Kuvuliwa ukuu sekondari kuendane na maafisa elimu mikoa na wilaya zifuatazo.

DT125

JF-Expert Member
Oct 19, 2011
380
573
Napongeza kuvuliwa madaraka wakuu wa shule za sekondari zilizofanya vibaya hata kama zipo sababu zilizo nje wa uwezo wao. Napendekeza na Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam na maafisa elimu sekondari wa wilaya Msalala, Kisarawe na Morogoro(V) pamoja na wilaya kumi za mwisho wavuliwa madaraka. Afisa elimu mkoa ashushwe awe wa wilaya na wale wa wilaya wakawe wakuu wa shule. Sababu wa Dar es Salaam shule zake nyingi kuwa za mwisho, maafisa elimu sekondari wilaya hizi, wilaya zao kufanya vibaya ukilinganisha na mwaka uliopita. Wilaya za kumi za mwisho (Rufiji, Mafia,Bahi, Korogwe, Ruagwa, Musoma, Liwale, Nanyumbu, Kusini na Nachingwea. Wafuatao wapate pongezi Afisa Elimu mkoa wa Njombe na maafisa elimu sekondari wilaya ya Wangingombe, Njombe na Ludewa zote za mkoa wa njombe wamepandisha ufaulu ukilinganisha na mwaka jana. Wengine wa kupongezwa ni wilaya kumi za kwanza.
 
Napongeza kuvuliwa madaraka wakuu wa shule za sekondari zilizofanya vibaya hata kama zipo sababu zilizo nje wa uwezo wao. Napendekeza na Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam na maafisa elimu sekondari wa wilaya Msalala, Kisarawe na Morogoro(V) pamoja na wilaya kumi za mwisho wavuliwa madaraka. Afisa elimu mkoa ashushwe awe wa wilaya na wale wa wilaya wakawe wakuu wa shule. Sababu wa Dar es Salaam shule zake nyingi kuwa za mwisho, maafisa elimu sekondari wilaya hizi, wilaya zao kufanya vibaya ukilinganisha na mwaka uliopita. Wilaya za kumi za mwisho (Rufiji, Mafia,Bahi, Korogwe, Ruagwa, Musoma, Liwale, Nanyumbu, Kusini na Nachingwea. Wafuatao wapate pongezi Afisa Elimu mkoa wa Njombe na maafisa elimu sekondari wilaya ya Wangingombe, Njombe na Ludewa zote za mkoa wa njombe wamepandisha ufaulu ukilinganisha na mwaka jana. Wengine wa kupongezwa ni wilaya kumi za kwanza.
Inapendeza, ukifaulisha unapanda cheo ukifelisha unakula demotion, kwa mwendo huo tutapunguza uzembe
 
Napongeza kuvuliwa madaraka wakuu wa shule za sekondari zilizofanya vibaya hata kama zipo sababu zilizo nje wa uwezo wao. Napendekeza na Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam na maafisa elimu sekondari wa wilaya Msalala, Kisarawe na Morogoro(V) pamoja na wilaya kumi za mwisho wavuliwa madaraka. Afisa elimu mkoa ashushwe awe wa wilaya na wale wa wilaya wakawe wakuu wa shule. Sababu wa Dar es Salaam shule zake nyingi kuwa za mwisho, maafisa elimu sekondari wilaya hizi, wilaya zao kufanya vibaya ukilinganisha na mwaka uliopita. Wilaya za kumi za mwisho (Rufiji, Mafia,Bahi, Korogwe, Ruagwa, Musoma, Liwale, Nanyumbu, Kusini na Nachingwea. Wafuatao wapate pongezi Afisa Elimu mkoa wa Njombe na maafisa elimu sekondari wilaya ya Wangingombe, Njombe na Ludewa zote za mkoa wa njombe wamepandisha ufaulu ukilinganisha na mwaka jana. Wengine wa kupongezwa ni wilaya kumi za kwanza.
Afisa elim wa dar hana hata mwez tangu achukue ofisi.
Na hao maafisa elim unaowataja sio chanzo cha vijana kufeli,inaonesha ww haupo kwenye sekta ya elimu,tembelea hayo maeneo kabla huja conclude,hata wqkikushswa na wengine watashushwa pia
 
Wanafunzi wenyewe dar es salaam kazi kunyoa viduku...halafu ban ale mkuu wa shule!unfair kabisa!
Kama serikali itawabana wanafunzi na wazaz wao basi ufaulu utaonekana.Wazaz hawawafatilii watoto kabisaaaa,wapo watoto mwaka mzimaaaaa hawajawah kufika shule kwa wakat.Daily wanachelewa au wanajificha MAPORINI
 
Tatizo ni kubwa kuliko wanavyotuaminisha kuwa ni wakuu wa shule, elimu ni miundo mbinu, hizo shule hata wampeleke mkuu wa Marian boys kuziongoza wanafunzi watafeli tu, wasiweke siasa kwenye taaluma, serikali iwekeze kwenye hizi shule na sio kutegemea matokeo mazuri wakati miundombinu ni ovyo
 
Kumbuka mtihani unafanywa na mwanafunzi sio Mkuu wa shule.

Kulazimisha wakuu wa shule wafaulishe ni kuchoche wasaidie udanganyifu katika mitihani.

Suala waulizwe wanafunzi SBB za wao kufeli.

Na wakaguzi wakague kama walimu wa kila somo walifundisha kwa mujibu wa mwongozo na walimaliza topics. Then kwenye udhaifu kutatuliwe na kama ni adhabu apate mhusika haswa.

Viongozi wetu mfanye kazi bila chembe ya siasa. Kuboresha elimu nchini
 
Kama serikali itawabana wanafunzi na wazaz wao basi ufaulu utaonekana.Wazaz hawawafatilii watoto kabisaaaa,wapo watoto mwaka mzimaaaaa hawajawah kufika shule kwa wakat.Daily wanachelewa au wanajificha MAPORINI
Inainesha wewe ni mtaakam wa mambo ya elimu umenena mulemule,tatizo siasa nyingi tz huyu ndakichako kaharibiwa kabisa palitakiwa pakaliwe pande tatu kujadili hili suala la anguko la elimu yaani WAZAZI,WAALIMU NA WANAFUNZI WENYEWE WALOFELI jibu lingeonekana,sasa kukurupukia waalimu tu na kuwaacha wazazi na walofeli wenyewe ni bure
 
Inainesha wewe ni mtaakam wa mambo ya elimu umenena mulemule,tatizo siasa nyingi tz huyu ndakichako kaharibiwa kabisa palitakiwa pakaliwe pande tatu kujadili hili suala la anguko la elimu yaani WAZAZI,WAALIMU NA WANAFUNZI WENYEWE WALOFELI jibu lingeonekana,sasa kukurupukia waalimu tu na kuwaacha wazazi na walofeli wenyewe ni bure
Hao watoto wa feza,wazaz wao wapo makini sana kufatilia taaluma za watoto wao,mzaz anamlipia mtoto ada mil 8 na bado mtoto anasimamiwa kimasomo na mzaz.Serikali haijaweka mechanisms za kuwabana wazaz wasiotimiza makujumu.Mzaz hamfatiliii mtoto kwa chochote zaid ya kumpa nauli tu.Mzaz hadi leo hajafata report ya mtoto ya mwaka jana shuleni,mzaz hajui mwanae amefaulu form II au lah na ana smart phone,mzaz anapigiwa simu kuelezwa shida za mtoto wala hajali,mzaz hahudhuriii vikao vya shule.Watoto hawa wanahitaji UTATU.
SHULE
Mwanafunzi
MZAZI
Watafeli sana watoto,serikali kwakua inawalipia ada Iwabane wazaz na wanafunzi,bila hivyo watafeli SANA
 
Mimi sina shida na waalimu,wanapiga kazi sana mbali ya kuwa serikali haiwajali,hii suala la elimu bure ndo linaua elimu yetu wazazi wengi wa vijijini hawajui umuhimu was elimu so kwakuwa ni bure haumii hata mwanae akifeli.
 
Napongeza kuvuliwa madaraka wakuu wa shule za sekondari zilizofanya vibaya hata kama zipo sababu zilizo nje wa uwezo wao. Napendekeza na Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam na maafisa elimu sekondari wa wilaya Msalala, Kisarawe na Morogoro(V) pamoja na wilaya kumi za mwisho wavuliwa madaraka. Afisa elimu mkoa ashushwe awe wa wilaya na wale wa wilaya wakawe wakuu wa shule. Sababu wa Dar es Salaam shule zake nyingi kuwa za mwisho, maafisa elimu sekondari wilaya hizi, wilaya zao kufanya vibaya ukilinganisha na mwaka uliopita. Wilaya za kumi za mwisho (Rufiji, Mafia,Bahi, Korogwe, Ruagwa, Musoma, Liwale, Nanyumbu, Kusini na Nachingwea. Wafuatao wapate pongezi Afisa Elimu mkoa wa Njombe na maafisa elimu sekondari wilaya ya Wangingombe, Njombe na Ludewa zote za mkoa wa njombe wamepandisha ufaulu ukilinganisha na mwaka jana. Wengine wa kupongezwa ni wilaya kumi za kwanza.
Ni sahihi kabisa,na pia napendekeza mgonjwa akifariki daktari apewe demotion, hii itasaidia kupunguza uzembe,majambazi wakizidi maaskari wafukuzwe kwakuwa wameshindwa kutimiza wajibu wao wa ulinzi na usalama,wakili wa serikali akishindwa kesi nae apumzishwe ili kuongeza uweledi na na walioshindwa kuwapa watumishi stahiki zao maana yake wameshindwa kutimiza wajibu nao wapewe demotion ,nafikiri hii itakua sahihi sana ili kuongeza uweledi
 
Pia Pia Wagonjwa wanapokufa Hospitalini MGANGA MKUU WA HOSPITAL HIYO ASHUSHWE CHEO AWE DAKTARI WA KAWAIDA, MGANGA MKUU WA WILAYA,MKOA,NAE ASHUSHWE CHEO,N.K, UHALIFU UKITOKEA MKUU WA KITUO CHA POLISI ASHUSHWE CHEO , GOROFA LIKIPOROMOKA INJINIA WA WILAYA ASHUSHWE CHEO, Siasa at Work.
 
Tatizo la elimu Tanzania si la watendaji pekee, tatizo kubwa ni mfumo mzima toka chekechea mpaka Chuo kikuu, na utendaji wa wizara toka nzima toka utawala katika chekechea mpaka Wizarani. Elimu haina vision wala mission, kinacholengwa ni kuhitimu tu na ufaulu kuongezeka, Wakati wenzetu huku nje wamewekeza kwa asililmia 100, katika Maarifa na ujuzi, yaani kila hatua ambayo mtoto anapiga lazima aoneshe kwa nadharia na vitendo, ujuzi na maarifa aliyoyapata toka ngazi moja kwenda nyingine. Ndiyo maana watoto wanaanza kuibuliwa na kutengwa kwenye makundi ya specialization mapema ili kupata wataalamu wabobevu. Hapo kwetu ni tambo za ilani ya chama tawala ndo inayotawala mstakabali wa maendeleo ya elimu, bado kuna safari ndefu, kama miaka 100 kufikia hapa walipo nchi kama Hong kong au Japan.
 
Napongeza kuvuliwa madaraka wakuu wa shule za sekondari zilizofanya vibaya hata kama zipo sababu zilizo nje wa uwezo wao. Napendekeza na Afisa elimu wa mkoa wa Dar es salaam na maafisa elimu sekondari wa wilaya Msalala, Kisarawe na Morogoro(V) pamoja na wilaya kumi za mwisho wavuliwa madaraka. Afisa elimu mkoa ashushwe awe wa wilaya na wale wa wilaya wakawe wakuu wa shule. Sababu wa Dar es Salaam shule zake nyingi kuwa za mwisho, maafisa elimu sekondari wilaya hizi, wilaya zao kufanya vibaya ukilinganisha na mwaka uliopita. Wilaya za kumi za mwisho (Rufiji, Mafia,Bahi, Korogwe, Ruagwa, Musoma, Liwale, Nanyumbu, Kusini na Nachingwea. Wafuatao wapate pongezi Afisa Elimu mkoa wa Njombe na maafisa elimu sekondari wilaya ya Wangingombe, Njombe na Ludewa zote za mkoa wa njombe wamepandisha ufaulu ukilinganisha na mwaka jana. Wengine wa kupongezwa ni wilaya kumi za kwanza.
Mtoto kufeli ni sababu nyingi sana zinasababisha,kumtuhumu tu mkuu wa shule na kumshusha madaraka hata haisaidii. Tuangalie hizo shule zilizofeli,mazingira yake,watoto walimaliza waliingia na ufaulu gani. Wazazi wa watoto waliofeli je,wao wenyewe wako serious kweli? Mwanafunzi toka anavyoingia tu firm three walimu na wazazi hujua hatima yake...kwamba huyu ni wa div zero au one. Kumlaumu tu mwalimu binafsi sioni kama ni kumtendea haki. Hao wakuu wa wilaya wanaotumia media kama kujisifu kwa kutaka wakuu wa shule husika wavuliwe madaraka,hivi kwa nini wasianze wao kuachia madaraka kwamba wameshindwa kuongoza wilaya zao katika swala la elimu!? Tatizo walifikiria madawati ndo kitu kinachofanya watoto wafeli,nguvu nyingi sana iliwekwa kwenye madawati. Litafutwe suruhisho la watoto kufeli na sio kushusha vyeo.
 
Hivi wanafunzi wanafeli wenyewe au wanafelishwa???
MKUU NALO HILO SWALI"MAJIBU KAMA WANAFELISHWA INA MANA MTIHANI HUFANYWA NA MWALIMU NA KAMA WANAFELI WENYEWET UDHALILISHAJI KWA WAKUU WA SHULE WA NINI?"
 
Back
Top Bottom