Kwa heshima na taadhima sisi Wastaafu tunaolipwa na LAPF pamoja na HAZINA hatujalipwa pensheni zetu za mwezi Julai 2019 na HAZINA. Maisha ni magumu sana huku mitaani na pensheni ndiyo tegemeo letu kwa sasa ukichukulia umri wetu na magonjwa yanayotunyemelea kwa sababu ya uzee. Tulipeni haki zetu.