Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,143
Iwe kujitumia;kutumika au kutumiwa,wawili hawa wamekuwa 'lulu' kwa wapinzani wa CHADEMA. Wawili hawa wamekuwa wakitumika kuchora picha ya kwamba CHADEMA ina mgogoro na si chama cha kukiamini. Imekuwa ikichorwa picha yao ya kwenda kinyume na chama chao,hasa maamuzi na misimamo ya chama kwakuwa eti CHADEMA 'hakuna amani'. Propaganda zimekuwa zikijengwa juu ya Zitto na Shibuda. Wengine ni wafuasi wa hawa tu.
Sijui kwanini watunzi wa propaganda hizi hawabadiliki.Hawabadilishi namna ya kuwatumia watu hawa. Watanzania wa sasa hawadanganyiki. Wanaelewa vyema ukweli na uongo. Nani ashindwe kujua uongo suala la Shibuda kuwa amehama CHADEMA huku akiendelea kujiita na kutajwa kama Mbunge wa Maswa Magharibi na Mjumbe wa Bunge la Katiba? Ingewezekanaje kisheria kuhama chama na kubaki kuwa Mbunge?
Hatahivyo, propaganda hizi ingawa ni chakavu, zinaiimarisha CHADEMA na kuifanya idhibiti mianya ya kisaliti chamani.
Sijui kwanini watunzi wa propaganda hizi hawabadiliki.Hawabadilishi namna ya kuwatumia watu hawa. Watanzania wa sasa hawadanganyiki. Wanaelewa vyema ukweli na uongo. Nani ashindwe kujua uongo suala la Shibuda kuwa amehama CHADEMA huku akiendelea kujiita na kutajwa kama Mbunge wa Maswa Magharibi na Mjumbe wa Bunge la Katiba? Ingewezekanaje kisheria kuhama chama na kubaki kuwa Mbunge?
Hatahivyo, propaganda hizi ingawa ni chakavu, zinaiimarisha CHADEMA na kuifanya idhibiti mianya ya kisaliti chamani.
Last edited by a moderator: