Kuzuia msafara wa Rais ni uhaini!

Kuzuia msafara wa Rais ni uhaini!

Siamini pia kama wananchi wanaweza kusimamisha msafara Wa rais hasa Wa aina kama huyu tuliyenae,
ila kuhusu wananchi kuwa wengi inatokana na kule mkoani watu humuona rais kipindi cha kampeni labda itokee kuna tukio maalum kama ufunguzi wa bomba kama hili tofauti na dar au Dodoma ambao humuona kila mala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi habari za kusema wananchi wamezuia msafara wa Rais kumuelezea shida zao nadhani ifike mahala sasa tuseme ukweli!!!
Hakuna anayezuia msafara wa Rais,kama ushaona speed ya gari za kwenye msafara,utakubaliana na mimi kuwa hakuna mwananchi wa kawaida anayeweza kufanikiwa kuzuia msafara!

Turudi nyuma kabla ya kuzuia,unawaandaa watu kwenda kumpokea Rais halafu unasema wamezuia msafara!Mnafunga masoko na na kuwalazimisha walimu na watumishi wa serikali kwenda kujipanga barabarani halafu mnasema wamezuia msafara!!!!!

Hebu wananchi wajipange kimya kimya halafu wajue kuna msafara wa Rais,waende kuuzuia waone kitakachowakuta!

Hizi kiki ifike mahali media nazo ziache kutoa promo zisizo na kichwa wala miguu!

Kuna taarifa kuwa huko Tanga kesho soko litafungwa ili watu waende kwenye mkutano!Watumishi wataandikishwa hadi majina na ole wao wasioukuwepo!!!!
Kiki unaita uhaini?
Kipimo cha mkojo kina kuhusu.....!!!

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Ila lowassa alikua anasimamishwa na wananchi hamkusema kiki......Bali mlisema anakubalika zaidi ndomana wamemsimamisha rais wao wa mioyo yao...Leo kwa JPM mnasema kiki vipi jamani!?
 
Tuache siasa za kitoto.
Hakuna mwananchi anayeweza kusimamisha msafara wa rais
Hivi mnasahau speed ya gari za msafara wa rais??

sent from Sokoro nkorambokande
Spidi ya msafara Wa Lowassa upoje vileee
 
Ila lowassa alikua anasimamishwa na wananchi hamkusema kiki......Bali mlisema anakubalika zaidi ndomana wamemsimamisha rais wao wa mioyo yao...Leo kwa JPM mnasema kiki vipi jamani!?
Huyu ni Rais wa JMT!Hebu jaribu mfanye kumsimamisha kimya kimya kama hamjalambwa shaba!
Kiki tu hizo!
Hata kukamata vichwa vya treni ambavyo mmiliki wake hajulikani ni kiki
 
Bora hii ya kusimamisha msafara wa rais inaweza kuingia akilini kidogo KULIKO ule usanii wa kupiga deki barabara eti fisadi apite, khaa!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wajinga tu wanaweza kuamini kwamba unaweza kuzuia msafara wa Raisi!!
 
Tuache siasa za kitoto.
Hakuna mwananchi anayeweza kusimamisha msafara wa rais
Hivi mnasahau speed ya gari za msafara wa rais??

sent from Sokoro nkorambokande
Mleta nada ni bavicha hajui maana ya uhaini anataka kuhalalisha ujinga wao kwa kuchochea kuwa wananchi wanapotaka kuongea na rais ni uhaini. Lowassa akisimamishwa wanasema waache watu waongee na rais wa mioyo yao. Wananchi tukimsimamisha tuongee na rais wa nchi wanapagawa eti uhaini.
 
Back
Top Bottom