Kuzaliana kunamsaidia nini kiumbe anayezaa?

Kutokuzaa ni sawa na kukana your own existence, kwan wewe uliungwa garage ndugu , kama umezaliwa na wewe zaa utakua umelipa deni.
 
Kuzaa ni kulipa deni lako la kuzaliwa, unapozaliwa unatakiwa uzae ili kizazi kiendelee kuwepo. Hilo wazo lako ni zuri sana ukiwa katikati ya upumbavu, lakini ni swali baya ukiwa timamu kweli, jiulize kile kizazi kilichotoka kwenye safina kingejiuliza hivi we ungeulizia wapi??
Maana yake ni kwamba asingekwepo na kwani kutokuwepo kwake duniani, angepata hasara gani.


Yesu ni Kristo!
 
Arabi ni kwamba wenye uwezo mkubwa kiuchumi hawana utitiri wa Watoto....!!
Kikawaida mke wa tajiri akipata mimba possibility ya kuharibika mimba ni kubwa sawa na ya kuzaa 50/50 lakini masikini akishika mimba kuzaa ni 90 % kuharibika ni 01% kutoa 09% ndipo uelewe Tajiri na Mali zake masikini na watoto wake.
 
kwani ukizaa ndio maisha yako hayakomi ,uzae usizae lazima ufe na maisha yako ndio yamekoma hapo
Kwa sisi viumbe tulio hai tunazaana ili maisha yaendelee na huo mwendelezo ndo faida kwetu sababu tumepata tunachokitaka, maisha yakikoma ni hasara kwetu sababu tumekosa tulichokitaka.

Kuhusu wanachopata waliokufa kwa kuendeleza maisha hakuna ajuaye kama wewe usivyojua utapata hasara gani usipozaliana pale utakapokufa.
 
Kuzaa kunafaida ya kujihisi raha tu unapowaona watoto wako na kuwafundisha fundisha vitu, BINADAMU WOte tunapenda tuonekane tunajua vitu na kutaka umpate mtu wa kumfundisha mambo, Sasa ule muda unamfundisha ndio raha Tena hasa akaelewa.
Hi ipo kwa kuku pia anapenda pia kufundisha vifaranga kuparua chakula,njia za mpambano nk
Pia uwafikirie wale ambao walizaa watoto wenye matatizo mbalimbali kwa mfano, seli mundu vilema vya mwili na akili, mashoga, nk nk ambao kila siku ni kupisha a kwenye korido za mahospitalini, na maziko kila mara, ...


Jesus is Savior
 
kwani ukizaa ndio maisha yako hayakomi ,uzae usizae lazima ufe na maisha yako ndio yamekoma hapo
Maisha si wewe pekeyako. Naongelea uwepo wa viumbe hai waitwao binadamu.

Kwani uwepo wako humu JF una maana gani kama hakuna binadamu waliozaliwa kama wewe kujadiliana nao?
 
Kuzaa ni kulipa deni lako la kuzaliwa, unapozaliwa unatakiwa uzae ili kizazi kiendelee kuwepo. Hilo wazo lako ni zuri sana ukiwa katikati ya upumbavu, lakini ni swali baya ukiwa timamu kweli, jiulize kile kizazi kilichotoka kwenye safina kingejiuliza hivi we ungeulizia wapi??
Unamlipa nani hilo deni wazazi wako au?
Wenyewe watapata faida gani wewe ukiwa na mtoto,binafsi naona hasara za kuwa na mtoto ni nyingi kuliko faida.
 
Sasa Duniani unakuwepo ili kulinda nini, Wakati siku moja utakufa tu?
Nikuulize: unataka kusiwe na kifo ndipo maisha yawe na maana?

Kwani Kutokuwepo kwa maisha duniani kuna faida gani? absence of life ina maslahi gani kwako? Ukiweza kunijibu hili swali la pili nitaelewa mantiki ya hoja zako.
 
But why kunakiwa na upendo kati ya mzazi na mtoto.?
Maswali ya why huwa hayana mwisho. Nasikia ndomana Mungu kajificha maana binadamu mngemchosha na why why wakati saa nyingine jibu ni Just because, For no reason, Coz I can
 
.... ungekuwa mwanaume usiye na uwezo wa kuzalisha au mwanamke usiye na uwezo wa kutunga mimba usingewaza haya, siku zote aliyeshiba hamfikirii mwenye njaa...kiafya binadamu anasaidiwa na kuzaa sababu moja ya kazi ya mifumo ya mwilini ni kutengeneza viini vya uzazi wa binadamu mwingine na zoezi zima uitimishwa na Sex kati ya mwanaume na mwanamke na ndiyo maana kutokuwa na uwezo wa kuzaa au kuzalisha ni tatizo la kiafya.!
Hatuzungumzii binadamu pekee. Ng'ombe, kuku nk
 
Mwili wa binadamu na viumbe wengine wote unahangaika sana na mambo mawili. Kusurvive na kuzaliana. Sasa najiuliza kuzaliana kunamsaidia nini kiumbe anayezaa. Kuendeleza kizazi cha ng'ombe, kunamsaidia nini ng'ombe anayezaa. Binadamu walioishi miaka ya BC huko, wanafaidika vipi na kuendeleza uzao wa binadamu? Kungekuwa hamna kufa ningeweza kidogo kuelewa.

Zaidi naona uzazi unamnyonya mzazi kiafya, kichumi nk. Kuzaliana kunamsaidia nini anayezaa?
Itakuwa hupendi kula wewe! Kama unapenda kula kaulize mimea kwanini inatoa mavuno na kisha yenyewe inachomwa kama mabua n.k

Shabash! Sasa si ufe ili usimyonye mzazi wako kiuchumi?
 
Mwili wa binadamu na viumbe wengine wote unahangaika sana na mambo mawili. Kusurvive na kuzaliana. Sasa najiuliza kuzaliana kunamsaidia nini kiumbe anayezaa. Kuendeleza kizazi cha ng'ombe, kunamsaidia nini ng'ombe anayezaa. Binadamu walioishi miaka ya BC huko, wanafaidika vipi na kuendeleza uzao wa binadamu? Kungekuwa hamna kufa ningeweza kidogo kuelewa.

Zaidi naona uzazi unamnyonya mzazi kiafya, kichumi nk. Kuzaliana kunamsaidia nini anayezaa?
Kiumbe anafaidi saaana mnoooooo, yaaani ni raha hadi mwisho.

Ukiachana na akili za kimaskini[kiuhitaji] na kiupungufu[scarcity] kuna kanuni za kiutoaji[utajiri] na utele[abundance].

Kiufupi hata unavyoona mtu anatafuta mali kwa bidii zote jua kindani yake kabisa ni ile tamaa ya kutoa/kujitoa kwa kiasi kikubwa inayomuongoza. Akiishia kuwapa mali watoto wake atapata furaha ya kakiwango fulani, lakini akiweza kuwapa nchi yake furaha itakuwa juu zaidi.
USHAHIDI: Misaada ya matajiri kwa nchi na mabara mazima huwapa 'raha' matajiri. Na mbahili hana furaha. Tena yule ambaye badala ya kutoa kapokea pasi na haki[madhulumu] anakuwa ni tajiri mwenye huzuni/atakosa usingizi etcetc

Ukifuatilia hata kwenye mapenzi kuna wenye umasikini[wanahitaji kuoewa raha] na wenye mawazo ya kitajiri [kutoa raha]. Chunguza yupi, mwanaume yupi anayefurahia mapenzi kati ya yule anayemridhisha/furahisha mpenzi wake na yule asiyemridhisha? Hapo wote[hao wanaume] hufikia mshindo binafsi ila utakuta wanahangaikiaga kuoata dawa za kumfurahisha mtu mwingine sio wao.

Kwa hiyo hata kwa viumbe ni hivyohivyo, kuwasaidia viumbe wengine kuishi kwao ni furaha, watawazaa [watawaleta duniani] watawalinda, watawahudumia na watafurahi hata wakifo ikiwa watakuwa na hakika kuwa wametengeneza tabasamu kwa wengine wanaowajali 😊.

Umesema inahasara kiafya, kiuchumi etc...... haujajua huo uchumi ni kwa ajili ya kuzaa, na afya yooote unayoiona ni kwa ajili ya kuwezesha kuzaa. Kwa hiyo hatupotezi muda, tunatumia muda katika kuzaa. Na hatuharibu afya, tunaitumia afya na uchumi kuzaa na kuhudumia vizazi - ndio matumizi yake [lengo]

It will remain eternally true: Ni heri zaidi kutoa, kuliko kupokea............ ondoa tu mawazo ya kimaskini na ukweli utauona waziwazi.
 
Binadamu ni mifugo ya mimea. Mimea ina wafuga kwa kuwapa oxygen maji na chakula mkisha wiva ina wavuna through death.
Umeiangalia kimaskini sana, kwamba mimea ina uhitaji fulani wa wanyama sana

Lakini pia unaweza kuiangalia kitajiri, kwamba mimea inafurahi tu kuwapa mbuzi oksijeni wavute afu warukeruke kama ndama basi inafurahi kuwaona.

Vivyo hivyo kiumbe anayezaa anafurahi tu kujitolea kuwapa hao wanae furaha. Furaha yao ndio furaha yake.
 
elewa mada, mti ukizaa maembe wenyewe una faida gani na yale maembe
Hicho kitendo cha kuweza kutoa ndio faida yenyewe..........

Umetoa maembe na mbegu za miembe mingine basi wenyewe unafurahi.

Kumbuka hata wewe ukila chakula ukaikusanya nishati hutafurahi hadi uitoe kama sio kwa kazi basi hata kwa gym. Kimsingi tunahangaikia kutoa hapa duniani inayo 'masquerade' kama tendo la kujikusanyia rasilimali.

Hata utajiri ni ili mtu aweze kutoa zaidi. Manaa milele Neno hili litasimama - Ni heri zaidi kutoa kuliko kupokea.
 
Back
Top Bottom