Kutoelewana ndani ya mahusiano

Saa ingine kuna kuchokana tu na suluhisho la hilo ni kila mtu kuanza kivyake. Unajua kuwa na mtu huyo huyo day in day out kunachosha? Binadamu tumeumbwa kuwa na matamanio na matamanio yetu hutufanya kuchoka na kutamani vingine.

Kwa mfano, wakati bado mko wapenzi wapya mlikuwa mnapendana sana. Mlikuwa mnakumbukana sana. Mwenzio ndio alikuwa mwanzo na mwisho. Lakini baada ya kuwa pamoja kwa muda, mnaanza kuonana wa kawaida sana. Ule u-special unapungua. Katika muda huu unakuwa tayari unajua ushuzi wa mwenzako unanukaje. Harufu ya mdomo wake ikoje asubuhi akiamka. Unakuwa unajua harufu ya mavi yake. Mwishowe anaanza kukutia kinyaa. Haya yote yanapelekea kuanza kumwona mwenzako kuwa wa kawaida sana na pengine kuanza hata kukuudhi. Na ukishaanza kuudhika basi ujue huo uhusiano umefikia hatua mbaya.
Mahusianio ni mambo magumu sana. Yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu.

Ili kuzuia matatizo ya kutoelewana, dawa kamili ni mapenzi ya kweli. Kama mlikuwa mnapendana kwa dhati, hamtachokana. Watu wanaishi maisha bwana!
 
...kuchokana kupo sana tena, kuna wakati mwingine unamuona mtu unahic kama vile unapita daraja la salender....lol
Baeleze mamaaa!
Akina baba/kaka hudhani wao tu ndio wanawachoka wanawake.....hawajui na sisi twawachoka hivyo hivyo...tena labda kuliko wafikiriavyo au kuliko wanavyotuchoka.Fikiria mtu anayekuudhi kila kukicha -mara kapita kona hii na kimada, mara katembea na mfanya kazi wako wa ndani, mara anatembea na sekretari wake, mara analala na muuza baa, mara anaokota changudoa wanamalizana kwenye gari.Akija home anategemea wewe upo tu unamsubiria kama vile yeye ndo samaki pekee aliyebakia baharini.Binafsi sina nafasi na mwanaume kama huyu.Ikitokea sababu tu ya kusepa atanisikia kwenye radio.Atajuuuuuuta! kumfahamu Queen!
 
Wasuluhishi hawahitajiki zaidi ya wawili washitakianao. Nafikiri walengwa ni mke na mume si mtu mwingine.

mahusiano yamenishinda kuelea mpaka leo, ni kitendawili. Ninachoona mimi bora mtu ukae kivyako kuliko kuingia sehemu ambayo utawahi kuchoka au vitimbi vingi ili muachane.

Siku hizi waume kwa wanawake wote tumekuwa vichaa tu hakuna mwenye akili timamu. Mtu akipata ki nyumba kidogo nje anaanzisha tabia ambayo mwenzie hawezi vumilia ili mmoja awe na maamuzi ya kuacha mwenyewe. Hili nalipinga sana kwa sababu unavyoniacha kwa style hiyo make sure mpya hajui akijua anakumwaga kwa style hiyo.

Tujifunze kupendana jamani, tumake difference. Ukiesema bora ukae bila kuolewa au kuoa kwa sababu mnachokana kweli ni makosa anyway sitaki kuhukumu. tufudishane njia za kufanya kuridhishana, maana hata huko unakoenda hujui kama hizo huduma zitadumu au la. Inaniuma sana tunafanya maisha kuwa magumu.
 
Wakuu kuna hiki kitu kimekuwa kikinitatiza saana kujua chanzo halisia cha wanandoa kutoelewana kila kukicha wakati wa uchumba wao walikuwa wanaelewa na walikuwa pamoja kwa kila kitu.


  • Hivi hiki kitu kinatokana na mmoja wa wanandoa kuridhika na hali ya ndoa? au
  • Inatokana na kutikubali kujishusha hata kama amekosea ila atalazimikia kuawa juu wa wababa? au
  • Inatokana na watu kutokubaliana kumaliza tofauti zao pindi zitokeapo na kualika watu wa njee ili waje kuzimaliza kana kwamba ndoa ya watu wawili ni ndoa ya jamii?au
  • Inatokana na mmoja wao kutokubali kubadilika na hali halisia ya ndoa kuwa kila kitu kina kuwa kimoja badala yake kila mmoja anaendelea kukumbatia tabia aliyokuwa nayo kipindi cha uhuru wake kabla ya kuoa au kuolewa?
Na je pindi tatizo ndani ya ndoa litokeapo ni nani hasa anastahili kuja kutatua na kupatanisha toafuati zilizopo?


  • Je ni wapambe wa harusi?
  • Je ni wazazi wa pande zote mbili?
  • Je ni marafiki wa karibu hata wale ambao hawajaoa japo ni marafiki?
  • Je ni washenga ?
Nisaidie tafadhali

...ndoa ni kama kiatu tu, kikikubana au kukupwaya weye ndiye mvaaji. Kiatu kinastiri siri ya mguu, hata kama umeking'arisha na polish ilhali soksi ndani imetoboka, wewe ndiye mwenye mwamuzi..

Kutafutana shari au amani ndani ya ndoa ni chaguo lako wewe (mvaaji). Hakuna mpatanishi wala msuluhishi atayewapatanisha iwapo mwenyewe 'hutaki!'
 
Back
Top Bottom