Valentina
R I P
- Oct 12, 2013
- 24,688
- 28,834
Wapendwa ni matumaini yangu mpo wazima na mko vizuri katika majukumu yenu
Leo ninaomba kushare nanyi jambo ambalo limekua likinitatiza kwa muda sasa. Ninatambua kila mmoja wetu ana historia yake ya kimapenzi na wengi tumetendwa na wale ambao tuliwekeza mioyo yetu kwao kwa kuwaamini kwamba wataiendeleza furaha yetu, ila kwasababu mbalimbali au kwa bahati mbaya wengi hatukuweza kufikia matarajio yetu juu ya hao wenzetu.
Binafsi nilikua katika mahusiano na mtu ambae nilimpenda mno narudia tena nilimpenda tena mno. Na ndie mwanaume wangu wa kwanza kukutana nae kimwili.
Naye kwa upande wake alionyesha uaminifu na moyo wakujali,maneno yote mazuri yenye matumaini mtoto wa kike niliambiwa, kifupi tulipanga uhusiano wetu uzae ndoa.
Ilifika hatua mwezi wa sita mwaka jana akaja Arusha kwalengo la kujitambulisha nyumbani kwetu. Lakini ghafla katika hali ambayo sikuitarajia akabadilisha maamuzi yake akanipa visingizio.
Baada ya muda mfupi kabla ya yeye kurejea kwenye makazi yake, nikamfumania akiwa na rafiki yangu wa karibu, rafiki niliye mchukulia kama ndugu yangu na kushare nae baadhi ya mambo.
Waliosalitiwa bila shaka wanaelewa uzito wa maumivu hayo. Ikabidi niwe mpole,na kuwaambia waendelee mbele,siku zilivosonga yule binti akaanza mambo ya dharau kwangu ila namshkuru Mungu nilipata moyo wa kumsamehe na kupuuza dharau zake.
Ilipofika mwezi wa 9 yule binti aliacha kazi kwa shari na kurudi kwao.
Sasa kilichonifanya nije hapa mbele yenu leo, nikwamba yule mwanaume anataka kurudi kwangu na mimi moyo wangu unakua mzito kumrudia, nimetokea kumchukia.
Jambo linalonisumbua zaidi kila ninapoanza mahusiano mapya hua nashindwa kuendelea mbele, hofu ya kwamba huyu atanifanyia kama yule inanijia mara kwa mara na matokeo yake nakua sababu ya kuvunjika uhusiano huo.
Wapendwa nifanye nini kukabiliana na hali hii ya pili? Ninatamani sana hali hii iniondoke. Karibu kwa mchango wako kimawazo.
Kwenye makosa ya kiuandishi mnisamehe maana natumia simu.
Leo ninaomba kushare nanyi jambo ambalo limekua likinitatiza kwa muda sasa. Ninatambua kila mmoja wetu ana historia yake ya kimapenzi na wengi tumetendwa na wale ambao tuliwekeza mioyo yetu kwao kwa kuwaamini kwamba wataiendeleza furaha yetu, ila kwasababu mbalimbali au kwa bahati mbaya wengi hatukuweza kufikia matarajio yetu juu ya hao wenzetu.
Binafsi nilikua katika mahusiano na mtu ambae nilimpenda mno narudia tena nilimpenda tena mno. Na ndie mwanaume wangu wa kwanza kukutana nae kimwili.
Naye kwa upande wake alionyesha uaminifu na moyo wakujali,maneno yote mazuri yenye matumaini mtoto wa kike niliambiwa, kifupi tulipanga uhusiano wetu uzae ndoa.
Ilifika hatua mwezi wa sita mwaka jana akaja Arusha kwalengo la kujitambulisha nyumbani kwetu. Lakini ghafla katika hali ambayo sikuitarajia akabadilisha maamuzi yake akanipa visingizio.
Baada ya muda mfupi kabla ya yeye kurejea kwenye makazi yake, nikamfumania akiwa na rafiki yangu wa karibu, rafiki niliye mchukulia kama ndugu yangu na kushare nae baadhi ya mambo.
Waliosalitiwa bila shaka wanaelewa uzito wa maumivu hayo. Ikabidi niwe mpole,na kuwaambia waendelee mbele,siku zilivosonga yule binti akaanza mambo ya dharau kwangu ila namshkuru Mungu nilipata moyo wa kumsamehe na kupuuza dharau zake.
Ilipofika mwezi wa 9 yule binti aliacha kazi kwa shari na kurudi kwao.
Sasa kilichonifanya nije hapa mbele yenu leo, nikwamba yule mwanaume anataka kurudi kwangu na mimi moyo wangu unakua mzito kumrudia, nimetokea kumchukia.
Jambo linalonisumbua zaidi kila ninapoanza mahusiano mapya hua nashindwa kuendelea mbele, hofu ya kwamba huyu atanifanyia kama yule inanijia mara kwa mara na matokeo yake nakua sababu ya kuvunjika uhusiano huo.
Wapendwa nifanye nini kukabiliana na hali hii ya pili? Ninatamani sana hali hii iniondoke. Karibu kwa mchango wako kimawazo.
Kwenye makosa ya kiuandishi mnisamehe maana natumia simu.