Kutengua barua ya uchumba

Kutengua barua ya uchumba

Umri ni miaka 30 wake 24.
UMRI WAKE UNAFAA KUOLEWA, MNAENDANA

1. Nilimpenda kwa hisia kabisaaa but sasa imekuwa tuko kwa mazoea tu ule msukumo wa mapenzi kutoka ndani umekata kabisa.
SABABU ZA KUISHIWA HISIA NI NYINGI, KWANZA UMESHAMJUA SANA, MNA MTOTO PIA ANAYEGAWA MAPENZI YENU. KWA HIYO HII SI SABABU YA KUMWACHA . NDOA NYINGI TUNAISHI VIZURI TUU KWA AKILI, NA SIO HISIA . . KWA KUWA BAADA YA KUONA, MKAZAA NA KUONGEZA MAJUKUMU, LAZIMA MABADILIKO YA KIHISIA YATOKEE . . BADO ANAFAA KUWA MKE . .


2.Naweza sema vimepungua cse mahitaji na nyakati haviko sambamba. Matarajio yangu kwake ni kama hayapo maana ujuavyo mke au mume anatakiwa kuwa multipurpose maana ndoa ni zaidi ya kuwa watoto na kulala pamoja.

WEWE INAELEKEA HUJUI MAJUKUMU YA MUME, NDIO MAANA UNATAKA MKE MULTIPURPOSE . . KWANZA UNAISHI NAE KIMAKOSA KABISA, HUJAFUNDISHWA MAANA YA NDOA NA MAJUKUMU YAKO, WEWE UNAISHI KWA HISIA TUU . . INAELEKEA UNATAKA KUTUNZWA NA MKE, KUMBE WEWE NDIE UNATAKIWA KUMTUNZA MKE WAKO NA WATOTO WAKO. UNATAKIWA KUMFUNDISHA YOTE JINSI UNAVYOTAKA AWE, SIO KUMKIMBIA . . OMBA USHAURI ZAIDI KWA WATU WAZIMA WENYE NDOA ZAO IMARA KABLA HUJAMWACHA, MIMI SIONI KOSA LAKE . .

3.Nadhani natakiwakiwa kuwa selective zaidi kupata yule ambaye ataweza kuwa multipurpose kwa angalau hata 75% ili nami niweze kufurahia mahusiano kuliko ilivyo sasa maana najikuta kama nipo mwenyewe kuanzia ushauri, financially na mengineyo na imefikia wakati naona ni bora kuwa single kuliko kuonekana upo na mtu kwenye macho ya watu wakati nafsi ipo single.
TATIZO UNALO WEWE, HUYO BINTI KAMA AMEWEZA KUKUPIKIA, KUKUFULIA, KUKUTUNZIA MTOTO, KUBEBA MADHAIFU YAKO, KUISHI NA WEWE AKIPENDA NDUGU ZAKO, BASI ANAFAA KUWA MKE.
JICHUNGUZE WEWE ZAIDI KAMA UNAFAA KUWA MUME NA BABA BORA . .

4. Mtoto ni wangu. Naamini naweza pata kitu kizuri zaidi na mtoto tayari ninaye. Usalama naona utakuwepo maana hata kama sitapata kizuri zaidi lkn nitakuwa single na furaha kuliko kuendelea na hii unhappy relationship.
MLIFANYA MAKOSA KUISHI PAMOJA KABLA YA KUONA, NYIE NI MKE NA MUME SIO WACHUMBA TENA . . UNGEOA RASMI, USINGEKUJA HAPA NA HADITHI ZA HISIA . . KUOA NI KAZI YA WANAUME, SIO WAVULANA . .
WEWE NI SELFISH MAN . . HUYO MWANAMKE ANAFAA KUWA MKE, SIJAONA SABABU YOYOTE YA MAANA ULIYOTAJA INAYO M DISQUALIFY KUWA MKE WAKO

5. Sihisi kushindwa kummudu ila ninaona kuendelea naye ni kuja kukosa ile support ya mke ambayo mimi naitarajia kutoka kwake kwani naanza kuyaona hayo mapema.

6.Bado sijazunguza naye kuhusu kuachana na bado napata wakati mgumu kulieleza hilo kutokana na sababu nilizozieleza kwenye mada. But yeye pia ameanza kuona tofauti kwangu maana ki ukweli nimepoteza furaha kabisa kwenye hii relationship.

Ushauri wako tafadhali.

ANGALIE USIJE KUJUTA KIJANA, HAKUNA MKE MALAIKA HUKO UNAKOTAKA KWENDA KUCHAGUA MKE MWINGINE. PIMA RISK YA UNALOTAKA KUFANYA, JICHUNGUZE WEWE ZAIDI KAMA UNAFAA KUWA MUME NA BABA BORA, HALAFU PATA USHAURI TOKA KWA WATUMISHI WA MUNGU.
ACHA KUISHI KWA HISIA, ANZA KUISHI SASA . . , LIFE IS REAL !


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chozi la huyo mwanamke halitakuacha salama milele na milele mpaka unakuta.
Tusione vichaa wengi barabarani, wengine mnajitakia

Ujana haubagui.
 
Unachokisema ni kweli. Shida inakuja family yake watanichukuliaje na barua nilishatoa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Aidha bado wewe ni mvulana au hujielewi. Katika ndoa hakuna mapenzi bali mazoea na kuvumiliana. Lazima ujitahidi kulazimisha kumpenda la sivyo usioe uwe na gf miaka yote. Binadamu tumeumbwa kukinai ila ukiamua kuoa hakikisha kila wakati umuone ndiye mrembo kuliko mwanamke yeyote ulimwenguni. Vumilia usimuache wote wapo hivyo
 
hivi una uhakika gani huyo mwingine utakayempata utakuwa na hisia nae milele. angalia wapi palipo na mapungufu na mrekebishe kwa kushirikiana. Pia jitahidi kuongeza spices kwenye mapenzi yenu outing, shopping, kupika na kufanya usafi pamoja, utani wa hapa na pale.
Usisahau siku mojamoja kujitoa ufahamu kwa kumpigia simu na kumtongoza upya.
 
Chozi la huyo mwanamke halitakuacha salama milele na milele mpaka unakuta.
Tusione vichaa wengi barabarani, wengine mnajitakia

Ujana haubagui.

Hapa nd nachokaga na wanawake, mnapenda kuolewa lakini hamjiongezi hata chembe. Unakuta huyo mtu umemtolea barua kama mdau hapo juu na umezaa naye lakini hana support na wewe hata ukimpigia simu usiku kwamba unaumwa haonyeshi kujari wala hana muda. Kuna siku moja niliwai kumpima wangu kwa kumwambia nahitaji elfu 50 urgently alinikwepa kwepa zen huyo nd unataka uingie naye mkataba kulala uchi maisha.

Kuna mabinti wazuri sema wengi wenu vuvuzela sana na hampendi wazazi wa upande wa kiume hasa mkigundua au kuona familia hiyo ni fukara au inamaisha standard. Mimi namsupport mdau hapo mtu anahitaji ndoa kama hataki vile kisa ushazaa naye.
 
Wanawake na nyie mshtuke jamani miaka 3 hujaolewa upo ndani kila siku unalala bila chu.pi bwana katoa barua ya uchumba tu umesharidhika
 
Kama mwanamke simtaki huwa namwambia tu....bora uonekane mbaya kuliko kumpotezea muda mtu.



Huwa nkishakwambia ukweli nakata mawasiliano ili upate reality sio leo tunaachana kesho tunaanza kuchat sijui kupigiana cmu
Being honest is nice bro.i like no strings attached relationship
 
Jambo la kwanza si kwamba huna hisia naye ila hamfanyi nyinyi wenyewe muwe na hisia kwa mwenzake,


Pili umeshamzalisha halafu unakimbia huo ni udhalimu, kama mpaka barua ya uchumba ulitoa alikuamini,


Tatu hautapata wa tofauti maana hata huyo anayekuvutia sasa kuna mtu yupo nyuma yake anayemfanya akuvutie


Utakayempata mpya baada ya muda pia naye atakuwa hivyo hivyo nawaonea huruma wadada wanaoangukia mikononi mwako.

Nothing straight from crooked timber of humanity can be done
 
Mkuu we ni zaidi ya mse.ngerema .. mbinafsi unaangalia nyege zako kuliko hata hicho kiumbe ulicholeta duniani eti hisia mtoto wako upo radhi aishi maisha ya mzazi mmoja na Mungu naomba wanaume kama hawa wape wake wa kafanana nao wanyanyasaji wabinafsi .. na naenda kutoa sadaka kwa hili hutakaa upate amani
 
Mkuu we ni zaidi ya mse.ngerema .. mbinafsi unaangalia nyege zako kuliko hata hicho kiumbe ulicholeta duniani eti hisia mtoto wako upo radhi aishi maisha ya mzazi mmoja na Mungu naomba wanaume kama hawa wape wake wa kafanana nao wanyanyasaji wabinafsi .. na naenda kutoa sadaka kwa hili hutakaa upate amani

Huwa hawapatagi amani kabisa. Nina mfano hai, jamaa aliacha mwanamke aliyeishi nae na kumzalisha. Akaenda akaoa tena kwa ndoa. Baada ya miezi kadhaa akaanza kurudi kwa baby mama wake . Alichokitarajia kwenye ndoa mpya hakukipata. Akamkumbuka zilipendwa wake. Huyu mleta mada mwache aende akaoe upya, atakuja na mrejesho wa kuteseka ndoani. Machozi ya mwanamke hayajawahi kumuacha mwanaume salama.
 
Back
Top Bottom