Kutema mate Bungeni

Inkoskaz

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
6,359
Reaction score
2,379
Bunge ni muhimili mmojawapo wa serkali na huitwa bunge tukufu
Vikao vya bunge huanza kwa dua na sala
Bunge huendeshwa kwa KANUNI
Kitendo cha Mwigulu Nchemba kutema mate wakati akitoa hoja yake kuashiria dharau juu ya anachokisema tena kukirudia mara mbili ni kulinajisi bunge..spika..ile fimbo ya bunge na taifa kwa ujumla
Viongozi wetu huchukua hatua haraka kwa vitendo vidogovidogo ikiwa vimetokea kwa wabunge wa upinzani
Pia wabunge wengi huomba "mwongozo wa spika" au "taarifa" kwa vitu visivyo na tija lakini hili lilitafsiriwa vipi? Kiongozi hakutoa karipio wala hakuna mbunge aliyeomba mwongozo
Inatufundisha nini wananchi na wanetu tunaoangalia vitendo hivyo?
Kile ni kitendo cha kunajisi bunge!
Bunge linalozuia baadhi ya mavazi..kauli nk lakini linaruhusu kutemewa mate?
Hata kiafya si sawa!!!

Msipowakemea na kuwapa stahiki yao wanajisi hao keshokutwa msishangae matendo ya ajabu zaidi
 
Last edited by a moderator:
picha itathibitisha zaidi..angalia uso wake na waombolezaji wengine....
kwa hisani ya michuzi.
http://1.bp.blogspot.com/-HWfIr1s6y2g/UrRUWkkH5EI/AAAAAAABdcc/XPO5m_MIYzQ/s1600/IMG_8095.J
PG

Duh...picture speaks louder!
 
Hamna ni malezi mabaya tu, tumsamehe bure maana nasikia pia ukifika mwezi mchanga ndo huwa anakuwa hivyo
Nyoka wenye sumu ndio huwa na tabia ya kuspit sasa sijajua mwenzetu ana tabia hizo za kinyokanyoka?
 
Sasa inanipasa kuionea huruma CCM kuliko,kwa kuwa na huyu jamaa km kiongozi wa kitaifa..Siku wanaamka watamkuta milembe ndipo watajiuliza CDM walishaona hayo kabla ya CCM wanayeishi naye.

So far CCM wataona huo uendawazimu wake km janja ya kuiua CDM.
 
Ni hatari kuliko waliolimwa panga jana
 
Kiukweli binafsi huwa najiuliza huyu MWIGULU MADELU NCHEMBA amefikaje hapo? maana kama ni akili anazo kidogo sana na hekima na busara hana kabisa! kifupi ni kwamba hajitambui.Yeye anaweza kusema chochote,mahali popote na bila kujiuliza hicho anacho fanya au kusema yeye binafsi kinamweka mahali gani katika jamii.
 
Si ajabu baada ya kitendo hicho kuna "mizigo" ilimpongeza nje ya bunge. Akapimwe labda kuna kiumbe kinakua tumboni mwake.

Wale book 7 lazima walimtumia message kumwambia yeye ndie jembe wa ukweli ndani ya ccm! akili dhaifu mbili zimekutana.book 7 umasikini ndio unao wafanya wafanye wasio yaamini ili mradi tu siku imeingia.mwigulu yeye hajitambui,something is wrong upstairs.
 
Kwanza ni uchafu wa hali ya juu yaani anatema mate ndani? Chini? Aibu I guess he does the same in his home

Ukitumia idea ya Ritz kuwa kuna "watu wa kawaida" utajua kuwa aliyetema mate aka mwanasiasa siyo mtu wa kawaida.

Kwa maana hiyo basi anaweza kufanya lolote including kutema mate bungeni kwa sababu nyie "watu wa kawaida" hamwezi kumfanyia chochote zaidi ya kumpigia tena kura kwenye uchaguzi ujao.

Nyie "watu wa kawaida" kazi yenu kwenye siasa ni kupiga kura tuu.

"Watu wa kawaida" wanaofanya usafi bungeni watadeki hayo mate yake. Shida iko wapi?
 
hili ni lichizi tulishawahi na tutaendelea kusema siku zote....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…