Kutapeliwa

N

Kila la kheri... Ila amini katika hili, lililo pangwa liwe lako utalipata na kama hukupangiwa basi mshukuru Mungu na amini utapata zaidi ya kile ulichopoteza... Good luck

Asante kwa kunipa moyo ndugu. Kama ipo ipo, na kama haikua riziki.... basi yote kheri. Tunashukuru kwa kila jambo.
 
hivi siku hizi kuna kusema nataka nikutumie mtandao fulani? hela toka NMB haiangalii mtandao. ila kama wameweza kusave NMB. kwenye cm hao ni ma PRO.

Kabsa aiseee, au rafiki yake nae kafanya maujanja?
 
Ame edit meseji ya benki akaongeza tarakimu!!huu mchezo tumechezeana sana kwenye upatu na washkaji zangu !!!
Mkuu wewe ndie umekuja na majibu sahihi, hapa ndipo mdau kapigiwa. Nampa pole sana
 
Asante kwa kunipa moyo ndugu. Kama ipo ipo, na kama haikua riziki.... basi yote kheri. Tunashukuru kwa kila jambo.
Hili la kusema ''jambo lililopangwa''au ''kama riziki haikuwa riziki haikuwa riziki'' au ''tushukuru kwa kila jambo'' ni misemo ya kijinga sana na haina nafasi kwenye karne ya leo. Hivi wewe unafikiri kuna kiumbe kilipanga utapeliwe? Umetapeliwa kwa sababu hukuwa makini. Wewe ulipatana kumuuzia hiyo bidhaa na yeye akulipe meseji au fedha? Inakuwaje unampa bidhaa baada ya kuona meseji na siyo fedha? Kama ilikuwa ni jioni basi ungemwambia mauziano yafanyike kesho yake na wewe ukishahakikisha fedha imeingia kwako ndiyo unampa bidhaa. Duniani kote wanakofanya biashara kwa njia ya mtandao huwa wanapeleka bidhaa baada ya kuhakikisha fedha zimeingia kwenye account zao na siyo meseji.
 

Ndo ishakua hivo sasa...nifanye tu utaratibu wa kusaka polisi. Thats the only option ilobakia
 
Ndo ishakua hivo sasa...nifanye tu utaratibu wa kusaka polisi. Thats the only option ilobakia
Ni jambo zuri kama utafuatilia kuliko kusema ''haikuwa riziki'' na kukata tamaa. Ila hata huko polisi uwe makini usije ukapoteza fedha zaidi na usipate chochote. Hawa matapeli wanakuwa wamejipanga sana na hizo namba wanazotumia nyingi zinakuwa na usajili fake. Usikubali kuwapa polisi fedha kiasi kikubwa. Na zaidi usikubali kwenda mganga wa kienyeji yeyote kama watu wanavyokushauri kwani huko nako ni matapeli tu.
 
Mkuu pole hapo umepigwa. Wametumia bulk SMS na kwenye jina la sender wameweka (NMB.)
Next time hakikisha salio linasoma ndo utoe bidhaa. Yaani kufanya hivyo naandika script ya mistari michache sana ya Python + Bulk SMS API yoyote faster kitu kinatumwa
 
Lakini Kuna Jambo nimekumbuka wiki mbili zilizopita nikiwa foleni NMB IRINGA aliingia Dada mmoja kutia hell ATM akafanya transaction akiomba na risit pesa haikutoka, ikatoka risit tu..ilikua saa moja jioni Dada wawatu akadata hataki kutoka kwenye mashine Hadi hela itoke...nikamuuliza km kwenye rist salio limepunguzwa jibu likawa nindio! Kuna muda huduma za bank zetu nazo nitatizo, je kwa wakala Hali ikoje? Sijawahi kuweka hell ndefu kwa wakala...yule Dada sijui walimalizana VP na mlinzi asiejua lolote kuhusu banking!
 
 
Hili la fedha kukataa kutoka na ikatoka risiti tu tena imeandikwa kuwa umetowa fedha huwa linatokea mara kwa mara. Hata mimi lilishanipata. Mwanzoni nilichanganyikiwa ila nilipoulizia benki wakanimbia kama fedha hazikutoka basi nisubiri kesho yake nione kama zimepungua kwenye account yangu. Mimi nilicheki muda ule ule na nikakuta hazijapungua. Limeshanipata kama mara tatu na muda wote fedha hazikupungua kwenye account yangu.
 
Mimi nilijua kuwa anakutumia pesa kwa Airtel Money.
Acount ya bank inatuma pesa mitandao yote ya simu kwa makato sawia. Pole.
Sasa hapo aliyepaswa kwenda bank kutoa ni wewe mwenye pesa au best yako mwenye line?.
Kuna simu ilidukuliwa na watoto wa Kinondoni na kisha kuongeza contact mpya ndio maana kuna kialama cha mtu kushoto.
Aliyepokea sms ndiye hakuwa makini.
 
Asante ndugu, Na mimi pia ndo wasiwasi wangu ukianzia hapo. Nilijaribu kuangalia hata message za tigo pesa ila sikuona hiyo nukta kwa mbele. Ikaniongezea mashaka zaidi
Polee we,na karibu ndani ya club ya wahanga wa MITANDAONI. Juzi nilileta uzi wa kujinjwa pesa kupitia tigo pesa wachangiaji wakaninanga saana. Jàmani haya mambo yanaweza kukutokea ukabaki unashangaa hasa baada ya kuibiwa. Pole tena Jamaa yangu.
 
Dah mkuu mimi jana nimefua suruali tatu nikaanika kama saa tatu usiku, nikalala maana hazikuwa zimekauka, nimeamka asubuhi hazipo, nimekuwa na uchungu mkali kwa suruali tu, sasa nakufikiria wewe, dah! Mtafute huyo ndugu yake uliyempa mzigo ule naye sahani, OVA
 
Mkuu pole sana umeshapigwa hela hapo,daah nilipigwa lake 3,nikaona nyingi kwa mtindo huo kumbe kuna watu wanapigwa mpk milioni.kua makini siku nyingine mkuu. Matapeli mjini ni wengi na husiamini mtu siku hizi
 
Hapa sasa ndo nimeelewa..
 
Vibaka sio watu wazuri..Pole sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…