Kutokwa jasho usiku

Kutokwa jasho usiku

Guus

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2013
Posts
1,167
Reaction score
904
Wana JF,

Kama nilivyoandika katika "Heading", nina kama miezi mitano nimekuwa na shida ya kutoka jasho usiku nikiwa usingizini. Muda wote wa mchana na hadi pale ninapoenda kulala huwa sijisikii shida wala tatizo lolote. Lakini nikiwa usingizini basi ni kuhesabu masaa 3 hadi 4 lazima nishtuke, maana huwa nakuwa nimelowanisha shuka kwa kiwango cha kutia shaka (linakuwa halitamaniki tena). Kwa sasa nimeamua kulala na taulo pembeni, maana ninaposhtuka mwili huwa bado unajasho, kwa hiyo natumia taulo kujifuta. Kwa sasa siku zinazotokea kuwa sijatoa jasho usiku katika wiki ni za kuhesabika. Nimekwisha enda hospitali, na daktari alishauri nifanye check-up ya TB ambapo "Chest X-ray ikaonesha "normal", vipimo vingine ni HIV, Full blood count, Renal, Liver, Bone profile ambavyo vyote vipo "normal". Pia niliambiwa "thyroid function" ni "normal" na hakuna evidence yeyote ya kuonesha "Autoimmune disease". Hapa daktari ameniambia niwe na amani, kwa kuwa amejiridhisha na hayo yote basi kama kutakuwa na tatizo lingine litakalojitokeza nimfahamishe. Lakini aliniambia nisiwe na wasiwasi, ni vitu vinavyoweza kutokea kwa sababu ya mabadiriko ya mwili. Sasa shida yangu mimi ni kukosa "Comfortability"; kitendo cha kuingia kitandani na taulo na kushtuka usiku vinanikwaza sana.

Sasa madaktari humu mnisaidie ni nini laweza kuwa tatizo? Msaada wenu ni muhimu. Huyu daktari wangu ni muelewa sana, naweza shauriana naye kwa kutumia majibu yenu na akayafanyia kazi. Msaada wanajamvi.
 
Unaishi wapi? Je, una hakikisha chumbani kwako kuna hewa ya kutosha ili kupunguza utokwaji wa jasho? Kwa jiji kama la Dar wengi hutumia AC au fan ili kupunguza hali ya joto iliyopo Dar.
 
Nimeshangaa dr wako hajakupima sukari. Hebu nenda hata zahanati, asubuhi usipate breakfast, halafu upime sukari.

Pole sana. Jitahidi uwe unakunywa maji mengi sana wakati wa mchana, walau 3lts.
 
Kunywa maji mengi kukorrect dehydration maana kwa hali hiyo unapoteza maji mengi sana kupitia Jasho.


Jambo jingine nakushauri nenda hospitali nyingine kubwa ukafanye vipimo kuhakikisha zaidi majibu ya mwanzo, hiyo siyo hali ya kawaida.
 
Kwa sasa nina kama mwezi na nusu nipo Lyon ila kwa bongo ninaishi Dom. Thanks BAK

Unaishi wapi? Je, una hakikisha chumbani kwako kuna hewa ya kutosha ili kupunguza utokwaji wa jasho? Kwa jiji kama la Dar wengi hutumia AC au fan ili kupunguza hali ya joto iliyopo Dar.
 
Thanks King'asti kwa kutoa moja ya yanayoweza kuwa sababu, nitakwenda kucheki. Thanks

Nimeshangaa dr wako hajakupima sukari. Hebu nenda hata zahanati, asubuhi usipate breakfast, halafu upime sukari.

Pole sana. Jitahidi uwe unakunywa maji mengi sana wakati wa mchana, walau 3lts.
 
Mkuu Chakii, sasa mwili umekuwa kama tofali zinazomwagiliwa; muda wote ni maji.
Kwa hospitali, hii hospitali niliyoenda usiwe na mashaka nayo; hata hivyo hivi vipimo wamevirudia mara 3 katika miezi 3 tofauti.

Kunywa maji mengi kukorrect dehydration maana kwa hali hiyo unapoteza maji mengi sana kupitia Jasho.


Jambo jingine nakushauri nenda hospitali nyingine kubwa ukafanye vipimo kuhakikisha zaidi majibu ya mwanzo, hiyo siyo hali ya kawaida.
 
Dalili ya kisukari hiyo, wahi hospitalini kacheck kwanza then tujulishe tafadhali
 
Jamani Lyon ipo mambele huko france msifikiri amepimia hospitali zetu wanazokata kichwa badala ya miguu.

Kiongozi huo ushauri wa kucheki sukari ni muhimu japo na mimi nina shida kama yako na nilipima mpaka kisukari kibongobongo hamna.

Mimi shida kubwa ni uric acid ndo huwa inanisumbuaga.
 
Body temperature Lina correspond na chemicals za mwili kukufanya upate usingizi. Mara nyingi mwili hutulia body temperature ikiwa chini na hii hutokea mkabala wa saa nane, Tisa mpaka 10 asubuhi.

Kama unaouwezo weka AC au nunua fan
 
Wana JF,

Kama nilivyoandika katika "Heading", nina kama miezi mitano nimekuwa na shida ya kutoka jasho usiku nikiwa usingizini. Muda wote wa mchana na hadi pale ninapoenda kulala huwa sijisikii shida wala tatizo lolote. Lakini nikiwa usingizini basi ni kuhesabu masaa 3 hadi 4 lazima nishtuke, maana huwa nakuwa nimelowanisha shuka kwa kiwango cha kutia shaka (linakuwa halitamaniki tena). Kwa sasa nimeamua kulala na taulo pembeni, maana ninaposhtuka mwili huwa bado unajasho, kwa hiyo natumia taulo kujifuta. Kwa sasa siku zinazotokea kuwa sijatoa jasho usiku katika wiki ni za kuhesabika. Nimekwisha enda hospitali, na daktari alishauri nifanye check-up ya TB ambapo "Chest X-ray ikaonesha "normal", vipimo vingine ni HIV, Full blood count, Renal, Liver, Bone profile ambavyo vyote vipo "normal". Pia niliambiwa "thyroid function" ni "normal" na hakuna evidence yeyote ya kuonesha "Autoimmune disease". Hapa daktari ameniambia niwe na amani, kwa kuwa amejiridhisha na hayo yote basi kama kutakuwa na tatizo lingine litakalojitokeza nimfahamishe. Lakini aliniambia nisiwe na wasiwasi, ni vitu vinavyoweza kutokea kwa sababu ya mabadiriko ya mwili. Sasa shida yangu mimi ni kukosa "Comfortability"; kitendo cha kuingia kitandani na taulo na kushtuka usiku vinanikwaza sana.

Sasa madaktari humu mnisaidie ni nini laweza kuwa tatizo? Msaada wenu ni muhimu. Huyu daktari wangu ni muelewa sana, naweza shauriana naye kwa kutumia majibu yenu na akayafanyia kazi. Msaada wanajamvi.
Mkuu ulipata ufumbuzi ? maana na mimi ilinitokea kipini nilipoendaga secondary songea toka mwanza,

Baada ya miezi sita nilianza kujisikia baridi ambalo sio la kawaida na nikilala usingizi vivyo hivyo nilishtuka na kuamka nimelowanisha shuka hata nikilala mchana usingizi ukipita tuu nikija kuamka shuka limeloa.
Nilienda kupima malaria amna kitu japo sikupima vipimo vingi ila nikirudi likizo nilikuwa sioni tatitzo. mpaka nilimaliza miaka miwili nikatoka mpaka sasa sijawahi tena kuona hali hiyo.

Leo siku ya kifua kikuu ndo nimesikia dalili zake nikaamua kufuatilia no nmekuta ni moja wapo lakini naona tena ulipima ila lilikuwa sio tatizo.

Saivi naomba ushauri maana nataka nikapime TB lakini tatizo halipo saivi.
 
Mkuu ulipata ufumbuzi ? maana na mimi ilinitokea kipini nilipoendaga secondary songea toka mwanza,

Baada ya miezi sita nilianza kujisikia baridi ambalo sio la kawaida na nikilala usingizi vivyo hivyo nilishtuka na kuamka nimelowanisha shuka hata nikilala mchana usingizi ukipita tuu nikija kuamka shuka limeloa.
Nilienda kupima malaria amna kitu japo sikupima vipimo vingi ila nikirudi likizo nilikuwa sioni tatitzo. mpaka nilimaliza miaka miwili nikatoka mpaka sasa sijawahi tena kuona hali hiyo.

Leo siku ya kifua kikuu ndo nimesikia dalili zake nikaamua kufuatilia no nmekuta ni moja wapo lakini naona tena ulipima ila lilikuwa sio tatizo.

Saivi naomba ushauri maana nataka nikapime TB lakini tatizo halipo saivi.

Pole Mkuu!
Nashukuru mimi hii hali iliisha kipindi kilekile cha 2015.
Jambo la muhimu kufahamu ni kuwa kutoka jasho kwa wingi (sio ile hali ya kutoka jasho kwa kawaida) yaweza kuwa ishara ya ugonjwa fulani ama yaweza kuwa ni hali ya mwili unapojaribu kukabiliana na mabadiliko fulani (mf. mazingira; hali ya kifikra kama vile kutingwa sana-too much engagement, msongo sana wa mawazo, "too much excitement", na nyinginezo; nk.). Kwa vile nilikuwa nimeshapima vipimo vingi na hali ikiwa inaendelea, daktari alinikutanisha na mwanasaikolojia hospitalini, ndiyo akaniambia hivyo baada ya mahojiano. Kwa hiyo nilirekebisha kidogo ratiba za siku, na baadaye nikajikuta tu mambo yako sawa. Lakini pamoja na hayo, hatua ya kwanza ya kuchunguza afya kwa kupima ni muhimu. Hata kama hivi unavyosema tatizo halipo tena, vile umepata nafasi ya kupima TB sidhani kama una sababu ya kujiuliza. Unapopata nafasi ya kuchunguza afya, nashauri uone kama fursa. Ahsante
 
Back
Top Bottom