Dah!! Kiukweli WTZ tumekuwa wajinga sana na hasa vijana wa sasa. Tumekuwa na tabia ya kuiga mambo bila kujua chanzo chake. Kuvaa kata K kwa sasa ndo imekuwa fassion ya vijana. Kijana yeyote asipovaa mlegezo anaona kuwa atakuwa mshamba mbele ya vijana wa mjini. HUU NI UJINGA kutokujiamini na kutojitambua kama vijana. Kijana yeyote mwenye kujitambua mwenye akili timamu na anayejiamin hawezi kuvaa mlegezo(kata K). Ninajiuliza hivi taifa letu miaka 20 ijayo litakuwaje??? Maana 65% ya vijana wanavaa mlegezo alimaarufu KATA K. Je, watoto wao watakuwa na maadili kama vijana wa zamani au itabaki historia tu?? VIJANA BADILIKENI NA MJIHESHIMU kuvaa mlegezo sio ujanja bali ni ujinga tu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.