Kwa Aston Villa hii Samatta atarudishwa kundini?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,305
12,600
Aston Villa aliyoiacha Mbwana sio kama ya sasa baada ya yeye kuondoka kwenda Uturuki kwa mkopo. Je, kuna uwezekano kiasi gani kwa Samatta kurudi tena Aston Villa kama mchezaji?
 
Kuna kitu hakikuwa sawa hata kabla ya Samatta kujiunga Aston,kaikuta kwenye ventilator ila alipotoka tu ndo ufumbuzi ukapatikana.
Usajili wa dirisha dogo ni wa kimkakati zaidi, ni kama drip la maji kwenye mwili wa mgonjwa. Baada ya mgonjwa kuwekewa drip ndugu wanategemea mgonjwa wao atabadilika kuelekea kupona. Lakini Samatta hakufanya kazi chanya ya drip kwenye timu. Timu ilikuwa afadhali ya jana.
 
Samata umri unamtupa, ndio maana hata huku alipo kwa mkopo kila mara anakuwa majeruhi. Arudi bongo achezee Yanga kwa mkopo kabla ya kustaafu rasmi.
 
Ile Aston ilikuwa mbovu bwana kwanzia kwa kipa

Wameasajiri wachezaji kama nane ndo unaona imekuwa hivyo

Otherwise ingeshuka daraja
 
Yule alishauzwa kwa lugha danganyishi ya kutolewa mkopo...

We ushaona wapi mtu anatolewa mkopo kwa miaka mitatu
 
Back
Top Bottom