Kutongoza Kabla ya Simu, Facebook na Twitter

Kutongoza Kabla ya Simu, Facebook na Twitter

Mzalendowetu

Member
Joined
May 22, 2012
Posts
87
Reaction score
36
Kabla ya matumizi ya simu, facebook, twiter n.k sanaa ya ushawishi (kutongoza) ilikuwa na styles za pekee kama vile kumsubiri msichana akiwa ametumwa dukani, kuandikiana barua n.k Tupia ya kwako
 
kuna wengine walikuwa wanawekewa order na wazazi wao...
 
Me nilikuwa naandika kwenye ukuta wa shule au godauni kwamba me tarimo nakupenda sana manka john bas akipita hapo akiona full kutafutwa.
 
hizo mambo za kutuma mtu zilimtokea puani shija wa bongo movie. alimtuma sajuki aeende kumtongozea kwa wastara.
kufika kwa wastara akatongoza yeye kama yeye na akakubaliwa.
ila nampongeza sana marehemu sajuki alioa kabisa wastara. RIP sajuki.

' shija aliwai kukiri ili jambo ni kweli'
 
unamface binti unamwambia halafu anakuambia niandikie barua.Unamwandikia barua unampa dogo anaipeleka, unakuta binti tayari alikuwa na kumbe binti tayari alishakuwa na mtu anampelekea halafu aibu inakukumba.Wakati mwingine unamtuma mdada akuunganishie anakuwekea kausibe kumbe yeye nae anataka.Mwingine unamtuma kijana anajipigia pande mwenyewe yaani ilikuwa ni vituko tupu.
 
hizo mambo za kutuma mtu zilimtokea puani shija wa bongo movie. alimtuma sajuki aeende kumtongozea kwa wastara.
kufika kwa wastara akatongoza yeye kama yeye na akakubaliwa.
ila nampongeza sana marehemu sajuki alioa kabisa wastara. RIP sajuki.

' shija aliwai kukiri ili jambo ni kweli'

Teheeee ati anajipasia mwenyewe dah! Mdada nae kumbe kakupenda asee gud memories
 
Mi nilikuwa navizia dirisha la jikoni anakopika. Akiingia tu naita jina kwa sauti ya chini, sasa kuna siku si akaingia mama yake. Na kwa jinsi wanavyofanana you can imagine nini kilofuata....

Halafu nilishaandika barua kwa wino mweusi, kijani blue na nyekundu yaani kila paragraph na rangi yake. Unaifunga kwenye bahasha iliyopulizwa pafume. Yaani unaifungi ile harufu humo
 
Kabla ya matumizi ya simu, facebook, twiter n.k sanaa ya ushawishi (kutongoza) ilikuwa na styles za pekee kama vile kumsubiri msichana akiwa ametumwa dukani, kuandikiana barua n.k Tupia ya kwako

Zamani kabisa, sisi tulikuwa tunatafutiwa na wazazi!
 
Anaesema zamani sio raha afeeee!
Mi nilipenda tulivyokua tunawasiliana, mtoto alikua geti kiasi flan, afu ukimuona wako nyomi, mara yuko na maza or faza wake duh! Sasa mi nilikua sichoki kujipitisha kwao, na nikimkwaa tu lazime aniibe, natembea hafu kama najipiga kisigino cha mguu kwa mkono, natulia mbele, mtoto uyooo. Hata kama kabanwa alichopoka tu. Aaaaaa! Zamani rahaaa!
 
Kuna watu wengine walikuwa wambeya akiona tu demu kapewa barua anaenda kusemea kwa mwalimu, mwalimu anamkagua demu mpaka anatoa ile barua, sikilizia kichapo. Shule nzima inaitwa mnachapwa hadharani afu mkitoka hapo aibu yake mpaka wiki ndo mtu unasahau!
 
Ilikuwa noma, kuna siku niliandika barua kwenda kwa mchum ikadakwa na mwalimu alivyokuwa anakagua madafutari.... ilikuwa aibu iliposomwa hadharani ilibidi nikache masomo kwa muda kupisha soo, halafu sasa demu mwenyewe naye akawa anataniwa kishenzi hivyo kila kitu kikatumbukia nyongo!
 
Kabla ya matumizi ya simu, facebook, twiter n.k sanaa ya ushawishi (kutongoza) ilikuwa na styles za pekee kama vile kumsubiri msichana akiwa ametumwa dukani, kuandikiana barua n.k Tupia ya kwako

mwaka gani huo ambao kulikuwa hamna simu???1940s??im not that young lakini nilitumia simu[landline] kutongozea sana,tena unaongea hata 4hrs bili ndogoooo[hata sijui ilikuwa kiasi gani coz silipi mimi]unavuta redio kaseti pembeni unaweka muziki laini pale mnaendelea....na sasa hivi sina facebook wala twitter lakini hainizuii kutongoza.....
 
Back
Top Bottom