Habari wapendwa,
Hivi inawezekekana kuvunja uchumba kwa mchumba ambaye umemtolea barua ya uchumba? Kama jibu ni ndio, upi ni utaratibu wa kufuata?
Nimekuwa kwenye mahusiano na binti mmoja kwa miaka mitatu na tumefanikiwa kupata mtoto mmoja.
Miaka miwili iliyopita nilimtolea barua ya uchumba na ikajibiwa ila kwa kweli kwa sasa nimekosa kabisa hisia naye na naona ni bora kila mtu achukue ustaarabu wake kuliko kuendelea kupotezeana muda.
Naombeni ushauri nini nifanye kwa maslahi ya pande zote?
Sent using
Jamii Forums mobile app