Iwe
kujitumia;kutumika au kutumiwa,wawili hawa wamekuwa 'lulu' kwa wapinzani
wa CHADEMA. Wawili hawa wamekuwa wakitumika kuchora picha ya kwamba
CHADEMA ina mgogoro na si chama cha kukiamini. Imekuwa ikichorwa picha
yao ya kwenda kinyume na chama chao,hasa maamuzi na misimamo ya chama
kwakuwa eti CHADEMA 'hakuna amani'. Propaganda zimekuwa zikijengwa juu
ya
Zitto na Shibuda. Wengine ni wafuasi wa hawa
tu.
Sijui kwanini watunzi wa propaganda hizi hawabadiliki.Hawabadilishi
namna ya kuwatumia watu hawa. Watanzania wa sasa hawadanganyiki.
Wanaelewa vyema ukweli na uongo. Nani ashindwe kujua uongo suala la
Shibuda kuwa amehama CHADEMA huku akiendelea kujiita na kutajwa kama
Mbunge wa Maswa Magharibi na Mjumbe wa Bunge la Katiba? Ingewezekanaje
kisheria kuhama chama na kubaki kuwa Mbunge?
Hatahivyo, propaganda hizi ingawa ni chakavu, zinaiimarisha CHADEMA na
kuifanya idhibiti mianya ya kisaliti chamani.