Kutana na Dogo Genius

Red Scorpion

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2012
Posts
5,736
Reaction score
4,254
.KATIKA PITAPITA ZANGU NILIKUTANA NA HII YA HUYU DOGO IMENIFURAHISHA SANAA...!
Mtoto: Mwalimu mimi nataka nisome darasa la
nne kwani hili la3 halinifai.
Mwalimu: Kwa nini unasema hivo?
Mtoto: Nina akili...
Basi mwalimu kamueleza mkuu wa shule na
mkuu kaitisha interview kwa dogo.
Maswali ni haya....
Mwalimu: Kwenye ndege kuna matofali 20
tukitoa moja tukalidondosha chini yatabaki
mangapi?
Dogo: Yatabaki 19.
Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka tembo
kwenye friji.
Doo: Unafungua friji unamuweka tembo kisha
unafunga.
Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka nyani
kwenye friji.
Dogo: Unafungua friji unamtoa tembo
ulemuweka kisha unafunga friji.
Mwalimu: Kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa
kwa simba, wanyama wote wameenda kasoro
mmoja. Ni nani na kwa nini?
Dogo: Ni nyani kwa sababu tumemuweka
kwenye friji.
Mwalimu: Bibi kizee amevuka mto unaokuwaga
na mamba na viboko wakali, aliwezaje?
Dogo: Aliweza kwani mamba na viboko nao
walienda kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa
simba.
Mwalimu: Ingawa bibi kizee alivuka mto,
baadae alikufa. Unadhani kwa nini?
Dogo: Alidondokewa na lile tofali tulotoa
kwenye ndege na kutupa chini.
Mwalimu mkuu: Huyu dogo akasome chuo
kikuu....
 
Good good....dogo kaonesha how to think on past, present and future
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…