Kuvunja poverty circle sio kitu rahisi

Nashukuru mungu nilisoma kwa scholarship 100% non return fund ila jua kali la mtaa naliona na napambana
Ila mtoa uko sahihi
 
Huu Uzi mkuu umetugusa wengi tuliotokea familia hizo, tunapambana nayo
 
Kumbukumbu la Torati 28:13

Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;

Kumbukumbu la Torati 28:1-14 SUV
1 Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako. 3Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani. 4Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, kuongezeka kwa ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo wako. 5Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. 6Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. 7 BWANA atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba. 8 BWANA ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo BWANA, Mungu wako. 9 BWANA atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya BWANA, Mungu wako, na kutembea katika njia zake. 10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la BWANA, nao watakuwa na hofu kwako. 11 BWANA atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi BWANA aliyowaapia baba zako kwamba atakupa. 12Atakufunulia BWANA hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe. 13BWANA atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya; 14msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lolote, kwenda mkono wa kulia wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.

Kumbukumbu la Torati 11:27

baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, niwaagizayo leo;


Mithali 10:6

Baraka humkalia mwenye haki kichwani; Bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu.


Mithali 28:20

Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele; Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
 
Kuna Jamaa mmoja ana miliki mjini maghorofa ya kutosha,alikuja mjini akiwa na miaka 15 akaweka nadhiri tarudi kijijini nikiwa maiti au tajiri, akawa analala nje kariakoo kwenye maduka nje,akiamka Asubui anauza mifuko ya rambo, enzi hizo kwa Mali kauli yaani kuchukua kwa wenye Duka Asubui unazungusha unachukua cha juu,ikibaki jioni unarudisha dukani iliyobaki,akawa anasave kidogo kidogo kila siku,akafungua zipu wala vizibo,kwa miaka mitatu alikuwa na hela ya kutosha akafungua kijiwe akakisimamia ndani ya miaka miwili akawa na Duka kubwa,mwaka uliofata akaongeza Duka baadae akawa na maduka akaanza kwenda china kuchukua mizigo baadae akawa ajent wa mizigo anatumiwa na wachina kuuza mizigo kwa Jumla.Hapa kilichomtoa ni uaminifu,nidham,na kujiconnect na waliofanikiwa,ukikaa na mashetani utabaki kuwa shetani.
 
Nakuelewa sana mkuu
 
Asante kwa ushauri mzuri
 
Barikiwa sana
 
Kwa wote wanaopigana vizuri kuvuka viunzi vya umasikini.

Nawatakia mafanikio makubwa na mapema.

Mara nyingine strategy itakutaka uwafungie vioo watu fulani kwa muda fulani, sio kwa nia mbaya au uchoyo, bali kwa nia ya kujenga capacity ya kusaidia vizuri zaidi.

Ukitaka kusaidia sana wakati wewe mwenyewe mtaji wa manati, hapo ndipo wote mnabaki mnazunguka katika mzunguko wa umasikini.

Uzuri ni kwamba, ukiwafungia vioo watu fulani kwa muda mfupi kwa sababu zenye tija za malengo ya muda mrefu, malengo yakatimia na ukaweza kusaidia vizuri, walio na akili wataelewa.

Masikini wa kipato kumsaidia masikini wa kipato mwenzake kwa kipato ni vigumu sana.
 
Ungeandika kiswahili mwanzo mwisho,
Ila umenena kweli tupu mkuu, nayapitia yote uliyaandika hapa, ningekua milionea kwa sasa kama sio ukubwa wa familia na umaskini tuliokuanao, na mbaya zaidi kadri unavyozidi kuwasaidia ndugu zako ili waweze kujitegemea kwa kesho wasiwe mzigo kwako ndio wanazidi kukurudisha chini,
Mfano mdogo nimemfungulia mdogo angu biashara mbili kwa wakati tofauti na za mtaji mkubwa tuu sio chini ya ml7 lakin kayafilisi yote na watoto wa3 kaniachia hajui wanalala vipi wala wanakula nini.
Sisi maskini hua tunaangamizana wenyewe kwa wenyewe, matajiri wana umoja wa kuinuana sisi tuna umimi wa kushushana, na hili sio mimi tuu nayashuhudia kwa watu wengi anafanikiwa mmoja anafanya juhudi kuwainua nduguze lakin ndio wanazidi kumdumaza.
 
Kweli ukifunga vioo hii inasaidia sana, lakin unaweza ukapata nafasi ya kumuinua mmojawapo kwa kumuajiri lakini mwisho wa siku ndio anazidi kukumaliza, au ukamtaftia kazi mahali siku si nyingi kaharibu, nimeyashuhudia sana haya,
Niseme tu kiukweli kama wafanyakazi wa sekta zote kuanzia serikalini hadi sekta binafsi wangekua waaminifu umaskini kwa nchi ungekua umepungua kwa 50% ya ulivyo sasa.
 
Umasikini ni hali ya MTU kushindwa kuyatumia mazingira yanayomzunguka kutatua matatizo yake.Shida IPO kwenye mindset zaid kuliko hali halisi, ndo maana mgeni anatarajika kwa kuwatumisha wenyeji.Umasikini ni hali ya kushindwa kuchukua hela toka kwa wanaokuzunguka.
 
Nakuelewa sana mkuu
 
Kila MTU anauhitaji,ukimtimizia mahitaji yake unapata hela,mfano kila siku MTU atatumia huduma au bidhaa.ni wewe ni kulibadili Wazo kuwa hela.
 
Thanks mkuu
Tutafika tu
 
Sasa hapo kwenye kutumia Elimu kujiajiri ndio kuna kaz wakati mtaji hauna
 
Sio kweli mkuu maisha yanakila nafasi ya wewe kufanikiwa na kutokufanikiwa usilauma wazazi kwa kufail fight for all weapons that you have trust in me you will never loose your part
Totally true!
Inahitajika hata kuhama na kutoongea na some of the ndugu, it’s tough lakini ukiwa na focus lazima utashinda tu!
Kitakacho kushinda ni wewe mwenyewe walahi!
Kuna mtu ninamfahamu aliiba ngombe wa baba yake ili imsaidie katika kujikomboa na umaskini na akafanikiwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…