Wakuu kwema? Nadhan mmeshasikia sana kuhusu mali zilizoachwa na wajerumani kipindi cha zamani, sasa kuna nyumba moja iko tanga ilikuwa inakaliwa na wajeruman na kwa sasa inamilikiwa na mtz, nyumba hiyo ina viashiria vyote vinavyoonyesha kuna mali ziliachwa ( ), mwenye nyumba anatafuta mtu ambaye atakuwa na uwezo wa kutoa hizo mali.
So if u knw anyone tutafutane
KUKU KUCHI NA MALI ZA KALE ZA MJERUMANI.
Uhusiano kati ya Mali za Mjerumani na Biashara ya Kuchi.
Watu wengi wamejikuta wanafilisika kutafuta mali za mjerumani mara birika mara pasi mara sijui sarafu ya mjerumani. Haya mambo yamekuwa yakivuta watu wengi kuingia kutafuta Mali za mjerumani.
UKWELI ULIVYO
Hakuna demand ya pasi wala birika la mjerumani kokote kule duniani.
I
Utapeli hui ulianza miaka mingi sana sasa hata baada ya matapeli kuacha muendelezo umekuwepo.
Matapeli walikuwa wana create Demand wao wenyewe kwa njia hii.
Tapeli anakuja kijijini au town anakuambia kuna wazungu wanatafuta birika la.mjerumani au pasi ya mjerumani au mali yoyote ile na watakuambia inatafutwa Nairobi au kokote kule na watatangaza Dau kubwa sana watakuambia hata Millioni 200 wewe utahamaki na utaanza kujiuliza utaipata wapi? WAO WATAONDOKA
WATATUMA MWENZAO TOFAUTI KABISA atafika mtaani atasema anasikia kuna Passi ya Mjerumani iko hata Songea au Lushoto na kuna mzee anayo atatoa link kwamba wanasikia kijiji fulani au eneo fulani kuna mtu analo hilo birika,
Wewe utaanza safari ya kutafuta hiyo Mali na utafika sehemu ulio elekezwa kwamba ipo. Ukifika kweli utaikuta na mwenye nayo atakuambia anauza kwa bei kadhaa hatataja kubwa sana kama jamaa waliokuambia milioni 200 jamaa anaweza kukuambia anauza kwa milioini 15.
Hapo utaona umasikini umeisha. Utatafuta pesa hata ikibidi kuuza shamba na nyumba na utanunua hiyo mali, Sasa kimbembe ni kuiuza, hao wanunuzi hutawaona wala kuwasikia tena, na unabakia na mali ya mjerumani.SO ALIE KUUZIA NA ALIE KUAMBIA INATAFUTWA SANA, WOTE NI KITU KIMOJA Jamaa walifanya utapeli kwa muda mrefu na wengi wamefilisika bila kujua watu wameishia hadi kwenda kwa waganga wakitafuta hiyo Mali
SASA NA WEWE UTATAFUTA WATU WA KUWAKAMATISHA HIYO PASS YA MJERUMANI.
KUCHI
Demand ya kuchi haipo na haina uhalisia,ni sawa kabisa na mchezo wa Mali za Mjerumani, mtu anaye fuga kuchi ukimuuliza atakuambia wana soko Uarabuni, Mara Pemba wanahitajika sana mara Kuna Waarabu Mombasa wananunua, ila yeye halijui hilo soko, so imejengeka hivyo hivyo kwamba kuna soko la kuchi mara Waarabu wanawataka kuchi,
Wengi hatujui huu mchezo wa kuchi tumekuwa tunauziwa bei za juu mno na anaye nununu ukimuuliza atakuambia anasikia yaani ni mwendo wa kusikia tu, ni fulu kusikia mara nimeambiwa mara wanasoko kubwa sana il halijui
SOKO KWA SASA
Kwa sasa kuna soko la Farmer to Farmer na hii ni sawa na ilivyo kuwa soko la kware na ni sawa na soko la Sungura pia, kila anaye nunua Kuchi anaenda kufuga ukimuuliza atakuambia kuchi wana soko,kuchi wana bei kubwa.
Sasa mwenye ushahidi wa soko aweke hapa, alie wahi ku export Kuchi aweke coppy za Export permit make huwezi export live animal bila kibali haipogo hiyo.
Na Kuchi hata Kenya wapo ila hawana hizo bei za huku Bongo na Kenya hakuna story za waarabu kuwanunua, why Waarabu watake tu kuchi wa Tanzania?
Kuchi ni sawa na Mali za Mjerumani ni watu walikaa chini wakatengeneza Demand ili wapige pesa, sasa muendelezo unaendelea na wengine wanaingia kingi bila kujua mchezo.
Mwenye ushahidi wa Waarabu kununua kwa hizo bei aweke hapa ushahidi sio wa maneno bali mtu a prove beyond dought.
HAKUNA DEMAND YA KUCHI ILA NI WATU WANA CREATE DEMAND WAPIGE PESA HATA KAMA UTAPELI ORIJINO ULIISHA ILA MWANGWI UNAENDELEA HADI SASA.
Anaye Jua Ukumbi wanako piganisha kuchi atuelekeze tukaingie tuona au ni siri? Kama ni siri yeye alijua vipi?
Kitu watu wasicho jua ni kwamba Kuchi hawapo Tanzania pekee wapo malawi wapo Zambia wapo Zimbabwe wapo Botswana na wapo Kenya ila hizo story hazipo huko.
g4cool Nazani umepata jibu sasa.