Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 3,520
- 6,503
Uvulana ni shida Sana!
Ilikuwa mida ya jioni muda ambao maji ya bahari huwa sometime yamejaa vizuri sana na kukufanya uvutiwe kuogelea. Ilikuwa kawaida yetu siku moja moja kupenda kuogelea na kuinjoy beach.
Ilikuwa miaka ya 1998/99 huko kivukoni maeneo ya Kigamboni, tukiwa watoto wa kota wa kile chuo ambacho kwa sasa kinaitwa Mwalimu Nyerere Memorial ila wakati ule kilikuwa kinajulikana kama chuo cha CCM Kivukoni. Kama unavyojua bahari ya Hindi iko karibu yetu kabisa, kwahiyo kuogelea siyo ishu kwetu kabisa.
Basi bwana siku ya kutaka kwenda kwa muumba wa mbingu na ardhi ilikuwa kama inani beep hivi. Kwa wale wakazi wa Kigamboni nadhani wanajua kuna ile minara ya kuongozea meli kuonyesha mipaka ya mwisho ambapo meli inatakiwa isiende nje ya hapo la sivyo yaweza kwenda nasa mchangani katika kina kidogo na huwa na taa nyekundu.
Sasa bwana kutokea ule upande wa kota zetu kuna mnara upo mbali kidogo kutoka nchi kavu na maji yakijaa ndiyo balaa zaidi. Basi bwana tukaweka ligi na mwamba mmoja tuende kwenye mnara na kupanda juu yake na kumpuzika kidogo na kurudi nchi kavu!
Dah sio poa kabisa, mwamba alikuwa anaenda sana ruti zile kwahiyo pumzi ya kutosha anayo. Sasa mimi bwana sikuwahi kwenda pande zile na kwa kukadiria ni kama mita 80 kutoka nchi kavu, na maji yamejaa kama yote. Kuhusu kuogelea niko vizuri lakini pumzi ikakata kama ilivyokata jana Kwa Mwakinyo! Sijui jamaa walijuaje kuwa mwamba pumzi ilikata, hilo nawaachia wao eti ndiyo maana mwamba akaona isiwe tabu ya nini kupigwa mbele ya dunia nzima wakati mpunga tayari ushasoma akaone isiwe kesi akachuchumaa!
Basi bwana pumzi ikakata na nishafika katika mnara bado kama mita tano tu niuguse na nipumzike! Dah kifo nakiona hiki hapa, unajua nilichoka mpaka maji sasa yamefikia kwenye kidevu yaani nanyanyua kidevu juu ili nisinywe maji. Nikaanza kukumbuka ndugu zangu, wazazi wangu na maisha yangu. Nilijua naondoka katika hii sayari ya dunia, na yule mwamba niliye kuwa naye yeye alishapanda juu ya mnara na kupumzika lakini baada ya kuona parapanda kama inaanza kulia hivi akajitosa kwenye maji na kuondoka.
Yaani alijua muda si mrefu nazama akaona hataki ushahidi ngoja asepe..
Tupate mambo yetu 🍿🍿🍿.
Naam, basi kama siku ya kuondoka haijafika aisee hauondoki ng'o, kumbe bwana kule nchi Kavu wadau walishaona bwege mimi nimeshazidiwa so ikahitajika back up kidogo. Huwezi amini alikuja dogo kama wa darasa la tano hivi na kidumu cha lita tano kuja kuniokoa. Kwahiyo mimi na yeye ndiyo tukakitumia hicho kidumu kwenda nchi kavu. Unajua ukiwa unajua kuogelea waeza hata kuokoka na mkungu wa ndizi kwasababu unachohitaji ni kujishikilia kidogo tu na ukaelea. Kiufupi hakika kweli Mungu yupo, ilikuwaje yule dogo apate ujasiri wa kuja na kile kidumu na kuniokoa sikupata majibu lakini nilijua Mola wangu ndio aliniokoa!
Kuanzia siku Ile ninayaheshimu maji, hata nikiogelea siwezi kwenda mbali kama sijafanya mazoezi ya kutosha! Nilitaka sifa kuonekana kuwa najua kuyakata maji kama kambale lakini mwisho wa siku ningerest in peace!
Wengine mnapenda sifa kuwang'oa warembo, wengine kuwa mnapiga pombe kali na mambo kama hayo, sifa zitawaponza mazee!
Ni hayo tu.
Ilikuwa mida ya jioni muda ambao maji ya bahari huwa sometime yamejaa vizuri sana na kukufanya uvutiwe kuogelea. Ilikuwa kawaida yetu siku moja moja kupenda kuogelea na kuinjoy beach.
Ilikuwa miaka ya 1998/99 huko kivukoni maeneo ya Kigamboni, tukiwa watoto wa kota wa kile chuo ambacho kwa sasa kinaitwa Mwalimu Nyerere Memorial ila wakati ule kilikuwa kinajulikana kama chuo cha CCM Kivukoni. Kama unavyojua bahari ya Hindi iko karibu yetu kabisa, kwahiyo kuogelea siyo ishu kwetu kabisa.
Basi bwana siku ya kutaka kwenda kwa muumba wa mbingu na ardhi ilikuwa kama inani beep hivi. Kwa wale wakazi wa Kigamboni nadhani wanajua kuna ile minara ya kuongozea meli kuonyesha mipaka ya mwisho ambapo meli inatakiwa isiende nje ya hapo la sivyo yaweza kwenda nasa mchangani katika kina kidogo na huwa na taa nyekundu.
Sasa bwana kutokea ule upande wa kota zetu kuna mnara upo mbali kidogo kutoka nchi kavu na maji yakijaa ndiyo balaa zaidi. Basi bwana tukaweka ligi na mwamba mmoja tuende kwenye mnara na kupanda juu yake na kumpuzika kidogo na kurudi nchi kavu!
Dah sio poa kabisa, mwamba alikuwa anaenda sana ruti zile kwahiyo pumzi ya kutosha anayo. Sasa mimi bwana sikuwahi kwenda pande zile na kwa kukadiria ni kama mita 80 kutoka nchi kavu, na maji yamejaa kama yote. Kuhusu kuogelea niko vizuri lakini pumzi ikakata kama ilivyokata jana Kwa Mwakinyo! Sijui jamaa walijuaje kuwa mwamba pumzi ilikata, hilo nawaachia wao eti ndiyo maana mwamba akaona isiwe tabu ya nini kupigwa mbele ya dunia nzima wakati mpunga tayari ushasoma akaone isiwe kesi akachuchumaa!
Basi bwana pumzi ikakata na nishafika katika mnara bado kama mita tano tu niuguse na nipumzike! Dah kifo nakiona hiki hapa, unajua nilichoka mpaka maji sasa yamefikia kwenye kidevu yaani nanyanyua kidevu juu ili nisinywe maji. Nikaanza kukumbuka ndugu zangu, wazazi wangu na maisha yangu. Nilijua naondoka katika hii sayari ya dunia, na yule mwamba niliye kuwa naye yeye alishapanda juu ya mnara na kupumzika lakini baada ya kuona parapanda kama inaanza kulia hivi akajitosa kwenye maji na kuondoka.
Yaani alijua muda si mrefu nazama akaona hataki ushahidi ngoja asepe..
Tupate mambo yetu 🍿🍿🍿.
Naam, basi kama siku ya kuondoka haijafika aisee hauondoki ng'o, kumbe bwana kule nchi Kavu wadau walishaona bwege mimi nimeshazidiwa so ikahitajika back up kidogo. Huwezi amini alikuja dogo kama wa darasa la tano hivi na kidumu cha lita tano kuja kuniokoa. Kwahiyo mimi na yeye ndiyo tukakitumia hicho kidumu kwenda nchi kavu. Unajua ukiwa unajua kuogelea waeza hata kuokoka na mkungu wa ndizi kwasababu unachohitaji ni kujishikilia kidogo tu na ukaelea. Kiufupi hakika kweli Mungu yupo, ilikuwaje yule dogo apate ujasiri wa kuja na kile kidumu na kuniokoa sikupata majibu lakini nilijua Mola wangu ndio aliniokoa!
Kuanzia siku Ile ninayaheshimu maji, hata nikiogelea siwezi kwenda mbali kama sijafanya mazoezi ya kutosha! Nilitaka sifa kuonekana kuwa najua kuyakata maji kama kambale lakini mwisho wa siku ningerest in peace!
Wengine mnapenda sifa kuwang'oa warembo, wengine kuwa mnapiga pombe kali na mambo kama hayo, sifa zitawaponza mazee!
Ni hayo tu.