala ya Blah Blah zao Wakati wameliteketeza Taifa Kwa Ulafi wa Madaraka.

Vile Vilw swala hili Mhe.G Lema alilizungumza Bungeni kwa Mapana sana Watanzania wote Tulisikia na Tukamuelewa, Hebu Spika wa Bunge Wampe Lema Nafasi ya Kuwasilisha Ushahidi wake Mbele ya Bunge na siyo uchochoroni kama Ambavyo walikalia Ushahidi wake juu ya Uongo wa Pinda. Tukipata Ushahidi wa Lema sasa Ikulu itakuja kuthibitisha kama ilivyokurupuka Leo na Majibu yao Mepesi kwenye Maswali tata.

Ni hayo tu kwasasa.
 
Usiongee maneno usiyokuwa na uhakika nayo ndugu, uchaguzi wa 2010 makanisa yalizuia waumini kufanya kampeni za aina yoyote katika maeneo yanayozunguka kanisa ila kwa upande wa pili hali ilikuwa tofauti. kauli zako ni zi zakichochezi waziwazi tafuta point nyingine ya kumuusisha Dr. Slaa na udini lakini si kucompare na uchaguzi wa 2010 kwamba kanisani zilifanywa kampeni za kumweka Dr. Slaa madarakani. Huo ni uongo na unapaswa kumuogopa Mungu wako na si kukurupuka pasipo kuwa na hoja za msingi.
 
Tumeshawajua humu wafuasi wa sheikh Ponda na Ilunga. Mlichokitaka mmekipata. Mnafanya dhambi halafu mnamyooshea kidole asiyehusika ionekane ana hatia ili nafsi zenu zifurahi. Na hii ndiyo asili ya udini ulioasisiwa na JK na CCM. Damu inayomwagika, mtkuwa na la kujibu mbele za Mungu.
 
Kwanza hakuna ubishi kwamba Dk Slaa ni mdini kama alivyo mtu mwingine kwa sababu amewahi kutumikia dini kwa ahadi kabla hajaamua kusaliti na kurudi uraiani nadhani kwa lengo la kuwatumikisha.

Pili, hakuna ubishi kwamba gazeti la Tanzania daima ni kampeni meneja wa CHADEMA na tatu hakuma ubishi kwamba kuna wimbi kubwa la masuala ya udini.

Ushauri wangu:
Kama kweli hawa viongozi wanataka kututawala na kuongoza nchi hii waache huu ujinga wa kupandikiza udini miongoni mwa watanzania.
Ukiwa unafanya kazi ya kilimo unaitwa mkulima ukiwa mvua samaki unaitwa mvuvia, ukina na dini ni lazima uwe mdini. Je ni nani kati yetu asiye mdini?
 
Ukweli uko wazi kwa Tz nani ni muasisi wa Udini nchini na laana iko juu yao
 
..strategy anayotumia Dr.Slaa kumshambulia JK kwenye udini sasa hivi wala haina mashiko.....maana maji yameshamwagika...Btw JK wala 2015 hatagombea urais....kwa hiyo kumshambulia JK wala kunaweza kusilipe kwa chadema....Mi nadhani Chadema watafte strategy ambazo zitawabana ccm kwa ujumla wao....mfano issue za wizi wa fedha za umma...na wizi wa madini yetu....na mikataba mibovu ya serikali hii....na hali duni za maisha ya watanzania huko vijijini...

Hili la udini tayari linajulikana kinara wake (ccm na viongozi wake kwa ujumla wao wako responsible)..na kulipiga kelele ni kuongeza pilipili kwenye kidonda...

Dr.Slaa afanye kazi ya kuwafungua macho huko vijijini....kwa kuwapa ukweli wa chanzo cha umaskini wao(ccm).....haya ya udini ni kuzidi kuwagawa watu....ni maoni yangu tu.......
 
Duh,kuna watu wanapenda vibaya hadi wamekuwa vipofu.
 
WEWE NI MZALENDO KWA UDINI HUU? TANZANIA DAIMA UNAOWATUHUMU KUWA NI WABAYA, mbona wewe umeleta utumbo uleule?

Hii ni safu ya wachangiaji haya ona sasa wachangiaji wanakuja kwa misingi ya dini!!!!........

Hoja zenu hizi si za kisiasa ni za dini.
bora umeliona hilo big up
 
Miongoni mwa maneno ya watu wa zamani wenye hekima ambao kwa jina moja huitwa wahenga, waliwahi kusema kuwa Uzee nyumba ya Magonjwa, wakimaanisha kuwa na umri mkubwa yaani Uzee ni kuwa karibu mno na magonjwa ya aina mbalimbali. Moja ya magonjwa ambayo uzee humsababishia yule aliyezeeka ni pamoja na ugonjwa wa kupungua kwa akili, yaani mtu kutowaza sawasawa, kuwaza pungufu ama kutowaza kabisa.

Miongoni mwa jamii yetu tunao wazee.,wazee hawa wamegawanyika katika makundi mbalimbali na pia walikuwa watu wa aina tofauti waliopitia na wenye uzoefu wa kada mbalimbali za kiutendaji. Ingawa kauli nyingine inayowataja wazee inawataja kuwa ni nyumba ya hekima kwa maana kuwa umri mkubwa unanasibishwa na uzoefu na kujua mambo mengi ambayo hawa wazee huwa wameyapitia katika maisha yao.

Jina lingine ambalo mtu akizeeka anaitwa kutokana na umri wake ni BABU.,mimi ninao mababu na nawajua mababu wengine wengi, ila yupo babu mmoja ambae pamoja na Uzee wake na kuchoka bado anatamani kuyafanya yale ambayo babu hapaswi kuyafanya, anayasema yale ambayo yanatoa tafsri tofauti na yanapingana na falsafa ya weledi na hekima ambazo mtu mzima mwenye umri mkubwa yaani babu anastahili kuwa nao.

Naomba nimtambulishe Babu huyu ninayemfahamu, ambae ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Chama cha Siasa Cha Upinzani. Babu huyu anazeeka vibaya sana.,na niliwahi kulisema hili hapo nyuma kuwa mtu mzima huyu amekuwa wa hovyo sasa na kauli yangu hiyo imeendelea kuthibitishwa na maneno na matendo ya Babu huyu.

Hivi karibuni Babu ametoa kauli si tu ya kupotoka bali yenye ziada ya Uongo Mkuu, ya fitina na uchonganishi, yenye kulenga kushawishi chuki, hasira, hasadi na utengano ndani ya jamii yetu ya kitanzania. Kauli ya Dr Slaa kuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Mwenyekiti wa Chama Makini Chenye kuongoza Dola CCM Ndugu Jakaya mrisho Kikwete ni muasisi wa Udini hapa nchini, ni kauli mbaya kuwahi kutolewa na KIONGOZI hasa wa kisiasa hapa nchini.

Kauli hii si tu ya uongo,bali pia haikupaswa kutolewa na kiongozi mwenye umri wa Slaa katika wakati huu ambao nchi imekaa pamoja kujenga umoja na mshikamano baina ya watu wa dini mbalimbali. Aidha, Kauli hii ni mfululizo wa kauli nyingine za uchochezi na zenye kuhamasisha chuki za kidini hapa nchini.

Kauli hii ni ya mtu asiyeweza kufikiri sawasawa ama mjinga asiyeelewa athari za kauli hiyo, ni ushahidi wa kukosa weledi wa kisiasa, hekima na zaidi ni kukosa Uzalendo na Utaifa. Ni mtu asiyelipenda taifa lake tu ndio ataishabikia kauli hiyo na kuipongeza lakini yeyote mwenye kufikiri sawasawa ameshtushwa na ataalaani vikali kauli hiyo na zingine mfano wa hiyo zenye kuhatarisha AMANI ya nchi hii.

Nisingelienda mbali zaidi na kufikiri juu ya Uzee na kufahamu kwangu kuwa Uzee unasababisha Ugonjwa na hasa wa Akili basi ningeliishauri dola kumchukulia hatua kali za kinidhamu mzee huyu. Bali naelewa kuwa Babu anazeeka vibaya, uzee wake unamjia vibaya sana. Kama ameyasema hayo kwa minajili ya kujiletea umaarufu wa Kisiasa katika kipindi kama hiki ambacho makanisa yanalipuliwa, misikiti inachomwa moto, masheikh na maaskofu wanajeruhiwa na kuuawa, basi nadiriki kusema ni siasa mbaya sana kuwahi kufanywa hapa nchini, na kama maneno hayo yatahalalishwa katika jamii kwa kuwa tu yametolewa na mwanasiasa na kubebwa kisiasa basi sasa siasa hii inaelekea kutuangamiza.

Babu hana sifa achilia mbali ya kuongoza nchi bali hata kuongoza taasisi yenye hadhi ya chama cha siasa, ni mtu wa hovyo, asiyejitambua, ni mtu ambae anaweza kusema ama kufanya lolote popote bila kujali chochote.

Kiongozi wa watu kamwe hawezi kutoa kauli kama hizi zenye kuharibu murua hata wa mzungumzaji mwenyewe. Ni kauli za kimbayuwayu zenye kujaa upotoshaji. Ni UCHOCHEZI ulio dhahiri, hii ni kauli nyingine iliyozifuata zile za awali kama "..NCHI HAITATAWALIKA.." na "..DAMU ITAMWAGIKA.."

Ni wazi akili ya Babu imechoka,ni vema tukawa washauri bora kwake kumshauri Babu kupumzika Siasa. Ni wakati wa kusataafu na kuwapisha vijana wafanye siasa. Mimi binafsi naamini Chadema inao vijana wanaofikiri, tena wasomi wazuri wanaoweza kuleta chachu na changamoto ya kuleta mwelekeo na taswira inayokubalika ya Chama hicho na viongozi wake ndani ya Jamii yetu.
 
Dr Slaa anaweweseka kwani hajui hatma yake ndani ya chadema
 
Alisema nchi haitatawalika kwa sababu alijua uongozi unaoingia madarakani ni dhaifu.
 
maneno ambayo ametamka dr slaa hayakustahili kutoka kinywani mwake, mtu ambaye anaota kuingia ikulu ingawa umri ndo umeshamtupa mkono. mbaya zaidi alikuwa padre ambapo wakati wa mafundisho aliambiwa kuwa kusema uongo ni dhambi
 
we ongea tu dr akiwa rais hatakung'oa jino wala kucha bali atakupa elimu ya kujitambua poleni sana.
 
As a Christian I have no duty to allow myself to be cheated, but I have the duty to be a fighter for truth and justice.

******************************************
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom