Kuvuta Bangi Ruksa Colorado/Marekani!!

Kuvuta Bangi Ruksa Colorado/Marekani!!

Leseni zaidi ya mia tatu zimetolewa na Jiji la Denver katika jimbo la Colorado kuanzia majuzi za kuuza bangi na kwamba sasa ni ruksa kwa yeyote mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea kuvuta bangi katika jimbo hilo. Inasemekana kuwa kwa utafiti uliofanyika kisayansi ni kwamba bangi inaweza ikasaidia sana katika kutibu maradhi kadhaa na pia husaidia kuwapatia watu usingizi mnono. Upepo huu ukifika kwetu hapa tutakuwa tumekwisha na hasa katika hali hii ya ugumu wa maisha. Tukiwa na wabunge wengi wanaovuta bangi mswada huu utapita kilaini. Tujihadhari!!!

Mtakuwa mmekwisha kivipi, fafanua!
 
Ki Ukweli Mimi Naona Hii Ni Fursa Hasa Kwa Vijana Wa Kitanzania Tunaomba Serikali Itengeneze Sera Ya Kusafirisha Bangi Kwenda Marekani Nafikiri Itaongeza Pato La Taifa. Biashara Hii Itaongeza Mapato Ya Kodi As Exportation Tax Pia Itaongeza Ajira Kwa Vijana Wa Kitanzania. Hakika Hii N Bonge Ya Fursa Kwa Sisi Watanzania
 
Wakulima wa hili jani wapo ila tatizo serikali, iruhusu kwanza serikali watu wafanye biashara.
Kitu cha Arusha.
 
Ki Ukweli Mimi Naona Hii Ni Fursa Hasa Kwa Vijana Wa Kitanzania Tunaomba Serikali Itengeneze Sera Ya Kusafirisha Bangi Kwenda Marekani Nafikiri Itaongeza Pato La Taifa. Biashara Hii Itaongeza Mapato Ya Kodi As Exportation Tax Pia Itaongeza Ajira Kwa Vijana Wa Kitanzania. Hakika Hii N Bonge Ya Fursa Kwa Sisi Watanzania

Kwanza USA ni katika baadhi tu ya majimbo yameruhusu matumizi ya jani. Ikumbukwe pia hawaagizi toka nje ya nchi; sheria yao inaambatana na kukuza uzalishaji wa ndani. Hivyo usilimezee mate soko la USA; halituhusu na halitotuhusu kwa muda mrefu.


Issue ni kwa nchi jirani ambako mzigo unakamatwa ukipelekwa kila kukicha na matumizi mengine ya bangi-mfano: kuondoa maumivu kwa wagonjwa wa kansa. Uhalalishaji wa kilimo cha zao hili ungekuwa tayari na soko kwa mahitaji walau haya yaliyowazi
 
Hata pale tabata dampo, manzese, mwananyamala ni ruksa kuvuta bange kauanzia saa 12 jioni.

Hata huku kijiji cha Kwenkeyu wilayani Korogwe bangi ni zao halali na kijiji kinakusanya ushuru kwa Wakenya wanaokuja kuinunua.
 
"if you fail to fight,join them" km serikali inaona hii vita ya kupambana na bangi ni ngumu,iruhusu tu watu wafanye biashara
 
watanzania ni wajinga sababu hawajui kati ya bange na pombe kipi kina matatizo... poor u tanzanians
 
Ili kuondoa kujaza magereza na mahabusu za nchi yetu kwa kesi za kukamatwa na bange na gongo,serikali inge halalisha hivi vitu viuzwe madukani ili serikaki ipate kodi kwani juhudi za kudhibiti ni ngumu sana.
 
Back
Top Bottom