Kuwa ‘Single’ Muda Mrefu: Ni Uhuru au Tatizo la Kutoamini Mapenzi Tena?

Kuwa ‘Single’ Muda Mrefu: Ni Uhuru au Tatizo la Kutoamini Mapenzi Tena?

Last_Joker

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2018
Posts
269
Reaction score
410
Unajikuta mwaka unaisha bado upo solo, hakuna bae wala boo, hakuna mtu wa kukutumia "umelalaje baby?" wala wa kukupa good morning texts zenye emoji ya jua na moyo... lakini wewe hujisikii vibaya. Au labda unajisikia, ila umezoea? Swali linakuja – je, kuwa single muda mrefu ni uhuru mtamu au ni jeraha lisilotibika la mapenzi yaliyopita?

“Single Life” ni Peace au ni Kujiburudisha Kimya Kimya?​

Kuna watu wakiamka asubuhi wanashukuru Mungu hawana stress za wapenzi. Hakuna mtu wa kulalamika, hakuna kufuatiliana, hakuna pressure ya birthday gifts au posting za anniversary.
Wako huru kama tai – wana-focus na maisha, kazi, ndoto zao. Na hawataki kuharibu hiyo "peace" yao kwa kuleta mtu atakayewa-balance emotionally.
Wanasema “mapenzi ni ya muda, amani ni ya kudumu.”

Lakini Vipi Wale Waloumia Mpaka Wakakata Tamaa?​

Sio kila mtu alichagua kuwa single. Wengine wamepigwa character development za kutosha hadi wamefunga mlango wa moyo na kutupa funguo baharini.
Unakuta mtu alikuwa romantic mbaya, sasa hata SMS ya hi inamkumbusha betrayal. Anaona mapenzi ni scam, watu wote ni waongo, na hakuna love ya kweli.
Kuwa single kwake si kwamba anapenda, ni self-defense. Ni kujilinda dhidi ya heartbreak ya pili au ya kumi.

Au Ni Sisi Tumeweka Vigezo Vikali Sana?​

Siku hizi, ukiongea na watu wengi waliopo single, watakwambia wanangoja mtu “mature”, “mwenye vision”, “asiwe mchepukaji”, “mwenye fear of God”, “anajua kujielewa”, “not toxic”...
Lakini vigezo hivyo vimekuwa vikali hadi mtu wa kawaida hawezi kuvipita.
Labda tatizo siyo kukosa mapenzi, bali ni kutoweka realistic expectations. Mapenzi ya ki-movie hayaishi Tanzania, jamani 😂

Hebu Tujiulize...​

  • Ni lini mwisho uliwahi kupenda bila hofu?
  • Unajisikiaje unapowaona watu wako wakipost couples goals?
  • Unaamini bado kuna mtu wa kukupenda real au ushawachoka?

Njoo utoe ya Moyoni hapa kwa Comments​

Wewe ni mtu wa #TeamSingle by choice au umekula matukio hadi ukapewa kitambulisho cha uanachama?
Kuwa single muda mrefu ni uhuru halisi au ni kivuli cha maumivu yaliyopita?


Drop maoni yako pale chini – tuchambue mapenzi bila presha, bila bias, kwa lugha ya mtaa!
 
Kwenye mahusiano unakuwa kifungoni sio 😀 😀
Yeah inakuwa kama upo kwenye gereza flani hivi.. Imagine furaha yako ni kuangalia series na muvi na muda huo unacheki series moja matata sana iliyokuteka moyo afu anakuja manzi kukukata stimu na phone call au text ya kuomba vocha na ukiangalia Mpesa unakuta imebaki 2k ya kununulia bando iwapo hizo zitaisha. Asee inauma kuliko hata kuachwa
 
Unajikuta mwaka unaisha bado upo solo, hakuna bae wala boo, hakuna mtu wa kukutumia "umelalaje baby?" wala wa kukupa good morning texts zenye emoji ya jua na moyo... lakini wewe hujisikii vibaya. Au labda unajisikia, ila umezoea? Swali linakuja – je, kuwa single muda mrefu ni uhuru mtamu au ni jeraha lisilotibika la mapenzi yaliyopita?

“Single Life” ni Peace au ni Kujiburudisha Kimya Kimya?​

Kuna watu wakiamka asubuhi wanashukuru Mungu hawana stress za wapenzi. Hakuna mtu wa kulalamika, hakuna kufuatiliana, hakuna pressure ya birthday gifts au posting za anniversary.
Wako huru kama tai – wana-focus na maisha, kazi, ndoto zao. Na hawataki kuharibu hiyo "peace" yao kwa kuleta mtu atakayewa-balance emotionally.
Wanasema “mapenzi ni ya muda, amani ni ya kudumu.”

Lakini Vipi Wale Waloumia Mpaka Wakakata Tamaa?​

Sio kila mtu alichagua kuwa single. Wengine wamepigwa character development za kutosha hadi wamefunga mlango wa moyo na kutupa funguo baharini.
Unakuta mtu alikuwa romantic mbaya, sasa hata SMS ya hi inamkumbusha betrayal. Anaona mapenzi ni scam, watu wote ni waongo, na hakuna love ya kweli.
Kuwa single kwake si kwamba anapenda, ni self-defense. Ni kujilinda dhidi ya heartbreak ya pili au ya kumi.

Au Ni Sisi Tumeweka Vigezo Vikali Sana?​

Siku hizi, ukiongea na watu wengi waliopo single, watakwambia wanangoja mtu “mature”, “mwenye vision”, “asiwe mchepukaji”, “mwenye fear of God”, “anajua kujielewa”, “not toxic”...
Lakini vigezo hivyo vimekuwa vikali hadi mtu wa kawaida hawezi kuvipita.
Labda tatizo siyo kukosa mapenzi, bali ni kutoweka realistic expectations. Mapenzi ya ki-movie hayaishi Tanzania, jamani 😂

Hebu Tujiulize...​

  • Ni lini mwisho uliwahi kupenda bila hofu?
  • Unajisikiaje unapowaona watu wako wakipost couples goals?
  • Unaamini bado kuna mtu wa kukupenda real au ushawachoka?

Njoo utoe ya Moyoni hapa kwa Comments​

Wewe ni mtu wa #TeamSingle by choice au umekula matukio hadi ukapewa kitambulisho cha uanachama?
Kuwa single muda mrefu ni uhuru halisi au ni kivuli cha maumivu yaliyopita?


Drop maoni yako pale chini – tuchambue mapenzi bila presha, bila bias, kwa lugha ya mtaa!
Kwani ukiwa ni mpenda Ice cream ni lazima uwe na kiwanda cha Ice cream? Watu wanapenda nyama na maziwa na kila siku wanavipata lakini hawafugi.
Kuna mfugaji anafuga ng'ombe na mbuzi na kuku lakini hali nyama kila siku, ila asiyemfugaji hula kila siku.
Kwa sasa maisha tunayoishi ni take away, hakuna ulazima wa kufunganafungana.
Kama qewe kazi yako ni kuuza duka au ajili yako ni kwenda kazini na jioni kurudi nyumbani kila siku haina shida, oa au olewa, lakini kama kazi yako ni leo hapa kesho pale, kwanini usifuate flow ya kazi yako kwa kuishi na bag mgongoni? Ya nini uoe au uolewe na mtu ambaye kimsingi atakuwa ni mtunza nyumba?

Vijana wanatakiwa kabla ya kuoa au kuolewa wajitafakari na mfumo wao wa maisha/ajira kama upo inline na ndoa/mahusiano.

Huenda mahusiano si kitu kibaya kabisa, lakin8 hata kiatu kinachokubana siku zote kitakuletea maumivu, au ukigeuza viatu au suti/nguo bila ya kujali vina thamani kiasi gani utaishia kuadhirika na heshima kushuka .
Mahusiano/ndoa ni jambo jema, huenda mfumo wako wa maisha tayari una settings ambazo haziendano na mahusiano/ndoa hiyo, labda unastahili aina tofauti na si yale ya kimazoea
 
Back
Top Bottom