Kwa hili Arfi na Shibuda mmechemsha

Kwa hili Arfi na Shibuda mmechemsha

Centrehalf

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2013
Posts
509
Reaction score
145
Amani kwa wote,ni nimeshangazwa sana na kauli zinazotolewa na Arfi pamoja na shibuda kama utetezi wao juu ya ushiriki wao kwenye Bunge Maalum la katiba.

Nikianza na Arfi yeye anasema anaenda kuwakilisha wapiga kura wake maana yeye ni mbunge,kauli ambayo haitofautiani na ya Shibuda anaedai kuwa anaenda kuwakilisha wakulima wa pamba na wafugaji wa maswa kama mbunge wao.

Maswali ninalo jiuliza juu ya kauli za hawa watu ni

1.je ni lini hawa watu wamewahi kusanya maoni ya wapiga kura wao majimboni juu ya uandikaji wa katiba mpya?maana kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba aliyepewa mamlaka ya kukusanya maoni nchi nzima ni tume ya Rais iliyoongozwa na Mh Warioba tu, na wala hakuna chombo kingine kilicho ruhusiwa kisheria na kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba ni maoni yaliyokusanywa na hiyo tume ndiyo yanayotambulika kuwa rasmi kisheria.

2. Ni lini Arfi na Shibuda walichaguliwa na wananchi kwenda kuwawakilisha kwenye bunge maalum la katiba?maana kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba hakuna mbunge wa Bunge Maalum la katiba aliyeingia pale kwa kuchaguliwa wote wameteuliwa na Rais.

Rais pekee ndiye aliyepewa maamlaka ya kuteua wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba hakuna mahala sheria ilipo wahusisha wananchi kuchagua wawakilishi wao ndani ya hilo bunge.

Hao mnaosema mnawawakilisha waliwatuma lini na kwa kutumia utaratibu gani?kusema ule ukweli kwa hili mumechemsha wala hamna hoja ya kujitetea bora mungeweka wazi ni nani mnaemtumikia ieleweke kuliko kusingizia wananchi.ni suala lilowazi kuwa nyie ni vibaraka wa CCM ndio maana Arfi wamekutenga usijihusishe na mambo ya kambi rasmi ya upinzani na leo umelithibtisha kwa kufanya hadharani ulichokuwa una kataa kumbuka duniani hamna siri ndio maana utakuta hata mchawi anayefanya mambo kwa kificho tena gizani kuna siku anakamatwa mchana kweupe .

Shibuda ni mmoja wa vibaraka wa CCM ndani ya upinzani kama unakumbuka Shibuda umewahi tajwa kuhusika kwenye mpango wa kukihusisha CHADEMA na ugaidi.

Umewahi tajwa kwamba ulikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wanawashawishi vijana wawataje Mbowe na Slaa kuwa wanafadhili ugaidi kwa ahadi ya vijana kupewa pesa na vyeo, leo imedhihirika mchana kweupe nafuu ya Zitto yeye kwa unafiki mkubwa amejitenga nanyi japo lenu ni moja.ana maana yake kwa kuwa ana malengo fulani ndio maana ameweza hata kutamka wazi kuwa UKAWA wako sahihi je yeye kwa kutoingia bungeni hana wapiga kura munge kaa nae mumuulize kuliko kujichomeka.

Maana Shibuda mimi ninge kuelewa iwapo tu ungerudisha kadi ya CHADEMA na kuwaandikia barua ya kujivua uanachama hiyo ingekujengea heshima kubwa kwa mtu kjivua ubunge kupinga uonevu au mwenendo wa CHADEMA.

Unatangaza kujitoa CHADEMA kwa mdomo tu mbona taratibu za kujivua uanachama hujazitekeleza?kama sio usanii huo.

Mh Fred Mpendazoe alipo kiponda na kukipinga CCM aliandika barua ya kujivua uanachama na kurudisha kadi yao akawa amepoteza na ubunge wake ilikutimiza kauli yake na dhamira yake yakutetea wanyonge.

Arfi na Shibuda mmechemsha maelezo yenu hayana mashiko masikioni mwa watanzania.

Nawasilisha
 
posho posho posho posho posho posho posho, chezea laki tatu chezea laki tatu kila siku weweeeee
 
Yangu macho,namkumbuka na kuwafananisha jamaa hawa na Dan'hi Makanga ambaye sasa ni mkuu wa wilaya moja huko mkoani Kigoma.Huyu alikuwa na tambo na matusi zaidi yao akiwa UDP akimtukana Mwkt wake akidai alipata ubunge kwa umaarufu wake,leo yupo wapi?
 
Nimeamini hakuna adhabu mbaya kama kupuuzwa mkuu. Hayo yote wanayoyafanya ni mahangaiko ya psychological torture ya kupuuzwa. Wamekuwa kama vile mwanamke aliyefumaniwa na mumewe halafu mumewe hasemi kitu bali anatabasamu tu. Wanachofanya sasa ni kutaka angalau uongozi wa CHADEMA uwakalipie, na wanaumia sana wanapoona jamaa wanawaangalia tu.
 
Nakumbuka Shibuda kuondolewa uongozi km mkt wa muda wa mkoa wa Shy ndani ya wiki moja baada ya kugundulika kuhusika na kufanya njama za kifo cha aliyekuwa mshindi wa ubunge Shy mjini(CDM_2010) ambaye aliibiwa kura na Steven Masele mshindi wa kura 1.
 
Amani kwa wote,ni meshangazwa sana na kauli zinazotolewa na arfi pamoja na shibuda kama utetezi wao juu ya ushiriki wao kwenye bunge maalum la katiba.ni kianza na arfi yeye anasema anaenda kuwakilisha wapiga kura wake maana yeye ni mbunge,kauli ambayo haitofautiani na ya shibuda anaedai kuwa anaenda kuwakilisha wakulima wa pamba na wafugaji wa maswa kama mbunge wao.maswali ninalo jiuliza juu ya kauli za hawa watu ni 1.je ni lini hawa watu wamewahi kusanya maoni ya wapiga kura wao majimboni juu ya uandikaji wa katiba mpya?maana kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba aliyepewa mamlaka ya kukusanya maoni nchi nzima ni tume ya rais iliyoongozwa na mh warioba tu.na wala hakuna chombo kingine kilicho ruhusiwa kisheria na kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba ni maoni yaliyokusanywa na hiyo tume ndiyo yanayotambulika kuwa rasmi kisheria.
2.ni lini arfi na shibuda walichaguliwa na wananchi kwenda kuwawakilisha kwenye bunge maalum la katiba?maana kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba hakuna mbunge wa bunge maalum la katiba aliyeingia pale kwa kuchaguliwa wote wameteuliwa na rais.ni rais pekee ndiye aliyepewa maamlaka ya kuteua wa jumbe wa bunge maalum la katiba hakuna mahala sheria ilipo wahusisha wananchi kuchagua wawakilishi wao ndani ya hilo bunge.hao mnaosema mnawawakilisha waliwatuma lini na kwa kutumia utaratibu gani?kusema ule ukweli kwa hili mumechemsha wala hamna hoja ya kujitetea bora mungeweka wazi ni nani mnaemtumikia ieleweke kuliko kusingizia wananchi.ni suala lilowazi kuwa nyie ni vibaraka wa ccm ndio maana arfi wamekutenga usijihusishe na mambo ya kambi rasmi ya upinzani na leo umelithibtisha kwa kufanya hadharani ulichokuwa una kataa kumbuka duniani hamna siri ndio maana utakuta hata mchawi anayefanya mambo kwa kificho tena gizani kuna siku anakamatwa mchana kweupe .nae shibuda ni mmoja wa vibaraka wa ccm ndani ya upinzani kama unakumbuka shibuda umewahi tajwa kuhusika kwenye mpango wa kukihusisha chadema na ugaidi.umewahi tajwa kwamba ulikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wanawashawishi vijana wawataje mbowe na slaa kuwa wanafadhili ugaidi kwa ahadi ya vijana kupewa pesa na vyeo.leo imedhihirika mchana kweupe nafuu ya zitto yeye kwa unafiki mkubwa amejitenga nanyi japo lenu ni moja.ana maana yake kwa kuwa ana malengo fulani ndio maana ameweza hata kutamka wazi kuwa UKAWA wako shihi je yeye kwa kutoingia bungeni hana wapiga kura munge kaa nae mumuulize kuliko kujichomeka.maana shibuda mimi ninge kuelewa iwapo tu ungerudisha kadi ya chadema na kuwaandikia barua ya kujivua uanachama hiyo ingekujengea heshima kubwa kwa mtu kjivua ubunge kupinga uonevu au mwenendo wa chadema.wewe unatangaza kujitoa chadema kwa mdomo tu mbona taratibu za kujivua uanachama hujazitekeleza?kama sio usanii huo.mh fred mpendazoe alipo kiponda na kukipinga chama cha ccm aliandika barua ya kujivua uanachama na kurudisha kadi yao akawa amepoteza na ubunge wake ilikutimiza kauli yake na dhamira yake yakutetea wanyonge.kwa hili arfi na shibuda mumechemsha maelezo yenu hayana mashiko masikioni mwa watanzania.nawasilisha

huyo shibuda hana maana hata raia wake anaosema wameshamchoka .
 
Hawa watu walishatoks CDM siku nyingi wamo wamo kumalizia ubunge wao.
Hakuna sababu ya kuhangaika nao.
 
nimependa ulivyoweka wazi uwepo wa uwakilishi wa wananchi kwenye bunge hili la katiba.
Ni dhahiri shibuda na Arif wamjichanganya kwenye mtego hatari kisiasa (they have choose a bad card).
hata matamko yao wanayatoa kwa hoja shallow na kwa unyonge mkubwa kwasababu wameshajua matokeo ya hili wanalolifanya.
 
kwa kweli nimeshindwa kusoma, ila nilitamani nijue ulichoandika.
 
Shibuda sawa, ila bado siamini kama Mzee Arfi kweli kaingizwa mkenge na vijana wadogo akina MM!!
 
Yangu macho,namkumbuka na kuwafananisha jamaa hawa na Dan'hi Makanga ambaye sasa ni mkuu wa wilaya moja huko mkoani Kigoma.Huyu alikuwa na tambo na matusi zaidi yao akiwa UDP akimtukana Mwkt wake akidai alipata ubunge kwa umaarufu wake,leo yupo wapi?

zidumu fikri za mwenyekiti dj
 
wanazeeka vibaya na misongo ya kukataliwa na wananchi,ajabu wanasema wanawakilisha wapiga kura wakati huo wananchi washawatupilia mbali sasa sijuhi wanamdanganya nani
 
Back
Top Bottom