Kutoana kafara kwenye familia, na Siri ya wazazi wetu

Kutoana kafara kwenye familia, na Siri ya wazazi wetu

Jack Daniel

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2021
Posts
4,042
Reaction score
16,872
Habari za mchana.

Hii nimeitoa kwenye familia moja kanda ya ziwa.

Hivi ulishawahi kuona familia fulani ina watoto wengi lakini mmoja haolewi,au haoi na akioa anaacha ndoa haidumu.

Au kama ni mwanamke anaachika ili tu arudi Kwa wazazi?

Unakuta kijana anapambana lakini hatulii,anajikuta anaacha nyumba yake na kurudi Kwa wazazi?

Au binti anazalishwa mpaka watoto wanne na wanaume tofauti lakini ndoa zake zote hazidumu?

Hebu fuatilia kisa hiki cha mwanaume wa miaka 40,akinisimulia kisa chake baada ya kusoma mikasa yangu hapa Jamii forum.............

Naitwa Moses (siyo jina halisi) nimezaliwa moja ya mkoa maarufu kanda ya ziwa,nimezaliwa mwaka 1985 katika familia ya watoto wanane,watano wakiwa wa kiume na watatu ni wa kike. Huku Mimi nikiwa ni mtoto wa mwisho kuzaliwa.

Nilibahatika kumaliza shule ya msingi mwaka 2001 ,huku nikifaulu vizuri Sana kiasi cha wazazi wangu pamoja na Kaka na dada zangu kunisaidia ili niendelee na masomo ya pili ,nilisoma hadi kidato cha nne nikashindwa kufaulu vizuri kwenda advance hivyo nikarudi nyumbani nikajiunga na moja ya Kaka zangu kwenye biashara yake ya samaki.

Kifupi nimedumu kwenye biashara hiyo miaka mingi nikiwa na Mtaji wangu,hadi kufikia hatua ya kujenga kibanda changu (nyumba) hatua ambayo iliniweka kwenye mazingira mazuri kwani niliaminiwa,nilipendwa kijijini kwetu,lakini hata wanawake walinipenda nadhani ni kwasababu ya maendeleo niliyokuwa nayo.

Na ilipofika mwaka 2012 niliweza kutangaza ndoa na moja ya mchumba wangu wa muda mrefu Aitwaye zawadi, taratibu za kuoana zilifuata na ndoa ikapata baraka Kwa wazazi wote wanne.

Zawadi ni mwanamke ambaye tulipendana sana,Kwanza tulifanana vitu vingi ikiwemo wote kuwa ni malast born,hii ni moja cha pili familia Yao nao wapo wengi kama Sisi huku wao wakiwa tisa na mwanaume ni mmoja tu ya Yule first born ,waliofuata wote ni jinsia Ke.

Lingine ni heshima na maadili ya familia ile kuanzia dada zake namna wote walivyotulia kwenye ndoa zao lakini pia namna walivyo wazuri,zawadi ni moja ya wanawake weupe na Mimi mtu mweupe mrefu ulikuwa ni ugonjwa wangu kiukweli.
anasimulia Moses.

Mimi: siyo wewe tu Mimi mwenyewe Kwa mwanamke mweupe sipindui meza na nikiwekewa mtego ni rahisi kunasa (tunapeana tano na kucheka)

Moses:Ni kweli bro lakini sisi kabila letu tumezidi,yaani tangu zamani mwanamke mweupe alipewa thamani kubwa.(Huku akicheka zaidi)

Mimi:hebu nambie maisha yalikuwaje baada ya kuoana.

Anaendelea kusimulia..................

Bro we acha tu,Kwanza maisha yalianza vizuri kama tupo kwenye beach ya kimataifa vyakula vizuri,pesa nilizochangiwa,zilitosha Mimi kukaa mwezi mzima bila kujihusisha na kazi yeyote,fungate ilikuwa fungate kweli .

Na baada ya miezi minne ya ndoa yetu mke wangu kipenzi ilionekana ana ujauzito,hili lilinifurahisha sana pamoja na yeye mwenyewe alifurahi mno muda mwingi tuliangaliana na kutabasamu,licha ya ujauzito wake bado alifanya kazi Kwa bidii pamoja na kunionesha kunijali kama mume,nilipotoka kazini alinipokea Kwa shangwe,alinipa pole alinihurumia lakini niendapo kazini hakusita kunihusia kuwa makini.

Nilivimba nilijiona mwanaume mwenye bahati kana kwamba hakuna mwanaume mwingine aliwahi kuoa.
Hata baadhi ya washikaji walinionea wivu kimtindo hakika nilikuwa mfano wa kuigwa kama mtu anayeifaidi ndoa yake.lakini baada ya muda fulani mimba ilivyokuwa kubwa mke wangu alianza kubadilika, uvivu,kunijibu akijisikia,kutokuwajibika kwenye majukumu yake ndani ya familia pamoja na hujiamini,yaani ule uoga ulimtoka aliweza nijibu atakavyo.
anaweka kituo moses

Inaendelea........👇
 
Habari za mchana.

Hii nimeitoa kwenye familia moja kanda ya ziwa.

Hivi ulishawahi kuona familia fulani ina watoto wengi lakini mmoja haolewi,au haoi na akioa anaacha ndoa haidumu.

Au kama ni mwanamke anaachika ili tu arudi Kwa wazazi?

Unakuta kijana anapambana lakini hatulii,anajikuta anaacha nyumba yake na kurudi Kwa wazazi?

Au binti anazalishwa mpaka watoto wanne na wanaume tofauti lakini ndoa zake zote hazidumu?

Hebu fuatilia kisa hiki cha mwanaume wa miaka 40,akinisimulia kisa chake baada ya kusoma mikasa yangu hapa Jamii forum.............

Naitwa Moses (siyo jina halisi) nimezaliwa moja ya mkoa maarufu kanda ya ziwa,nimezaliwa mwaka 1985 katika familia ya watoto wanane,watano wakiwa wa kiume na watatu ni wa kike. Huku Mimi nikiwa ni mtoto wa mwisho kuzaliwa.

Nilibahatika kumaliza shule ya msingi mwaka 2001 ,huku nikifaulu vizuri Sana kiasi cha wazazi wangu pamoja na Kaka na dada zangu kunisaidia ili niendelee na masomo ya pili ,nilisoma hadi kidato cha nne nikashindwa kufaulu vizuri kwenda advance hivyo nikarudi nyumbani nikajiunga na moja ya Kaka zangu kwenye biashara yake ya samaki.

Kifupi nimedumu kwenye biashara hiyo miaka mingi nikiwa na Mtaji wangu,hadi kufikia hatua ya kujenga kibanda changu (nyumba) hatua ambayo iliniweka kwenye mazingira mazuri kwani niliaminiwa,nilipendwa kijijini kwetu,lakini hata wanawake walinipenda nadhani ni kwasababu ya maendeleo niliyokuwa nayo.

Na ilipofika mwaka 2012 niliweza kutangaza ndoa na moja ya mchumba wangu wa muda mrefu Aitwaye zawadi, taratibu za kuoana zilifuata na ndoa ikapata baraka Kwa wazazi wote wanne.

Zawadi ni mwanamke ambaye tulipendana sana,Kwanza tulifanana vitu vingi ikiwemo wote kuwa ni malast born,hii ni moja cha pili familia Yao nao wapo wengi kama Sisi huku wao wakiwa tisa na mwanaume ni mmoja tu ya Yule first born ,waliofuata wote ni jinsia Ke.

Lingine ni heshima na maadili ya familia ile kuanzia dada zake namna wote walivyotulia kwenye ndoa zao lakini pia namna walivyo wazuri,zawadi ni moja ya wanawake weupe na Mimi mtu mweupe mrefu ulikuwa ni ugonjwa wangu kiukweli.
anasimulia Moses.

Mimi: siyo wewe tu Mimi mwenyewe Kwa mwanamke mweupe sipindui meza na nikiwekewa mtego ni rahisi kunasa (tunapeana tano na kucheka)

Moses:Ni kweli bro lakini sisi kabila letu tumezidi,yaani tangu zamani mwanamke mweupe alipewa thamani kubwa.(Huku akicheka zaidi)

Mimi:hebu nambie maisha yalikuwaje baada ya kuoana.

Anaendelea kusimulia..................

Bro we acha tu,Kwanza maisha yalianza vizuri kama tupo kwenye beach ya kimataifa vyakula vizuri,pesa nilizochangiwa,zilitosha Mimi kukaa mwezi mzima bila kujihusisha na kazi yeyote,fungate ilikuwa fungate kweli .

Na baada ya miezi minne ya ndoa yetu mke wangu kipenzi ilionekana ana ujauzito,hili lilinifurahisha sana pamoja na yeye mwenyewe alifurahi mno muda mwingi tuliangaliana na kutabasamu,licha ya ujauzito wake bado alifanya kazi Kwa bidii pamoja na kunionesha kunijali kama mume,nilipotoka kazini alinipokea Kwa shangwe,alinipa pole alinihurumia lakini niendapo kazini hakusita kunihusia kuwa makini.

Nilivimba nilijiona mwanaume mwenye bahati kana kwamba hakuna mwanaume mwingine aliwahi kuoa.
Hata baadhi ya washikaji walinionea wivu kimtindo hakika nilikuwa mfano wa kuigwa kama mtu anayeifaidi ndoa yake.lakini baada ya muda fulani mimba ilivyokuwa kubwa mke wangu alianza kubadilika, uvivu,kunijibu akijisikia,kutokuwajibika kwenye majukumu yake ndani ya familia pamoja na hujiamini,yaani ule uoga ulimtoka aliweza nijibu atakavyo.
anaweka kituo moses

Inaendelea........👇
Sehemu ya pili.

Mimi: Mimi nadhani ni kawaida pindi wake zetu wakiwa kwenye hali hiyo.

Moses: bro ni kweli ila kwangu ni tofauti kidogo,baada ya kuona mke wangu simuelewi nikaamua kuwaeleza mmoja dada zake mmoja ambaye yeye aliolewa hapo hapo kijijini kwetu,hivyo kabla ya kumweleza yeyote niliona yeye ni msaada zaidi.nakumbuka alinijibu sawa,huku akinipa pole na kuniahidi tukutane saa za jioni baada ya kazi kesho yake.

Kweli siku insyofuata kama kawaida jioni dada wa mke wangu alikuja nyumbani Kwangu akiwa na mwanamke mwenzie akimtambulisha kama rafiki yake,tukawa watu wanne,nilieleza matatizo ya mke wangu pamoja na vituko vyake,huku wote wakinisikiliza Kwa makini,baada ya kumaliza maelezo yangu mke wangu aliulizwa ana maana gani kunifanyia Yale yote lakini alikataa akidai tupo sawa , wala hakuna shida yeyote,ni Mimi nimemtafsiri vibaya.

Baada ya hapo dada yake aliniomba nitoke nje waongee watatu,nikafanya hivyo,walitumia kama nusu saa kisha wakatoka na dada mtu akanihakikishia kuwa mambo yale hayatajirudia tena,nilifurahi kimtindo kisha wageni wakaondoka.

Usiku wa siku hiyo haukuwa vizuri ni kama nilizidisha Tatizo badala ya kulitatua,mke wangu alinuna mara kumi zaidi.
Ila nikaacha tu kesho asubuhi kulipokucha nikaenda kwenye mishe zangu, lakini baada ya kurudi jioni sikumkuta,piga simu weeee lakini haikuonesha kupokelewa japo vitu vyote vilikuwepo ila begi lake dogo sikuliona nikathibitisha katoroka,moyo ulianza kuniuma,wivu haukucheza mbali,hasira kidogo zilininyemelea lakini nilitulia nikaenda Kwa mwenyekiti wetu kumpa taarifa za kupotelewa na mke wangu.

Mwenyekiti alishauri tu kuwa ningepiga nyumbani kwetu Kwanza huenda yupo Kwa wazazi wangu,nikaambiwa hayupo ,usiku Kwa usiku nikakodi pikipiki mpaka kwao kwakuwa hapakuzi mile Saba,nilimkuta akiwa na bashasha akipiga stori na mama yake mzazi.

Nilimsalimia mama Mkwe kisha nikakaribishwa ndani,nikamkuta Baba Mkwe nikamsalimia naye huku uso wake ukiongea Jambo.

Enheee baba tumempokea mwenzio tangu asubuhi anadai mna matatizo vipi imekuwaje? aliuliza baba Mkwe.

Ni kweli tulikuwa na matatizo takribani mwezi mzima,lakini Jana nilimuita Shemeji (jina kapuni)alitusuluhisha ila nimeshangaa narudi jioni hii sioni mtu.
Nilijibu.

Baba Mkwe alimuita mke wangu na kumtaka aeleze matatizo yake.

Mke wangu hakuwa na majibu ya kueleweka zaidi ya kujiumauma tu hapo Baba Mkwe alifoka na kumtaka mke wangu arudi nyumbani Kwangu,huku akidai maelezo aliyoambiwa asubuhi yanatofautiana hata hivyo,alikuwa anasubiri maelezo ya pande zote mbili,hata hivyo kashaujua ukweli hivyo mke wangu ainuke tuondoke.

Lakini ghafla aliinuka mama Mkwe na kudai yeye hawezi kuruhusu mwanaye arudi kwangu kwasababu moja Kwa moja inaonesha hatuna maelewano hivyo akaomba mwanaye nimuache Kwanza.

Baba,Mimi ndiye niliyemnyonyesha mkeo zawadi,Mimi mwanangu namfahamu ana hasira na wewe unaonesha Una hasira hivyo kulingana na hali ya tumbo lake nisingependa arudi kwako , kwasababu huyu anahitaji uangalizi,faraja,na mambo mengine yasiyo ya maudhi sasa naomba niachie mwanangu.mama Mkwe alisema.

Baba Mkwe alishindwa kuelewa alimwangalia mkewe ,akamgeukia mwanaye akahisi kuna kitu ,ugomvi ukaanza Baba anasema mwanaye arudi Kwa mumewe ,mama anasema kama alimzaa Kwa uchungu ,hawezi ruhusu mwanaye arudi abadani.

Mimi kuona vile nikaaga nikaondoka Kwa hasira Sana nikajikuta naanza kumchukia mama Mkwe.

Nikiwa njiani nilipokea simu ya mke wangu ,lakini aliyeongea ni mama Mkwe.

Baba Kwanza usijisikie vibaya na nadhani unaijua Hali ya mkeo vizuri Sana cha kufanya wewe tulia mwanangu huyu ni mkeo,Mimi nawaona wote mna hasira hivyo wewe katulie na mwenzako akiwa sawa atarudi.aliongea mama Mkwe huku Mimi nikiwa sijatia neno.

Inaendelea......
 
Shida sio kafara shida ni wanaokuzunguka kwenye ukoo na watu wako wa karibu.
Kuna jamaa yetu alizaa nchi za nje na hakutaka watu wake tanzania tufahamu hata yoyote wala ndugu.ila alijaribu kuzaa hapa tz na ndugu wakafahamu yani mtoto ni wa tz ni kama tabia za Tlaatlaah
 
Sehemu ya tatu.

Nilifika nyumbani nikiwa nina Mawazo kiasi,niliona wazi baba Mkwe yupo upande wangu ila mama Mkwe alikuwa upande wa binti yake.

Nililala huku nikizima simu nisisumbuliwe na yeyote,huku nikiwaza na kuwazua meeeengi Sana,moyo kulipuka Kwa wivu haukuacha,ila nilijipa moyo kwamba mke wangu na ujauzito wake wa miezi kadhaa hawezi kuwa na mwanaume mwingine,japokuwa inawezekana.asubuhi na mapema niliamka nikaiwasha simu yangu huku nikipiga Kwa wazazi wangu niwaeleze mkasa mzima ilikuwaje.

Wazazi wangu hawakutaka masuala yake tuongee kwenye simu badala yake wakanitaka nifike kabisa,ili tujue mbivu na mbichi.

Mwananguuuu (pole Baba pole sana)najua ni jinsi gani unaumia lakini najua tutayamaliza vipi.

Yalikuwa ni maneno ya mama yangu kipenzi ,nikiwa kama mtoto wa mwisho kwake nilifaidi mapenzi yake ya dhati,nilijua nilivyodekezwa,hata Kaka na dada zangu waliponiambia wazazi wetu walikuwa wakali Mimi nilibisha kwani nililelewa Kwa kudekezwa mno mithili ya mjukuu.

Nakumbuka niliwaeleza wazazi wangu mambo yote tangu visa alivyonifanyia mke wangu siku zote,na Hata nilivyomuita dada yake kuja kusuluhisha,pia alivyoondoka Kwa kutoroka,na aina ya majibu niliyopewa na wazazi wake akiwemo mama Mkwe.

Kwanza wazazi wangu walishangaa Sana lakini walishangaa zaidi mama Mkwe kumkumbatia mke wa mtu ikiwa hakuna ugomvi wowote.tulipata breakfast pale pale Kwa wazazi wangu kisha nikaondoka,huku Mzee wangu wakati tunaondoka akinihusia kwamba nijitahidi kuongea na mke wangu bila kuhitaji wasuluhishi na ikiwa mambo yatakwenda vigumu naweza kuachana naye.
Mzee akaongeza zaidi kwamba mara nyingi mke akianza kukukataa bila ugomvi wowote huwa ni dalili mbaya ,hatua ya kuchukua ni kuachana naye tu.

Maneno ya Mzee yalikuwa kama mwiba kwangu haingekuwa rahisi kuachana na mke wangu kipenzi zawadi,ningeanzaje niliona Mzee wangu hanitakii mema hata kidogo,hata hivyo point pekee niliyoishika kwenye usia wake nikutokuwashirikisha watu wengine kwenye ndoa hata kama ni ndugu.

Kiukweli nilikosa raha masaa yalisogea huku nikiwaza labda mke wangu atanipigia simu lakini haikuwa hivyo,kila nikimuwaza moyo uliniuma nilijaribu kufikiri labda kuna mtu alikuwa akimshawishi mke wangu vibaya sikupata majibu. Baada ya kutafakari Kwa muda mrefu nikakumbuka kuwa mke wangu ana kaugomvi na mwanamke mmoja ,sijawahi kujua chanzo cha ugomvi ila nilijua hawapatani.

Nikaona hii ni kete nzuri,nikamwendea Yule mwanamke na kuomba kuonana naye Sehemu tulivu isiyo na makelele ,tukakubaliana twende kwenye Mgahawa mmoja maarufu Kwa hadhi ya kijiji chetu kwakuwa hakuwa mke wa mtu nilikuwa na Amani huku nikijua Kwa ujirani tulipokuwa nao hakosi kujua habari za mke wangu.lazima nitajua mbivu na mbichi.

Niambie Musa naona umeniita halafu huongei,unajua mkeo yule mkali siku akijua Mimi na wewe tuliwahi kuwa pamoja inaweza kuwa kesi kubwa,na alivyo na wivu sasa.aliongea yule mwanamke.

Kwanza siitwi Musa,my name's Moses,
Najisikia poa nikiitwa
Mozes na siyo Musa.
Nilichokuitia hapa ni kuhusu mke wangu,unajua Mimi na mke wangu hatuna maelewano siku nyingi sana,hata hivyo,ni Jana tu katoroka kaenda kwao hata baada ya kumfuata kagoma kurudi, kiukweli najisikia vibaya sana,na sijui ni wapi nilipokosea na sijui ni. Nani anamrubuni mke wangu.

Sasa nilichokuitia hapa naomba niambie lolote unalojua kuhusu mke wangu nitakulindia siri hii ,na Imani kuna kitu unajua,najua unajua tafadhali chochote unachokifahamu niambie sitasema popote kuwa na amani dada.niliweka kituo huku nikimkazia macho.

(Huku akicheka kicheko hafifu)
Musa bwana,yaani unaona inawezekana kabisa, si bure naona umevurugwa ,yaani ni Nani mwenye akili timamu anaweza kuongelea habari za ndoa ya mtu na mkewe, serious! Acha kunidharau Musa sijui Moses,haya tufanye ni kweli nimekwambia huoni nitakuwa mwenye hatia mno, tafadhali naomba niruhusu niondoke kama huna cha kuniuliza kingine.aliongea akiwa design kama anachukia hivi.

Hapa dadangu nisamehe kama nimekukwaza naomba uketi basi tupate chakula kwani nilishaagiza na kipo tayari .
Niliongea Kwa upole .

Yule dada aliketi huku akiwa anatazama usawa wa jikoni wa mgahawa ule.

Vipi Musa umeagiza nini?nyamachoma?
Nina muda sijaila,wewe acha tu maisha magumu wanaume hakuna,waliokwenye ndoa wanazichezea,kweli kila mtu na chaguo lake,lakini mbona ndoa yenu changa nini kinasababisha haswa mkeo aondoke? na anavyonichukia akisikia nipo na wewe ataniua ngoja nile niondoke Fatuma mie. Dada alikuwa muongeaji Sana.

Vipi kwani wewe na mke wangu mna ugomvi gani mbona huwa hamuelewani,?niliuliza .

Mkeo alinunia tangu alivyoniona kwenye harusi yenu,halafu alivyogundua Mimi nakaa kijiji hiki ndiyo kabisaa akazidi kuninunia.aliweka kituo

Kwani mnafahamiana, niliuliza Kwa shauku.

Yule ni classmate wangu na Nina Siri yake naijua Kati ya yeye na mama yake,na wote si mkeo si mama mkweo wote wananichukia.
aliweka kituo dada Fetty huku nikiwa na shauku ya kutaka kujua kuna Siri gani Kati ya mke wangu na mama yake.nikawa na hamu kujua.

Inaendelea.........................
 
Sehemu ya nne

Mimi na rafiki Moses ambaye awamu hii amekuwa ni mwenyeji wangu na mtu mkarimu Sana asiye muongeaji,kila siku anakuja nilipo tunapiga stori kisha anaondoka tunaitana bro,kwakuwa hakuna anayejua umri wa mwenzake.

Lakini baadaye nagundua kiumri nimemzidi miaka mingi sana haswa baada kunieleza kisa fulani..

Sasa endelea.................

Wanaume ni watu mnafaidi sana yaani nyama ni tamu balaa,samahani naomba nichukulie safari lager hata Mimi swahiba wangu.aliongea Fetty huku akiangalia chini Kwa aibu ya kike.

Siyo mbili tu mwambie akupe bia unazoona zifakutosha kuwa na Amani,lakini hujaniambia Siri ya mke wangu na mama yake.niliropoka.

Musaaaa aaah khaah mwanaume wewe umepagaaaawa,Kwanza nakutania huwa situmii pombe lakini kuhusu mkeo na mama yake sina taarifa za kiundani kiviiiile ,ila najua mkeo anapendwa sana na mama yake.kwanini nasema hivyo.

Kipindi tunasoma mama zawadi alikuwa anapenda Sana kuja shule kuulizia maendeleo ya mwanaye,baadhi ya walimu walidhani ni Bibi yake kwani umri ulikuwa umeenda hata alipowaambia yeye ni mzazi wake baadhi ya walimu walikubali kishingo upande,ila walimsifu Sana mzazi kuja shule kuulizia matokeo ya mwanaye ,walidai ni mfano wa kuigwa,lakini kadri siku zilivyosogea ikawa kama kero Kwa walimu,wapo waliodai Bibi anazeeka vibaya.

Fatuma Mimi nikiwa kama rafiki wa zawadi na jirani yake niliweza kuuona ukaribu wa kuzidi wa mama na mwana, mwanzoni nilitamani na Mimi ningekuwa na ukaribu wa namna ile ila baadaye nikaona kama rafiki yangu zawadi anabanwa, haiwezekani iwe vile,kubwa zaidi baada ya Sisi kufikia umri wa kufatwa na wanaume kama desturi ilivyo,mama yake zawadi hakupenda,yaani hajawahi kupenda kuona mwanaye anajuhusisha au kuwa karibu na jinsia ya kiume,kwake haikuwezekana .

Baadaye akatokea mchumba aliyekubaliana na zawadi wafunge ndoa , familia nzima jamaa,ndugu, kaka na dada zake walikubali aolewe lakini mama alikataa akidai mwanaye bado mdogo, mwanaume Yule akakata tamaa na kusamehe baadhi ya gharama alizotoa.

Lakini ilitokea pia kazi ya kufanya kwenye moja ya kiwandq kikubwa kwenye mkoa wetu kazi ilihitaji wasichana kumi wanaojua kusoma na kuandika vizuri hivyo mimi na rafiki yangu zawadi tukapata nafasi iliyokuwa na ujira mzuri haswa Kwa siye tusio wasomi na elimu yetu ya kidato cha nne.

Lakini cha ajabu tulipofika kule shoga yangu zawadi hakumaliza wiki moja akarudi kijijini.

Na Mimi mkataba ulipoisha nilirudi nyumbani huku nikiwa na mpango wa kuolewa na mchumba wangu wa miaka mingi, ndoa yangu ikapita huku zawadi akiwa pale Kwa wazazi wake,akiwa hajaposwa wala hana mwanaume,
Mara kadhaa alinieleza kuhusu matamanio yake ya ndoa kwakuwa umri unaenda lakini kutoka nyumbani amuache mama yake alihisi haiwezekani kabisa.

Lakini miaka miwili baadaye zawadi alipata mchumba Kwa mara ya pili akaolewa Kwa sherehe nzuri na yenye kila sababu ya kuitwa ndoa ya gharama,hata Mimi fatuma mie nilimuonea wivu shogaangu Kwa kuolewa na mtu mwenye pesa tajiri wa madini.
anaweka kituo Fetty.

Wakati huo nilikuwa natetemeka huku hasira zikiwa karibu baada ya kusikia kumbe Zawadi mke wangu kipenzi alishawahi kuolewa ,tena ni mara mbili ,yaani Mimi ni watatu lakini mbona sijawahi kuambiwa,yote haya,hebu niambie da Fetty hana mtoto Yule kweli mbona nahisi kuna mengi siyajui? niliuliza

Hapana,sikiliza Musa,
Baada ya kuolewa walihamia Dar es salaam na mume wake lakini huwezi amini baada ya miezi miwili zawadi alirudi akidai ndoa imemshinda,anajikuta hampendi yule mwanaume Jambo lililopelekea watu waanze kuihisi familia yake vibaya haswa mama yake mzazi.

Baadhi ya watu walianza kumtenga zawadi kwani walihisi yeye na mama yake ni wachawi,hata Mimi nilianza kupunguza mazoea naye kwani nilihisi yeye na mama yake siyo watu wa kawaida.

Baada ya zawadi kujua kuwa namkwepa aliniambia ukweli kuwa nishike hamsini zangu,na Mimi sikuwa nyuma nikamwambia alichelewa kuniambia tu ,hata hivyo sihitaji mtu asiyejulikana ni binadamu au jini.hicho ndicho chanzo cha ugomvi Kati ya Mimi na zawadi.
aliweka kituo Fetty.

Sasa wewe uliwezaje kuja hapa kijijini kwetu.anauliza moses.

Nilifiwa na mume wangu hivyo nikaamua kuja kufanya biashara ndogo ndogo huku kwani kuna fursa nyingi,sasa nikashangaa shoga yangu anaolewa na wewe ,nikaamua kuja kwenye harusi yenu na aliponiona nilitambua hakupenda na hajawahi kunikubali hata kidogo.
alipigilia msumari Fatuma.

Niliinuka na kumuacha Fatuma huku nikiondoka bila kulipa bills nayodaiwa nikiwa nimechanganyikiwa Kwa mengi,Kwanza habari za uchawi wa mama Mkwe,uongo wa mke wangu,lakini hata hivyo mke wangu zawadi nilimpenda Sana aliyoniambia fatuma yalikuwa mwiba kwangu.

Itaendeleaaa.....
 
Back
Top Bottom