Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndg zangu wanaJF,
Kwa nini Chadema na Dr. Slaa (PhD) wao wanaonekana kuwa ni wadini lakini Mch. Mtikila ambaye jina lake halitajwi bila cheo cha Mch. lakini sijawahi kusikia Mzee Mtikila akilaumiwa hata mara moja kwamba ni mdini. Tena basi wakati mwingine Mch. Mtikila amekuwa akiirejea waziwazi Biblia Takatifu katika kujenga hoja zake mbele ya vyombo mbalimbali vya habari lakini hajawahi kulaumiwa kuwa ni mdini.
My take:
Dr. Slaa (PhD) anaonekana kuwa ni tishio kwa sisiem na mafisadi wake. Wameshindwa kupunguza kasi yake kwa kutumia nguvu ya hoja. Wamejaribu kutumia maisha yake binafsi ya ndoa, wameshindwa. Mwishowe, wamekimbilia kwenye UDINI kama silaha yao ya msaada. Sasa bahati mbaya silaha hiyo ni ya maangamizi. Badala ya kumwangamiza Dr. Slaa (PhD) na chadema yake, watakaoangamia ni jamii nzima ya Tanzania. Ukweli wa hoja hii umeanza kujionyesha MTO WA MBU. Watanzania tuipuuze na kuifutilia mbali sisiem. Ni chama kilichopauka. Kimeishiwa hoja. Tukiendelea kukiacha madarakani, taifa litaangamia. Mwenye macho na masikio asipuuze wito huu.
Kwa nini Chadema na Dr. Slaa (PhD) wao wanaonekana kuwa ni wadini lakini Mch. Mtikila ambaye jina lake halitajwi bila cheo cha Mch. lakini sijawahi kusikia Mzee Mtikila akilaumiwa hata mara moja kwamba ni mdini. Tena basi wakati mwingine Mch. Mtikila amekuwa akiirejea waziwazi Biblia Takatifu katika kujenga hoja zake mbele ya vyombo mbalimbali vya habari lakini hajawahi kulaumiwa kuwa ni mdini.
My take:
Dr. Slaa (PhD) anaonekana kuwa ni tishio kwa sisiem na mafisadi wake. Wameshindwa kupunguza kasi yake kwa kutumia nguvu ya hoja. Wamejaribu kutumia maisha yake binafsi ya ndoa, wameshindwa. Mwishowe, wamekimbilia kwenye UDINI kama silaha yao ya msaada. Sasa bahati mbaya silaha hiyo ni ya maangamizi. Badala ya kumwangamiza Dr. Slaa (PhD) na chadema yake, watakaoangamia ni jamii nzima ya Tanzania. Ukweli wa hoja hii umeanza kujionyesha MTO WA MBU. Watanzania tuipuuze na kuifutilia mbali sisiem. Ni chama kilichopauka. Kimeishiwa hoja. Tukiendelea kukiacha madarakani, taifa litaangamia. Mwenye macho na masikio asipuuze wito huu.